Mgomo wa wafanyabiashara nchi nzima kesho

Mgomo wa wafanyabiashara nchi nzima kesho

Huyu si ni mwenyekiti wa wafanyabiashara Kariakoo,sasa kwanini nchi nzima tugome?wagome hao hao wa Kariakoo

Ni mwenyekiri wa wafanyabiashara tanzania nzima. Kama hukujua tambua hilo na ni mtetezi mkuu wa wafanyabuashara wafanyabiashara kuona umuhimu wa huyu bwana ndio maana wanahamasishana kufunga biashara siku ya kesi yake ambayo ni kesho.
 
Kuna ujumbe unasambazwa na wafanyabiashara kufunga biashara nchi nzima kesho. Ujumbe huo ni huu hapa "Breaking News,tarehe 11/02/2015, M/kiti wa wafanyabiashara anapandishwa kizimbani, kwa hiyo wafanyabiashara wote wanatakiwa kufunga biashara zao zote, pamoja na magari kutofanya safari zake yale ya safari ndefu na fupi.TANGAZO HILI NI MHIMU, mrushie mwenzio..." My take: Serikali kwanini haiwasikilizi wafanyabiashara na kutatua matatizo yao? Wafanyabiashara wakifunga maduka nchi nzima serikali itaingia hasara ya shilingi ngapi? Kazi kwenu wadau, nawasilisha.
wagome tu, tumechoka.
 
huu ni upumbavu wa hali ya juu yaani wafanyabiara hamtaki kulipa kodi!
nchi itaendaje??
 
Serikali kwa hili imejitahidi sana kuwa wavumilivu, wafanyabiashara hawa hawa huko nyuma walikuwa wanalalamika kuwa wanakadiliwa kodi kienyeji na hivyo wanalazimika kutumia hongo ili wasilipe kiasi kilichokadiriwa na kuwa baadhi ya wakadiriaji - yaani TRA walikuwa wanawakadiria kiasi kikubwa kuliko kiasi halisi ili wahongwe.

Sasa serikali imekuja na utaratibu wa kutumia efd machines ambazo zinaonyesha mwenendo mzima wa biashara husika ili kodi ipasayo kulipwa iwe wazi wao wanalalamika tena, hapa ni dhahiri wamezoea kukwepa kodi ndio maana wanalalamika.

Tuweni wazalendo kama ni kulalamikia kodi kuwa kubwa tufuate taratibu ili mfumo wa kodi kwa ujumla ushuke na tushirikiane na serikali kuwalipua wenzetu wanaokwepa kodi badala ya kugomea efd machines.

Mimi kama mfanyakazi ninalipa kodi ipasayo ingawa tumekuwa tukilalamikia mfumo wa kodi ambao unatukamua kiasi cha kutufanya tushindwe kuishi kwa mwezi kwa kuitegemea hiyo 'take home' na pia tunapata taabu sana kukubali kulipa kodi bila shuruti kwa sababu tunaona kodi haituridii kabisa.

Huduma za jamii ni duni pale ambapo zipo na elimu kwa watoto wetu ni hovyo kabisa licha ya kwamba bado nazo kwa uhalisia tunalipia ingawa serikali inajifaragua kuwa ni bure. Muulize mzazi aliyepeleka mtoto wake kidato cha kwanza leo kwenye shule ya kata amelipa shilingi ngapi - shule zingine ni hadi shs 400,000/= kwa jina la michango.

Barabara tunajenga kwa fedha ya kodi ya ziada ya kwenye mafuta, na mikopo kutoka nchi za nje na ndani kwenye taasisi za fedha na kibaya zaidi hadi kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii ambazo ilikusudiwa kumsaidia mfanyakazi aliyepigika kwa kodi ili astaafu vizuri.

Tushirikiane kuikatta serikali hii ya CCM iliyotufikisha hapa tulipo kuliko tukiendekeza utaratibu huu wa kila mmoja kwa mabavu aliyonayo kuinuka na kufanya migomo ya kulipa kodi hatutafika popote, na nina imani kabisa hawa wafanyabiashara wanaendekezwa na serikali hii kwa sababu biashara nyingi ni za wakubwa hawa hawa wa serikali.

Twende pamoja watanzania wenzangu kila kundi limuonne huruma mwingine kama ambavyo mfanyabiashara mmoja alivyowahi kuteta nami kuwa kwa kweli hata yeye anatuonea huruma sisi wafanyakazi kwani hatuna hata namna ya kukwepa kulipa kodi kutoka kwenye mapato yetu ya mishahara, kwa maana akiwa anakiri kuwa wao wana namna au mianya fulani wanaweza kutumoa kukwepa kodi kiasi fulani.

Serikali ikitumia vizuri kodi za wananchi na ikaonekana ikiwarudia kama ilivyo kwenye nchi za wenzetu huko ulaya hakutakuwa na shida yote hii ya kutumia nguvu nyingi kupata kodi stahili, lakini kwa haya tuyaonayo machoni mwetu ya kodi zetu kutumika hovyo hayatupi motisha sisi wananchi kulipo kodi kwa hiyari.
 
