Mgomo wa Madaktari (Leo): Kiburi cha Blandina Nyoni

Hivi wana jf,lazima mtu afanyie intern mhimbili?akienda hospitali nyingine kuna tatizo gani?au hawa intern wanataka kwenda kufanya operation ya kichwa badala ya mguu kama siku zile?

Au ndio ule mtizamo kuwa lazima uishi dar na ufanye kazi dar ndio mambo yako yatakunyookea?ukienda mkoa una loose?

wasomi wetu wanatuangusha sana,sasa kama wao wanakuwa walalamikaji kama sisi,je nani atamsaidia mwenzake?nani atamuongoza mwenzake?
mi nawaomba hawa Intern wawe flexible,maisha popote,tena wao kutokana na elimu yao wakienda mikoani watafanya kazi vizuri sana maana kwanza kuna upungufu mkubwa wa wataalam hivyo watakuwa potential sana.

Acha kutoa tuhuma zisizo na mpango, hoja ya madaktari kufanya mazoezi muhimbili ama hospitali nyingine aliyoichagua kwa mujibu wa chama cha madaktari ni kwamba kila daktari huwa na ndoto za kuwa nani hapo baadae yaani za kubobea katika kijieneo fulani, na hivyo huenda kufanya mazoezi katika hospitali ambayo anaamini ina utaalam na vifaa ambavyo vitamsaidia kufikia malengo hayo. Kwao sio suala la kukaa Dar es Salaam bali ni hospitali gani inaweza kuwafanikishia malengo yao. Halafu kwa nini hujiulizi serikali iliwaruhusu kwenda kufanya mazoezi hapo Muhimbili halafu leo baada ya kuingia nao mgogoro ing'ang'anie kuwabadilishia vituo, ili iweje? Kuwakomoa?
 
Kweli kabisa; madaktari wakiboronga sawa lakini mtu mwingine akiboronga anashikiwa bango mpaka basi!! Kwani lazima wafanyie mazoezi Muhimbili Hospitali tu?

Mkuu mbona unasema hovyo? Unajua suala la uhamisho lilikujaje? Kwa taarifa yako wazo la kuwahamisha kuwapeleka mikoani lilikuja pale walipoanza kudai malimbikizo ya malipo yao. Kuwahamisha ilikuwa kama njia ya kuwaziba midomo na kuwaadhibu wasidai tena. Kama wizara ilikuwa inaona umuhimu wa wao kwenda kufanya kazi mikoani kwa nini haikuwapeleka huko from the beggining?

Fumbuka macho!!!!!

Tiba
 
Nashangaa sana kwa Media kutangaza kwamba Madaktari hawajagoma leo! Hivi wanataka tukafie getini!!? Nimetoka kuongea na Daktari Mwananyamala ananiambia wako kwenye mgomo, na hivi sasa anaelekea Don bosco kwenye mkutano wao. Isitoshe nimeongea na Mfanyakazi(Nurse) wa Muhimbili, amenihakikishia kwamba Maddaktari wako kwenye Mgomo. Sasa kwa nn Serekali na Media hazituambii ukweli!!???
Magazeti yapi ambayo yamesema kuwa hawajagoma!?niliyonayo mkononi mwananchi,tanzania daima,daily news wameripoti mgomo!!!anyway hata kama kuna magazeti yameandika tofauti ila mficha maradhi kifo umuumbua,itajulikana tu ni suala la muda!!!
 
Mkuu hakuna daktari aliyefukuzwa, waliamishwa kutoka Muhimbili wakapelekwa Amana, Temeke, Agha Khan na Mwananyamala kwa sababu walikuwa wamejazana muhimbili.

Think japo kidogo mkuu,,kwamba "wamejazana" ilikuja tambulika baada ya mgomo wa kudai maslahi? aliyeawapangia at first hakuona kama idadi yao itakuwa kubwa?unataka kusema walijipanga wenyewe?
 
umesema mambo ya maana sana,lakini kwa kuwa watanzania tunapenda kukurupuka kabla mtu hajajua tatizo anaanza kulaumu.hawa jamaa wanataka warundikane sehemu moja ili waweze kudeseana/kuangaliziana kazi.ka ufupi ni uzembe flani ambao huwezi kuuona kirahisi hadi uwe na akili timamu.kwani kuna tatizo gani wakihamishiwa amana,mwananyamala au temeke??????????????????????????????????????????????????????????????au wanakimbilia jina kubwa la hospitali ??????????????????

