Wapendwa wakati tukijadili suala la mgomo wa madaktari ambao wamesimama kidete kutetea hali mbaya ya utoaji wa huduma za afya nchini, kuna tetesi kuwa kuna mgomo mkubwa wa wabunge hasa wa CCM ambao wameamua kutohudhuria bunge kwa kigezo chakukerwa na spika kuwashinikiza kukubali kila kitu hata kama ni cha uongo, ilimradi kimetoka serikalini.
Hii inadhihirishwa na uhudhuriaji mdogo sana wa wabunge hawa wa CCM hali ambayo imempa wasiwasi sana spika wa bunge Anna makinda hadi akatoa tahadhari kuwa serikali inaweza kushindwa kupitisha makadirio ya bajeti zake iwapo wabunge (hasa wa CCM) hawahudhurii.
Wabunge wa upinzani wanahudhuria wa kutosha kiasi kwamba kuna wakati wanawazidi wale wa CCM, hivyo kura ikipigwa wanaweza kushinda(Wale mnaoangalia bunge ni mashahidi wa jambo hili).
CCM imetumia mbinu nyingi wakati wa kura ikiwepo mbinu ya kuwapigia simu wabunge wake waje upiga kura wakati wa kupitisha makadirio hata kama hawakuwepo wakati wa kuchangia.
Hali iliyopo ni kama ile ya madaktari kusaini asubuhi na kuondoka. Wabunge wa CCM wanafanya hivyo hivyo kuhakikisha wanalinda posho zao.
Mgomo huu pia nao unapaswa kujadiliwa na wote wenye akili.
Hii inadhihirishwa na uhudhuriaji mdogo sana wa wabunge hawa wa CCM hali ambayo imempa wasiwasi sana spika wa bunge Anna makinda hadi akatoa tahadhari kuwa serikali inaweza kushindwa kupitisha makadirio ya bajeti zake iwapo wabunge (hasa wa CCM) hawahudhurii.
Wabunge wa upinzani wanahudhuria wa kutosha kiasi kwamba kuna wakati wanawazidi wale wa CCM, hivyo kura ikipigwa wanaweza kushinda(Wale mnaoangalia bunge ni mashahidi wa jambo hili).
CCM imetumia mbinu nyingi wakati wa kura ikiwepo mbinu ya kuwapigia simu wabunge wake waje upiga kura wakati wa kupitisha makadirio hata kama hawakuwepo wakati wa kuchangia.
Hali iliyopo ni kama ile ya madaktari kusaini asubuhi na kuondoka. Wabunge wa CCM wanafanya hivyo hivyo kuhakikisha wanalinda posho zao.
Mgomo huu pia nao unapaswa kujadiliwa na wote wenye akili.