Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,198
- 7,539
yani haya mambo ya ajabu sana!waislam wamekuwa wakilaumu kwa kipindi kirefu kwamba si vyuoni tu bali serikalini kwa ujumla kuna upendeleo mkubwa kwa wakristo kuajiriwa huku wakitoa.data.hoja iliyotolewa na serikali na wakristo ni kwamba serikali huangalia uwezo na sifa na si dini katika kumpa mtu majukumu flani (hoja ambayo kimsingi mimi niliipenda kwa sababu ni ya kitaalam japo mimi ni muislam na si kuwa na kazi).saasa leo nashangaa sana ndugu zangu wakristo wakiibuka na kusema kwamba udom kuna udini mkubwa sababu wafanyakazi wake wengi ni waislam!.sasa pengine niulize maswali kadhaa anayeweza ajibu.je! ni sahihi taasisi flani ikiwa na watu wengi wa dini flani kusema ina udini?ni kweli kwamba watu wamekuwa wakiajiriwa nchini kwa sababu ya dini zao?je!ajira zinazozingatia udini zimeanzia udom?je!udini upo kwa waislam tu au hata wakristo?ikiwa udom kinazingatiwa kigezo cha udini kuajiri watu wasio na sifa kwa kuwa waislam wamekuwa wengi,je!maprofesa kama kikula pia walipata uprofessa kwa kuwa ni waislam? je!waalimu waliowafundisha maprofessa wa udom nao walikuwa waislam?kwa kuwa udsm nako watumishi wengi ni wakristo,je!wameajiriwa kwa kuwa ni wakristo! kama alie leta udini udom ni kikwete (kwa kuchagua viongozi wa chuo ambao ni waislam je nani aliyechagua na anaechagua viongozi wa udsm?ajab sana!Mwanzo tulianza na NSSF, watu wakapandwa jazba sana ila ndio ukweli wenyewe,
Now ni Udom,kiukweli chuo hicho kina udini sana angalia mawarden vilaza kutoka zanzibar wamejazana pale
bila hata qualification za maana!!Njoo kwenye depart ya finance My God utaimba haleluyah,kajaza ofisi nzima
masheikh!!Huyu prof uchwala mlacha ajiandae kwenda mahakama ya hague few years to come lol!!
hebu jaribu kuoanisha mambo kwa kutumia vigezo vya kitaalam kuliko hisia.vivi mfano mtu akikuambia ataajiriwa wizara ya fedha mwaka kesho halafu huyu mtu ni muislam,mwanaume,mpare,ana mke muhaya,ana masters ya utawala,ana ndugu yake anafanya kazi kilimo na sifa njingine mchanganyiko.je!ikitokea akiajiriwa kweli na wewe ukiju na moja kwa moja ukasema "jamaa kaajiriwa kwa sababu ni non-christian"unadhani hoja yako itakuwa ni ya kitaalam au ni emotional?iii) Hiki ni chuo ambacho non-christian anakuambia mwakani nataraji kuajiriwa UDOM na kweli akaajiriwa. Hiyo nayo ni nini? Taasisi gani ya UMMA ambayo mtu anaweza kupredict kuwa ataajiriwa nayo kama hajui chochote na kama taasisi hiyo itatangaza ajira?
iv) Unadai umefanya kazi na Prof na Dr amme ambae ni Director Graduate studies, kama hawa watu ni wachapakazi inakuwaje alieajiriwa kama mhadhiri msaidizi mwaka 2009 analingana mshahara na mhadhiri msaidizi alieajiriwa hata jana ama kesho alhamisi tarehe 1/11/2012? Nakuuliza tena hayo UDSM, SUA, MZUMBE , DUCE ama MUCE yanafanyika?