Mkuu Tamuchungu, unajua Intern doctors wanapenda kujazana Muhimbili kwa kuwa ni wavivu wa kazi za mikono, unajua kwa jinsi wanavyokuwa wengi wanashindwa ata kufanya kazi za mikono. Huu ndo ukweli, Muhimbili ni Teaching hospital, kuna wanafunzi wengi wa postgraduates ambao ndo wanaaminiwa na madaktari Bingwa na kupewa wagonjwa ili wafanye upasuaji mkubwa na mdogo na kwa kuwa Intern ni wengi ili kupata mgonjwa wa kujifunzia ni mbinde kweli kweli, wanachoweza kufanya ni kutazama tu kila kukicha kama medical students wanavyojifunza, sana sana kazi za mikono wanazofanya ni kuweka drip wagonjwa pamoja na kuosha vidonda na kucrack wagonjwa ili waje waonywe na post graduate students (Residents).

Intern wavivu ndo wanaofaidika Muhimbili na ndo maana wanan'gang'ania kubaki hapo. Shughuli katika hospitali za Wilayani au Mikoani ni pevu mno, Intern anapofika Wilayani, Viongozi wa wilaya yote wanafurahi kwa kuwa wanajua Daktari aliyefuzu kikamilifu kafika na inawezekana ndo ukawa MD kepe yako Wilayani hapo umezungukwa na AMOs. Intern welevu wanaweka vichwa vyao chini na kuanza kujifunza kazi kupitia kwa AMOs waliwakuta hapo, Amini nakwambia katika kipindi cha wiki 2 tu, Intern anakuwa surgeon anafanya kila kitu, kuanzia kuzalisha kina mama wajawazito kwa upasuaji, kufanya upasuaji wa ngiri (hernia), kufanya upasuaji mkubwa wa tumbo (Lapalotomy), kuunganisha wagonjwa walivunjika mifupa, kutahiri watoto na kutibu watoto na wakubwa na baada ya mwaka mmoja tu, huyu intern wa wilayani anakuwa amefikia uwezo wa Daktari Bingwa, hawezi kulingana ata chembe na intern kutoka Muhimbili na ata linapokuja suala la ajira hapo inabidi uangalie kwa umakini madaktari waliofanya intern muhimbili kwa kuwa wanakuwa hawana maskills kabisa, inabidi uanze kuwapa upya mafunzo ya vitendo. Ukweli huu wanaujua madaktari na si porojo ndo maana sasa interns wengi baada ya kugundua hili wameamua kufanya mafunzo yao ya vitendo (kazi za mikono) katika hospitali za wilaya na za Mikoa.
 
Ukiacha Magazeti, Leo nilikuwa nasikiliza clouds FM wakiripoti kuwa hospitali zote hapa Dar, zinaendelea kutoa huduma kama kawa. Walitoa pia na taarifa kutoka Wizarani kwamba huduma mahospitalini ziko vizuri, madaktari wanaendelea na kazi!!! Hicho ndicho kilichonsukuma kuwavutiaa wire watu wangu wa katribu, nao wamenitthibitishia kuwa Madactari wapo kwny mgomo!
Magazeti yapi ambayo yamesema kuwa hawajagoma!?niliyonayo mkononi mwananchi,tanzania daima,daily news wameripoti mgomo!!!anyway hata kama kuna magazeti yameandika tofauti ila mficha maradhi kifo umuumbua,itajulikana tu ni suala la muda!!!

u
 
Mama huyu aliwahi kuwa Mhasibu Mkuu wa Serikali pale Hazina, akawa Katibu Mkuu Maliasili akawang'owa wakurugenzi waliokuwa visiki pale na sasa yuko Afya huko madaktari mtaipata

Then she is a strong woman, ingawa hapo ameteleza...
 