Hawa ni wajinga sana, suala lao liko very clear, serikali imewafafanulia sana misingi ya uwekaji kumbukumbu za kodi na jinsi ya kukokotoa, lakini wanaonekana wana lao jambo. Wengi hawajasoma shule kabisa wanafuata mkumbo tu mimi naona sasa WAPIGWE TU
Very interesting!
Unadhani ni kwa nini hawakusoma shule!?
Na je, waliosoma unadhani ni kwa nini wameshindwa kuanzisha biashara na kuishia kuajiriwa!?

Kuna hoja hapa. Serikali ikitaka kushirikiana na watu ambao inadhani 'hawajasoma' ishirikiane nao kama 'wasiosoma' badala ya kuwalazimisha mawazo ya 'kisomi' huku ikijua hawajasoma. Lakini pia hawa waliomo serikalini wao 'walisoma' lini!? maana nao wamezaliwa na kuwepo katika nchi hii hii iliyojawa watu wenye vyeti vya bandia na kuingizana makazini kwa kujuana.

 
Hivi kwa nini mfanya biashara atumie mtaji wake kununua mashine? Huwa sielewi. Hajaomba hiyo mashine. Mwenye shida nayo ni TRA, inamlazimisha mfanyabiashara aisaidie kununua! TRA kama mnawalazimasha wafanya biashara kwakopesha hizo mashine, zinunueni toka kwao kwa riba ambayo wafanyabiashara wataamua ninginevyo nunua mashine za kwenu na sambaza nchi nzima muhowahold responsible kwa kutozitumia. Ubabe kwenye mitaji yao hausaidii !!!!:A S-confused1:
 
achaneni na majungu biashara ni yako suala la kuanza kukusanyana na kutaka kugoma is a rubbissh kama unaona biashara hailipi close your shop na kafanye mambo mengine yatakayokufaisha kuliko kutuletea vurugu. mkitaka kuona mnafanya ujinga acheni vibanda vyenu uone watanzania wengine watiifu watalipa kodi na kufanya biashara kwa uaminifu na uadilifu. tumechoka tunataka tusikie creative idea za kimaendeleo. my brother if u cant do others will, give us the facillities including premises we will, we are tired of you!!!! shame on you!!!

Umechoka na nani? Jinga kabisa! Kwanza wewe sio mfanyabiashara.
 
Mnaochangia hii hoja nakuwaponda wafanyabiashara mmewahifanya biashara? Vimekaliwa vikao vingi kutatua jambo hili utekelezaji wake nishida.

Yaani na Rizzy Mokko afunge shelli zake magari yasipate wese...haiwezekani!
 
ingekuwa china huyo mwenyekiti ashakula kitanzi zamani sana,huwezi gomesha watu kulipa kodi serikali bado iwe inakupet pet
 
Nafikiri hapa kuna utata. Kwa mujibu wa sheria ya sasa ya kodi ya mapato, kodi inakatwa kutokana na mauzo ghafi(gross sales).Hii ina kikomo kwenye shilingi milioni 20. Zaidi ya hayo mauzo ya shilingi milioni 20 kwa mwaka kodi inakatwa kutokana na faida na lazima mahesabu
yaliyokaguliwa yafanywe. EFD inarekodi mauzo ghafi na kodi ya ongezeko la thamani(VAT). Hapo mwanzo wafanya biashara waliifanya
asilimia 18% ya VAT kama faida yao, sasa wanashindwa kuiacha..
Jamani mfumo Wa kodi haumlazimishi mfanyabiashara kulipa kodi kutoka sales turnover kama atakuwa anakumbukumbu za biashara yake na mhasibu(CPA) amekagua na kudhibitisha atalipa kodi kwa tax rate
 
Wafanyabiashara hawakatai efd bali wanakataa mfumo wa efd. Efd inakata kodi kutoka kwenye mauzo haiangalii umepata faida kiasi gan. Efd haiingizai matumizi, kodi inatakiwa ikatwe kwenye faida na sio mauzo. Sasa hivi wafanyabiashara wanaambiwa walipe mapato mara mbili ya yale waliolipa mwaka jana. Wanatumia vigezo gani kupandisha mapato kiasi hicho? Huu ni unyonyaji kwa watz na sio kwa mfanyabiashara tu. Mlaji wa mwisho ndiye anaeumia zaidi kwa hiyo hili swala linamgusa kila mtz

kWA SHERIA GANI KODI INAKATWA KWENYE MAUZO? NI KODI GANI MAANA KAMA NI VAT LAZIMA IKATWE KWENYE MAUZO? FANYENI BIASHARA KWA UADIRIFU HACHENI UBABAISHAJI, MNASABABISHA WAFANYAKAZI WANALIPA KODI KUBWA KWA KUWA NYINYI HAMTAKI KULIPA KODI. UNAKUTA MTU ANA KIBANDA KARIAKOO ANAUZA MPAKA MILIONI MOJA LAKINI KWENYE VITABU ANAANDIKA LAKI MBILI.