yani haya mambo ya ajabu sana!waislam wamekuwa wakilaumu kwa kipindi kirefu kwamba si vyuoni tu bali serikalini kwa ujumla kuna upendeleo mkubwa kwa wakristo kuajiriwa huku wakitoa.data.hoja iliyotolewa na serikali na wakristo ni kwamba serikali huangalia uwezo na sifa na si dini katika kumpa mtu majukumu flani (hoja ambayo kimsingi mimi niliipenda kwa sababu ni ya kitaalam japo mimi ni muislam na si kuwa na kazi).saasa leo nashangaa sana ndugu zangu wakristo wakiibuka na kusema kwamba udom kuna udini mkubwa sababu wafanyakazi wake wengi ni waislam!.sasa pengine niulize maswali kadhaa anayeweza ajibu.je! ni sahihi taasisi flani ikiwa na watu wengi wa dini flani kusema ina udini?ni kweli kwamba watu wamekuwa wakiajiriwa nchini kwa sababu ya dini zao?je!ajira zinazozingatia udini zimeanzia udom?je!udini upo kwa waislam tu au hata wakristo?ikiwa udom kinazingatiwa kigezo cha udini kuajiri watu wasio na sifa kwa kuwa waislam wamekuwa wengi,je!maprofesa kama kikula pia walipata uprofessa kwa kuwa ni waislam? je!waalimu waliowafundisha maprofessa wa udom nao walikuwa waislam?kwa kuwa udsm nako watumishi wengi ni wakristo,je!wameajiriwa kwa kuwa ni wakristo! kama alie leta udini udom ni kikwete (kwa kuchagua viongozi wa chuo ambao ni waislam je nani aliyechagua na anaechagua viongozi wa udsm?ajab sana!
Mkuu heshima mbele, kwa maelezo uliyoanza nayo hapo juu inaonekana nawe ni muhadhiri au upo karibu na fani hiyo (samahani kama nimekosea). Katika maelezo yako mareeeefu, nasikitika kusema hujaweza kujenga hoja ya kushawishi (kama ni muhadiri, jamii inategemea zaidi ya hapo). Angalau kwenye mistari niliyoweka rangi ya blue kuna mantiki umeongea lakini ulipofika nilipoweka rangi nyekundu ukaamua kutumia masaburi kujenga fikra zako..... Mbona mnasema daladala kwanini msizitumie nasikia zipo dala dala za UDOM nyingi tu. Kwani sera zinasemaje kuhusu kupewa Nyumba? Nchi inafuata utaratibu wa kutibiwa kwa bima, au ndio ninyi wa UDOM tu mnataka kutibiwa bure jamani?. Kama kweli Dept. ya fedha ni waisilimu watupu basi nawapongeza. Maana ndio hao hao ambao waliowafanyia mipango mizuri ya kuishi vizuri, kwani nasikia ni Chuo Kikubwa na kizuri sana. Kwa hiyo Bursar wenu na timu yake inafanya kazi vizuri hadi kufikia kuongeza idadi ya wanafunzi na walimu. Mafanikio bwana ni mipango mizuri ya hawa mabwana.
Jichunguzeni, Bunge lilianza Jana. Au wakuu wa Chadema waliwafikia na kuwapandikiza kitu na ndipo mmeanza?. Eti walimu wanaacha kazi n... kwani waliopo hapo walipotoka si waliacha kazi kwingine na kuja UDOM. Huyo Nowe si aliacha Chuo sijui SUA na kuja UDOM?.
Waislam nchi hii ya Udom washakuwa kero kero! Kumbe hadi ninyi waalim mwapata shida? Nkajua sie wanafunzi tu bwana. Hlo la maprof kuondoka limetuathiri weng cuz wametuondolea prof Nwoye wetu! Sasa jamani kitumbo buku 2 per day afu migari yenyewe ile ka mapango ya panya inawezekana kweli? They are so unfair to u jamani! Wanakusanya hela za kampeni za ccm 2015 kwa migongo yenu? Mkiyakubali hayo bs mjue mmekwisha! Yeye mlacha, kikula na wengneo hayo magari SU wanalipia how much? Wao kwanza ndo wangetakiwa walipe house alowance cuz wana hela ndefu! Yaani ktk hayo mtakayosimamia kugoma, basi gomeni mpaka kieleweke, ikibidi wafunge mchuo wao bhana. Nimegundua nyie mnanyanyaswa hvo afu hasira mnatumalizia sisi kwa kutukong'oli SUP na makarai sio? NAWAOMBEA USHINDI, HAO PIMBI WAZEE WAONDOKE CUZ WASHAKUWA KERO!!