Mkuu Tamuchungu, unajua Intern doctors wanapenda kujazana Muhimbili kwa kuwa ni wavivu wa kazi za mikono, unajua kwa jinsi wanavyokuwa wengi wanashindwa ata kufanya kazi za mikono. Huu ndo ukweli, Muhimbili ni Teaching hospital, kuna wanafunzi wengi wa postgraduates ambao ndo wanaaminiwa na madaktari Bingwa na kupewa wagonjwa ili wafanye upasuaji mkubwa na mdogo na kwa kuwa Intern ni wengi ili kupata mgonjwa wa kujifunzia ni mbinde kweli kweli, wanachoweza kufanya ni kutazama tu kila kukicha kama medical students wanavyojifunza, sana sana kazi za mikono wanazofanya ni kuweka drip wagonjwa pamoja na kuosha vidonda na kucrack wagonjwa ili waje waonywe na post graduate students (Residents).

Intern wavivu ndo wanaofaidika Muhimbili na ndo maana wanan'gang'ania kubaki hapo. Shughuli katika hospitali za Wilayani au Mikoani ni pevu mno, Intern anapofika Wilayani, Viongozi wa wilaya yote wanafurahi kwa kuwa wanajua Daktari aliyefuzu kikamilifu kafika na inawezekana ndo ukawa MD kepe yako Wilayani hapo umezungukwa na AMOs. Intern welevu wanaweka vichwa vyao chini na kuanza kujifunza kazi kupitia kwa AMOs waliwakuta hapo, Amini nakwambia katika kipindi cha wiki 2 tu, Intern anakuwa surgeon anafanya kila kitu, kuanzia kuzalisha kina mama wajawazito kwa upasuaji, kufanya upasuaji wa ngiri (hernia), kufanya upasuaji mkubwa wa tumbo (Lapalotomy), kuunganisha wagonjwa walivunjika mifupa, kutahiri watoto na kutibu watoto na wakubwa na baada ya mwaka mmoja tu, huyu intern wa wilayani anakuwa amefikia uwezo wa Daktari Bingwa, hawezi kulingana ata chembe na intern kutoka Muhimbili na ata linapokuja suala la ajira hapo inabidi uangalie kwa umakini madaktari waliofanya intern muhimbili kwa kuwa wanakuwa hawana maskills kabisa, inabidi uanze kuwapa upya mafunzo ya vitendo. Ukweli huu wanaujua madaktari na si porojo ndo maana sasa interns wengi baada ya kugundua hili wameamua kufanya mafunzo yao ya vitendo (kazi za mikono) katika hospitali za wilaya na za Mikoa.

Here kwa hivi intern waende wilayani wakasimamiwe an AMOs?????? We vipi au wewe ni AMO nini?
 
mnamtahadharisha jk kwa yepi mema aliyotutendea? Mwacheni anase kwenye mitego aliyoshiriki kuitega. Mbaya zaidi wametega mingi kiasi hawajui njia sahihi ni zipi
 
mimi mpaka leo huwa najiuliza maswali mengi na bado sipati majibu

Hivi Waheshimiwa Ma Raisi ni kweli huwahawaoni utendaji mbuvu unaofanywa na waliowateuwa?
ama labda sisi wananchi ndio wenye matatizo hatuoni utendaji mzuri unaofanywa na hawa wateuliwa wa Mh Raisi?

haya ndio maswali yanayoniumiza kichwa tangu nikiwa kijana hadi sasa nimezeeka

kaka usiumie kichwa sana, hii ndo bongo. siasa ndo kila kitu
 
Jamani majua HEKIMA sio kila mtu anaweza kutumia,ni kitu ambacho mtu amezaliwa nacho. Huyu mama ndivyo alivyo. mi nawaomba tu tuendelee nae hivyo hivyo mapaka tuone mwisho wake. Huenda laana ya mungu ikamuangukia, huwezi jua!!
 
Kwakweli hii nchi yetu ni ya ''KUFIKIRIKA''. Ukiwaona hao wamama wa wizara hii, naibu waziri na Katibu Mkuu wake, walivyokuwa wanazungumza kwa ''jeuri'', ''kiburi'' na ''dharau'', juu ya hwaw wataalamu wanaoshughulikia maisha yetu, inasiskitisha. Wanaonyesha dharau kubwa kwa hawa madaktari, wanawachukulia kama watoto wadogo, wasiojua kitu, wasiokuwa na haja ya kudai chochote kile, hata haki yao wenyewe; ........ inatisha. Ni wapi kwingine utaona watu wazima, wenye akili timamu, wasomi, wenye taaluma, wanadharauliwa na watumishi wa serikali kama ilivyotokea?? Ni hapa Bongo tu. Ndio sababu hii imekuwa nchi ya kufikirika, haipo kiukwelikweli.


