Mgomo wa wafanyabiashara nchi nzima kesho

Mgomo wa wafanyabiashara nchi nzima kesho

wafanyabiashara wanalipa kodi vizuri tu ila ninacho kiona ni kwamba wanapinga kodi kandamizi. Ambazo hazita muadhiri sana mfanyabiashara kwani yeye atapandisha bei na ataye adhirika zaidi na hili ni mlaji wa mwisho ambaye ni ww na mm na ndugu zetu ambao wapo kijijini huko

mfumo wa efd unatumika nchi nyingi duniani...unayeona kodi kandamizi hujui mfumo wa kidunia unavyofanya kazi.
 
Kodi za gesi na madini kama dhahabu,tanzanite,almas na mengine mengi hatujawai ambiwA zimeingizia nchi faida ,hakuna uwazi ktka mambo hayo yenye utajiri wa nchi yetu.leo serkari wanaacha kuangalia vianzo hvo,wanabaki kulazmisha wafanyabiashara knunua efd, viongozi wa nchi nyngi africa ni majuha ,sio wabunifu hata kidogo, mbona china hakuna efd lakini nch inatajirika sana,...serkari weka mapato ya resource alizotupa Mungu tukiridhika ndy mutushawishi efd ni nini na ina manufaa gani!

Labda si vibaya EFD zikafungwa katika migodi yote!!!
 
Nafikiri hapa kuna utata. Kwa mujibu wa sheria ya sasa ya kodi ya mapato, kodi inakatwa kutokana na mauzo ghafi(gross sales).Hii ina kikomo kwenye shilingi milioni 20. Zaidi ya hayo mauzo ya shilingi milioni 20 kwa mwaka kodi inakatwa kutokana na faida na lazima mahesabu
yaliyokaguliwa yafanywe. EFD inarekodi mauzo ghafi na kodi ya ongezeko la thamani(VAT). Hapo mwanzo wafanya biashara waliifanya
asilimia 18% ya VAT kama faida yao, sasa wanashindwa kuiacha..

Zamani nilisikia mzunguko wa milioni14 ndio unatakiwa upate mashine lakini hapa umeanndika milioni20. Kiufupi huu ni mzunguko wa chini sana kwa mwaka na itabidi hata wauza magenge na pweza wawe wanatumia hizi mashine.

Ni nchi ya majuha, ukusanyaji kodi ni sample sana kama seikal inajipanga vizur:
Kwa mfano unapoanza biashara unatakiwa uwe na PIN hii ndio inayokutambulisha ulipaji wako wa kodi kama serikali itawaamulia wafanyabiashara wote wa Nguo kodi yao ni moja tuu ambao wabauza rejareja na hii unatakiwa uambiwe pale ukienda kuchukua tin no.

Mfano huo utolewe na kwa wafanyabiara wote wengine tofauti bila ya kuvutana kama nchi nyingine. .
 
Wakati mnaishinikiza serikali kuzikubali hoja zenu tumieni muda huu kuhamasishana kutoipigia kura ccm, hii ni golden chance kwenu
Umesema kweli, haiwezekani watu waonewe na bado mnyonyaji mnamkumbatia.
Tupia mbali ccm na wajinga wake
 
Kuna ujumbe unasambazwa na wafanyabiashara kufunga biashara nchi nzima kesho. Ujumbe huo ni huu hapa

"Breaking News,tarehe 11/02/2015, M/kiti wa wafanyabiashara anapandishwa kizimbani, kwa hiyo wafanyabiashara wote wanatakiwa kufunga biashara zao zote, pamoja na magari kutofanya safari zake yale ya safari ndefu na fupi.TANGAZO HILI NI MHIMU, mrushie mwenzio..."

My take: Serikali kwanini haiwasikilizi wafanyabiashara na kutatua matatizo yao? Wafanyabiashara wakifunga maduka nchi nzima serikali itaingia hasara ya shilingi ngapi?

Kazi kwenu wadau, nawasilisha
.

Ndio na wewe umetumwa kusambaza ujumbe? Basi lipia tangazo, ovyo kabisa!
 