Wasomi wenzangu, je hamjui namna ya kufuatilia matatizo yenu kwa njia sahihi? Kwani migomo ndio inayotatua?. Mbona ni suala dogo tu?. Kama mnashida fulani mfano ya kifedha inavyoonekana sehemu kubwa ya mada yenu ya mgomo, ni vema mkatuma wawakilishi kuanzia ngazi ya idara kama mnayo and then faculty na baadae ngazi ya chuo na ikishindikana sehemu husika mfano hazina kama mnavyosema na sio kwa Mh. Pinda au sijui kuilaumu CCM sijui na kulaumu mtu binafsi kama Misilamu au Mkristo fulani au Mzanzibar ???????.
Tukio hili kwanza limechochewa na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Balozi Mwapachu, wiki iliyopita kwenye baraza la chuo alimtukana Mwenyekiti wa jumuiya ya wahadhiri kwa kumuita Mugabe kwa sababu hataki kuitisha uchaguzi. Na akaamuru kikao kijacho asiingie kama uchaguzi hamna. [Tunaamini wana mpango wa kupandikiza mtu wao]
.....
2. Kwenye baraza la chuo, walitangaziwa Prof. Shaban Mlacha ameongezewa miaka minne na Raisi Jakaya Kikwete. Wahadhiri wanahoji mgomo wa mwaka jana,wa walimu na wanafunzi,waziri Mkuu Mizengo Pinda aliahidi atarudi kuja kutoa ufafanuzi hatua zilizofikiwa na serikali, hajarudi, wala ripoti ya tume alizounda haijatolewa, manunguniko ya wafanyakazi, na wanafunzi hayajafanyiwa kazi kabisa. Hili limesababisha wastani wa wafanyakazi watatu wakiwemo Prof. na madaktari huacha kazi kila mwezi. Kuanzia July 2011, hadi July 2012, jumla ya wafanyakazi 42 wameondoka chuo kwa sababu mbalimbali ikiwemo kuacha kazi (resignation). Mbaya zaidi kumekuwa na ulipizwaji kisasi wa hali ya juu. Wahadhiri wamefukuzwa sana kazi, na baadhi ya kesi zipo mahakamani. Kibaya zaidi imethibitika kikwete kawaongezea muda viongozi wote wa chuo. Prof. Kikula alistaafu 15 December 2012, ameongezewa nae mkataba, pamoja na lawama zote. Hili wamelichukulia kama Serikali haiwajibiki na imeonyesha dharau kubwa sana, lakini kibaya zaidi hili limechukuliwa kwenye taswira ya Udini, ambao umekuwa ukikitafuna chuo, kufikia hatua ya kuunda kamati ya kushughulikia suala hilo, ambayo pia inasemekana *ilivunjika bila mafanikio kabla hata ya kuanza kazi.
Ndugu mleta mada! Pole kwa kutumia muda mwingi kuandika hii habari kwenye ukurasa huu kwa faida ambayo mimi bado sijaijua bado, na kama wewe ulitumwa na hicho kikao uje hapa JF uelezee azimio hilo au la sijajua bado, kama ndivyo basi nina mashaka na uelewa wa wajumbe wa hicho kikao. Turudi kwenye point zako ulizotoa.
Kwanza kabisa umesema mwenyekiti wa baraza la chuo ALIMTUKANA KIONGOZI WA UDOMASA KWA KUMUITA MUGABE ,Hivi unataka kuaminisha wanajukwaa kuwa Mugabe ni tusi??, Je ni tusi la kabila gani, kwa maana ktk misamiati ya matusi ya Kiswahili halipo. Kama huyo kiongozi alichaguliwa na wajumbe, na muda wake umekwisha taratibu si zinasema uchaguzi unabidi ufanyike? Ni imani yangu kuwa katiba yenu inaelekeza hivyo, sasa kama hakuna maelezo yenye mantiki ya kwa nini hajaitisha uchaguzi huoni kuwa mwenyekiti wa baraza la chuo ana kila sababu ya kuhimiza hilo lifanyike?? Kwa nini aamini kuwa yeye ndiyo kiongozi pekee mwenye uwezo wa kuongoza hiyo jumuiya? Huoni kuwa hilo ni tatizo??? Unataka kuniambia kuwa hao wahadhiri watagoma kwa kuwa kiongozi wao kaitwa Mugabe????