Hivi mtoto wa mkulima, Waziri Mkuu, ameweza kuvumilia haya wanayoyafanya hawa wamama hapo wizarani?? Haiingii akilini kwamba ofisa anaweza kufedhehesha serikali kiasi hicho, halafu hakuna chochote kinachotokea. Hivi matendo ya hao watu wiarani kuboronga hadi maafa kama haya ya mgomo yakajitokeza, kwa kitu ambacho walitakiwa wakishughulikie kama kazi yao ya kuajiriwa inavyotaka, sio sawa na HUJUMA KWA WATANZANIA???. Julius Nyerere uko wapi??? Ile nchi yako uliyoijenga kwa jasho inaangamizwa na wahuni
 
Nyie si ndo mliopasua kichwa cha mgojwa kuunga mguu ulovunjika? Then mkachana mguu wa mgonjwa mwingine ili mumfanyie operation ya kichwa,hapo ingependeza wazir awe pombe magufuli au steven wasira ili washrikiane na mama nyoni kuwanyoosha,iweje mng'ang'anie kubaki muhimbili kwan huku mikoani tulipo kodi yetu haichangii kwenye mishahara yenu!!

hawa ndo vibaraka wa serikali...wewe umeona wote tupo muhimbili?we umeridhika na huduma ya afya unayopata??this is rubish kwani sisi hiyo kodi hatukatwi??
 
Kweli kabisa; madaktari wakiboronga sawa lakini mtu mwingine akiboronga anashikiwa bango mpaka basi!! Kwani lazima wafanyie mazoezi Muhimbili Hospitali tu?

Kwa sababu kwa upumbavu wa serikali yako kuna huduma ambazo zinapatikana muhimbili tu...kwahiyo uko radhi tutoke shallow halafu tupewe wilaya au kijiji unachotoka wewe nikaue ndugu zako??
 
Ile issue ilikuwa ni bifu la manesi na dactari manesi wakamchanganyia ma file ... Kazi ya surgeon ni kusoma file na kufanya upasuaji pale file inaposema afanyiwe .. wa Tanzania na waandishi wa habari uchwara mkambebesha lawama dactari ...

Huyu songoro anachekesha,huko mikoani kuna vifaa vya kufanyia kazi????mara ngapi tumeona nzi theater wakati wa operation?au kumuwekea nasogastric tube mwanamke anayepelekwa theater kwaajili ya caesar badala ya catheter??au kwa sababu hatuwaambi uchafu serikali yao inayofanya?
 
Jamani wanawake wakiwezeshwa wanaweza. Mama Njelekela na Nyoni Ndo uwezo wao huo. Tuvumilie tu maana wote ni wateule wa Mkuu wa kaya. Na anaridhika na utendaji wao ULIOTUKUKA.

Mkuu wa kaya wala hana habari,yeye kaenda majuu.sijui anaigiza movie huko?
 
Yani bongo hii sijui ni mema gani unayotakiwa kufanya ili watu wakusifie. Huyu mama Blandina Nyoni ninachojua ni kwamba anajitahidi kuzuia matumizi yasio ya lazima Wizarani lakini anaishia kulaumiwa.

Tukubaliane pia kwamba udaktari ni wito kama ulivyo upadri na kama hutaki unaacha. Hakuna asiyejua kwamba serikali kwa sasa hali yake ki fedha ni tata. Sasa hao madaktari wanapogoma wakati wanajua fika kwamba serikali imeyumba kwa sasa wanategemea nini? Kwa watu wafe kwa magonjwa sababu ya kugoma kwao? Sio kweli kwamba serikali haitaki kuwalipa, ila kuna wakati mwingine hali ya kifedha serikali inakua ya kusikitisha.

Wafanyakazi wengi wa Mawizara kwa sasa wanafanya extra duty kwa kukopwa kwa muda mrefu sana. Serikali ina hali ngumu kifedha na mahitaji ya nchi hii ni mengi balaa!

Kwahiyo walivyotumia bil 50 kwaajili tu ya sherehe ya uhuru we unaona huo ni ukata?
 
Back
Top Bottom