MVUMBUZI
JF-Expert Member
- Jan 8, 2011
- 5,182
- 2,304
alichoongea Mh. Betrice Shelukindo kuhusu Sita niukweli mtupu aanze yeye kuwajibika kwakuwa swala la Richmond lilizimwa na Mh sita, sasa sahivi anageuka na kujifanya mzalendo kweli? huu ni usanii wa sita ambao utamfikisha pabaya. alijifanya anatetea chama kisidhalilike sasa ukweli unaanza kuwaumbua, walimkumbatia Lowassa na wenzake wakasahau ni sehemu ndogo sana katika taifa hili.
Ukiona marafiki wanaanza kufanyana kitoweo wao kwa wao ujue utu umetoweka na unyama na ubinafsi umeingia,. Kujikanyaga na kujichanganya kwa CCM hakuwezi puuzwa na wasoma alama za nyakati kuwa it's over. Leo uko huku kesho uko kule nani atakuelewa na lazima utaonekana umepwaya na huna msimamo na watu watasema hawa wanagombana wenyewe kwa wenye na '" SASA TUWANYANGANYE ILI WAKOSE WOTE" Huku ndiko tunakoelekea na tunamwomba Mungu ili CCM waendelee kujichanganya hadi watoto wadogo wawacheke na kuwadharau. Ukiona Mume anamkimbiza mkewe hadi mtaani ujue ndoa ilishavunjika siku nyingi na kilichoko hapo ni jina tu. Hivi ndivyo CCM ilivyo kwa sasa.