LIPENI KODI NCHI IENDELEE, BILA KODI NCHI HAIWEZI KUENDELEA
 
Jamani mfumo Wa kodi haumlazimishi mfanyabiashara kulipa kodi kutoka sales turnover kama atakuwa anakumbukumbu za biashara yake na mhasibu(CPA) amekagua na kudhibitisha atalipa kodi kwa tax rate

Mkuu hawa wanatufanya watanzania hatujui kuwa wanaongoza kwa kukwepa kodi, hakuna sheria inayosema ulipe kwenye mauzo, kodi ya mapato waweke hesabu zao vizuri walipe bila kukadiliwa, wanaficha hesabu zao ndio maana wanakadiliwa na kulazimisha kulipa hicho kiasi ambacho ni kidogo pia, utakuta mtu ana duka anuza milioni mbili siku moja kodi ni 84,600.00 kwa miezi mitatu, na hii inasababishwa na wao kutoweka kumbukumbu zao za mauzo na manunuzi.

Walipe tu kodi maana hii nchi ni yao na lazima waiendeleze, kama hawataki waende wakalime waone kuwa kulima ni kazi ngumu kuliko biashara za kijanja janja
 
Hivi kwa nini mfanya biashara atumie mtaji wake kununua mashine? Huwa sielewi. Hajaomba hiyo mashine. Mwenye shida nayo ni TRA, inamlazimisha mfanyabiashara aisaidie kununua! TRA kama mnawalazimasha wafanya biashara kwakopesha hizo mashine, zinunueni toka kwao kwa riba ambayo wafanyabiashara wataamua ninginevyo nunua mashine za kwenu na sambaza nchi nzima muhowahold responsible kwa kutozitumia. Ubabe kwenye mitaji yao hausaidii !!!!:A S-confused1:

Mashine TRA ndio wananunua, pesa unayotumia si unaikata kwenye kodi unayotakiwa kulipa? lipeni kodi nchi iendelee, bila nyinyi mnafikiri maendeleo yatakuja na nini?
 
Hawa ni wajinga sana, suala lao liko very clear, serikali imewafafanulia sana misingi ya uwekaji kumbukumbu za kodi na jinsi ya kukokotoa, lakini wanaonekana wana lao jambo. Wengi hawajasoma shule kabisa wanafuata mkumbo tu mimi naona sasa WAPIGWE TU
Umetisha sana! Wanafanya biashara lakini hawajasoma kabisa!! Nadhani wewe siyo mfanyabiashara,hivyo hujui chochote kuhusu biashara!! Hii issue haikuhusu waachie wenyewe!!
We! Jamaa au ndo wale wale wa TRA?
 
Wafanyabiashara hawakatai efd bali wanakataa mfumo wa efd. Efd inakata kodi kutoka kwenye mauzo haiangalii umepata faida kiasi gan. Efd haiingizai matumizi, kodi inatakiwa ikatwe kwenye faida na sio mauzo. Sasa hivi wafanyabiashara wanaambiwa walipe mapato mara mbili ya yale waliolipa mwaka jana. Wanatumia vigezo gani kupandisha mapato kiasi hicho? Huu ni unyonyaji kwa watz na sio kwa mfanyabiashara tu. Mlaji wa mwisho ndiye anaeumia zaidi kwa hiyo hili swala linamgusa kila mtz
Lipeni kodi axheni visingiZio
 
Ninyi mnaojiita wasomi ndo watu mabwege zaidi mnaofanya nchi hii iendelee kuwa maskini.
Kama kweli ninyi ni wasomi mngefanya utafiti kujua nini chanzo cha mgomo.
Msidhan wafanyabiashara wote ni mambumbu.Huyo mwenyekiti wetu ni msomi na anao weledi mkubwa kwenye mambo yahusuyo kodi.Tafuta taarifa zake utazipata.
Hatupend kukwepa kulipa kodi bali mfumo unatulazimisha kufanya hivyo.
Kwa mfano pale bandarini kuna mawakala wamewekwa na tra.Unaweza ukaambiwa kulipia kontena ni mil 40 na ukitaka kwenda kulipa mwenyewe dirishan au benk hawataki na ukilazimisha kontena lako litakuguliwa mara kumi zaid na fain kibao hata kama ulifuata taratibu zote.
Ukiwapa madalali ml 40 watakupa risiti ya ml 10 kontena lako litapelekwa na wao hadi unapotaka lifike.
Hakika nchi hii ina watu wapumbavu ambao hushabikia tu kuwa wafanyabiashara hawataki kulipa kodi bila kujua madhila yanayowapata.
 
achaneni na majungu biashara ni yako suala la kuanza kukusanyana na kutaka kugoma is a rubbissh kama unaona biashara hailipi close your shop na kafanye mambo mengine yatakayokufaisha kuliko kutuletea vurugu. mkitaka kuona mnafanya ujinga acheni vibanda vyenu uone watanzania wengine watiifu watalipa kodi na kufanya biashara kwa uaminifu na uadilifu. tumechoka tunataka tusikie creative idea za kimaendeleo. my brother if u cant do others will, give us the facillities including premises we will, we are tired of you!!!! shame on you!!!

Wkt mwingine bora kukaa kimya,usome tu post za wenzako kuficha ujinga wako.
 
Back
Top Bottom