Suala la chuo kuletewa pesa kidogo kutoka serikalini hivyo kulazimisha kufanya cost sharing. Hembu tuwe wazalendo jamani, hivi vitu tujaribu kuviown!. Sasa kama Chuo kinapokea hela kidogo kutoka serikalini, mnatarajia pesa ya kugharamia hizo huduma zitatoka wapi??. Wewe kama mwalimu umetumia elimu yako kwa kiasi gani kukiingizia chuo kipato. Mimi nafahamu kuwa mwalimu unatakiwa uandike miradi na ufanye consultancy cervices, ambazo malipo yake partly yanaingia chuoni na kiasi kidogo unapata wewe, sasa kweli university lecturer unakaa unataka kugoma kwa sababu ya kuondolewa sh 500?? Kwa sababu zinazojulikana. Hata kama hamjapenda hilo suala haliwezi kuwa linacall for mgomo, ni suala linalovumilika wakati majadiliano na njia nyingine za kulitatua zinaendelea.
Kama Mlacha na hao wenzake wameongezewa mkataba tatizo ni nini? Kwani tatizo ni dini yake au ni utendaji wake wewe hujaupenda? Je unafikiri akiletwa mkristo tatizo unaloliona kwa mlacha hutoliona tena, au akisha kuwa mkristo tayar wewe uko happy??. Na unatuambia kuwa kuendelea kwa uwepo wa mlacha na wenzake kumefanya maprof na ma Dr kuacha kazi, mimi ninawasiwasi na elimu za hao walioacha kazi kwa hizo sababu!! Au walitarajia wangeteuliwa wao? Huo utakuwa ni ubinafsi uliokithiri!
Hivi unataka kutuaminisha kuwa, waajiriwa wengi hapo udom ni waislam, na hao hao waislam kwa wingi wao ndo wameadhimia kwenye hicho kikao chenu kumuondoa mlacha kwa sababu kuna uislamu sana hapo mahali????. Unajua mimi nawashauri kama mnataka mfanikiwe kwenye mambo yenu ya msingi hili suala la Udini msilizungumze kabisa, kwa maana linawagawa ninyi kwa ninyi kuwa ktk makundi mawili yenye interest tofauti, tumieni elimu zenu vizur kupambanua mambo.
Suala la kupunjwa mishahara na kuchelewa kupanda vyeo ni jambo ambalo halihitaji mgomo, mnaweza kutumia majadiliano na uongozi wa chuo mkishirikiana na watu wa hazina ili muone kuwa tatizo ni Mlacha ndiye hataki mpandishwe vyeo au ni nini? Hi indo namna ya kutatua mambo. Unapokuwa na Mtazamo hasi dhidi ya mtu matokeo yake ndo haya.
Malalamiko hapo juu hayana uhusiano wowote na dini ya watu. Huyo Prof. Kikula ametumikia kama Director IRA pale UDSM, akaenda ARU/UCLAS kama Principal mbona hajawahi kulalamikiwa kuwa ni mwislamu? hata Juma Mwabachu ana CV kubwa sana lakini kwa sababu tu amekuja UDOM basi ni mwislam. JAMANI ACHENI HIZO BIASNESS ZA UDINI, unless una evidency ya jambo lililofanyika la udini - mwandishi unapotosha umma.
hizo nafasi za juu kuna akina Mkapa, mbona hawatajwi? DVC academic ambaye anaajiri waalimu ni mkristo mbona hatajwi? acheni KUPOTOSHA jamani. unataka kusema kuna mwalimu alishindwa kuajiriwa akiwa na sifa kwa sababu ni mkristo?
I think watu walio nje ya udom wanaweza kujudge vyovyote wapendavyo bt ambao wamevivaa viatu wanajua vinapoumiza! Waislam kuwepo udom sio shida...tatizo qualification zao hasa hao malecturer wa kizenji! Wako shalow ktk ufundishaji, hawana confidence yaani wanaboronga mbaya! Nasapoti kikao endelevu kiwepo kuanzia kesho pale chimwaga....mpaka kieleweke jameni!