Wafanyabiashara hawakatai efd bali wanakataa mfumo wa efd. Efd inakata kodi kutoka kwenye mauzo haiangalii umepata faida kiasi gan. Efd haiingizai matumizi, kodi inatakiwa ikatwe kwenye faida na sio mauzo. Sasa hivi wafanyabiashara wanaambiwa walipe mapato mara mbili ya yale waliolipa mwaka jana. Wanatumia vigezo gani kupandisha mapato kiasi hicho? Huu ni unyonyaji kwa watz na sio kwa mfanyabiashara tu. Mlaji wa mwisho ndiye anaeumia zaidi kwa hiyo hili swala linamgusa kila mtz

Wafanyakazi wanakatwa kwa % ya kipato, swala la matumizi ni lako, let's be serious watu walipe kodi, na siye wa kwenye payroll ya serikalini tupate ahueni! wafanyabiashara tusiwachekee, walipe kodi, EFD zipo nchi nyingi tuu, tuzizoee vya kunyonga.
 
Kwani wafanyabiashara wanapoenda kwa mkulima wao wanachoangalia wanapata nini na sio mkulima anapata nini so mashine za efd ni LAZIMA..!!
 
Mashine zenyewe network hakuna, mi ni biz Kama kawa.., siwez kuacha mihela iende hivi hivi..
 
sasa faida inatotolewa vp?na mbona kenya na Kilimanjaro wafanyabiashara hawajapinga? kama biashara yako haitengenezi faida si unaiacha na kufanya kitu kingine? kila mnachouza lazma kikatwe kodi hata kama ni pipi kila inayouzwa lazma sumni itoke! Wapuuzi sana wafanyabisahara wa nchi hii, tumewachoka!
Usiite watu wapuuzi,
Wewe ni nani mpaka kufikia kutukana wafanyabiashara?
 
Naunga mkono mgomo,kwan hata kodi ikilipwa kwa usahihi mafisadi ccm yanatafuna.
 
Utam wa ngoma ingia ucheze hata walim wanapofanya migomo tunawapuuza hivyohivyo. Na ndio tunaona elimu yetu sasa ilipo. Mm binafsi sio mfanya biashara ila nimekuwa nifuatilia hili swala hili kwa karibu kwani kuna jamaa zangu wanafanya biashara na nikaona madai yao yanaukweli ndani yake. Katika nchi hii hakujawahi tokea mgomao wa wafanya biashara kabla ya mfumo wa efd, na kodi zilikuwa zinalipwa bila shaka na serikali ilipata mapato vizuri kabisa. Kwa nn serikali isirekebishe mfumo wa efd uendane na matakwa wanayotaka wafanyabiashara

Si bure, wewe ni mmoja wa wanaosambaza ujumbe huu, kutokana na coments zako, usiwe mjinga kiasi hiki, we kama biasahara imekushinda,funga masulupwete yako uwaachie wafanyabiashara waadilifu wafanye biashara, usijitie mjanja et we sio mfanyabiashara! Mchochezi mkubwa we.
 
Usiite watu wapuuzi,
Wewe ni nani mpaka kufikia kutukana wafanyabiashara?


Mkuu hata usiumize kichwa nimesoma hoja za hawa vijana nahisi ni wale bado hawajayajua maisha wako chini ya wazazi wao

Note: serikali sio friendly na wafanya biashara
 
Kodi ndugu yangu hailipwi mtu anavyotaka, kwani ingekuwa hivyo hakuna ambaye angekubali kulipa kodi
 
Wagome tu, tumeshachoka nasema wagome tu.
 
Wadau kuna tetesi kesho kuna mgomo wa wafanyabiashara Tanzania nzima wakishinikiza mwenyekiti wao kuachiliwa huru kwan kesho ndio anapanda kizimbani
 
Wadau kuna tetesi kesho kuna mgomo wa wafanyabiashara Tanzania nzima wakishinikiza mwenyekiti wao kuachiliwa huru kwan kesho ndio anapanda kizimbani

Kipepereshu
 

Attachments

  • 1423588813453.jpg
    1423588813453.jpg
    54 KB · Views: 274
Nimepita kwenye maduka songea habari ya wafanyabiashara kugoma kesho imesikika sana!
 
Ni kweli. Hapa songea nimesikia na nikalazimika kununua kabisaaaa mahitaji ya msingi. Big up jf kwa taarifa muhimu hz.
 
Nimepita kwenye maduka songea habari ya wafanyabiashara kugoma kesho imesikika

Mimi sitagoma njooni mnunue bidhaa kama kawaida mwenge. Nigome kwa manufaa ya nani VAT si analipa mlaji?? Sitaki kutumiwa Na wakwepa kodi Na wezi wa makusanyo ya VAT. Sitaki kabisaaa!!
 
Back
Top Bottom