Mgomo wa madaktari: Huu ni ugaidi

Umeongea, mwenye kusikia na asikie mwenye kusoma na asome. madaktari rudini kazini. Hili mnalolidai mko peke yenu. Kesho mtasema mama Salma hatutaki awe mke wako kwa sababu tunahisi anakushauri vibaya mkiwa nyumbani. Mnakwenda mbali!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Red: hauko nao wewe.
 
Tuanzie mbali kidogo kuhusu historia ya migomo nchini;
Wanafunzi wa vyuo vikuu waligoma wakapigwa, wakatishiwa wakafukuzwa vyuo wananchi wakaambiwa watoto wao hawana nidhamu, wakaamini wakaungana na serikali...wakubwa wakachukua chao mapema mgomo ukaisha....madai yao: posho za kujikimu kimaisha...mikopo ya elimu, nk... Matokeo yake serikali ikaonekana ina haki, wanafunzi wakaendelea kunyanyaswa wakubwa wakatumia vibaya fedha za mikopo ya wanafunzi...leo anayepewa mkopo si anayestahili...watoto wa maskini hawana haki na kodi za baba zao tena...ungepata nafasi kidogo ya kuwa maeneo waliyopo hawa watoto ungelia machozi! Wale wa kike wameopt umalaya na kuombaomba hawawezi tena kusoma, kiwango cha elimu kimeporomoka, ushahidi ni madhara tunayoona maofisini mwetu kwa graduates waliotoka vyuo vikuu, matokeo ya mitihani ya darasa la saba na sekondari kuporomoka...wananchi waliosapoti serikali wanamuona Ndalichako...Mwanaasha kapata nini?
Waalimu wakagoma kwa madai hayohayo...wakagawanywa na strategists kuwa waunde kamati, wakatishiwatishiwa na kikamati chao, wakanywea, wakubwa wanapeta wanafanya watakavyo na fedha zetu na maisha ya walimu yanazidi kuwa duni...wananchi wamedanganywa tena kuwa walimu wanadai kisichowezekana, wakaamini hizo propaganda wakaacha kuunga mkono walimu, madhara yake ni migomo baridi ya walimu na kufeli watoto. Walimu kwakuwa nao ni binadamu, wameopt viosk vyao viitwavyo tuition...darasani hawafundishi ili watoto waje tuition...mfumo wa elimu umeporomoka, wananchi wameacha kuilaani serikali, wanawalaani walimu kwa msaada wa serikali
Sasa madaktari. Wao wamejipanga. Serikali inaogopa kutumia nguvu kuwalazimisha warudi kazini kwa kuwa wanajua hawa jamaa wameshikamana na hawataki kamati inayoweza kununuliwa na mafisadi. Wanasimama kwa umoja wao dhidi ya dhuluma za serikali yao. Pinda katupiwa mzigo peke yake na mtalii anapiga propaganda akijua hawezi kushinda. Anajaribu kutafuta huruma za wananchi kupitia press. Tunawapata wananchi wachache wasioamini juu ya mabadiliko wanaona tu vifo iwapo madaktari watagoma na kuwatupia madaktari lawama. Hawaoni madhara ya mgomo huu kwa mbali...wanaishia kutetea serikali legelege.
Wasijue kuwa serikali hii ni kama punda asiyekwenda pasipo mjeledi...madaktari wasipoyumba, wagonjwa kweli watapata shida na wengine kupoteza maisha, lakini hatimaye serikali haiwezi kuwafukuza kwani haina mahali penginepa kupata madaktari na gharama yake serikali yetu haitaiweza. Kwa hiyo serikali itatekeleza tu matakwa ya madaktari...wakimaliza wao, wale watu wetu waoga -walimu, nao watadai, watapewa, askari wetu nao pamoja na kukubali kutumiwa vibaya, nao watadai, watapewa, na wengine. Hiyo ndiyo hofu kubwa ya mtalii.

Conclusion: pasipo mjeledi, punda huyu aitwaye serikali hatokwenda! Madokta wetu aluta continua, mapambano yaendelee, tuko nyuma yenu mpaka serikali hii dhalimu ianze kujirekebisha kwa kuweka vipaumbele vyake sawa na kuzuia matumizi mabaya ya fedha za umma ili wazielekeze kwenye mambo nyeti


MkUU HAPO KWENYE RED HAPO...
"SASA HIVI TUNAWAKARIBISHA MJE MBELE TUWE PAMOJA NA SERIKALI INAYOFIKIRIA KWA KUTUMIA MATUMBO IONE KUWA TUKO PAMOJA "
 
kimsingi nilikuwa nakubaliana na madai ya madaktari ila sasa naona wamelewa umaarufu na kuingilia kazi za watu.mi sioni msingi wa kulazimisha mawaziri kujiuzulu maana ata wakija wengine ni wa aina hiyo hiyo kwani ndege wa rangi moja huruka pamoja. cha msingi wadai madai yao na si kujadili watu,au wapendekeze waziri aliye safi wanayemtaka kama yupo. mwisho nawakumbusha pamoja na madai yao ya msingi lakini wajue hawa viongozi wetu hawana roho tena hawaumii hata kidogo na vifo vya watu ambao ni ndugu za madaktari na wao wenyewe maana ata wao uwezo wa kwenda apollo India hawana. rudini kwenye hoja ya msingi

Kamwambie alokutuma KIMENUKA NA AKICHEZA HUU MGOMO UTAMTOA MADARAKANI..
 
kifupi wanaowatumia kuleta machafuko au kuifanya serikali isiwe stable ni wapuuzi kama mlivyo nyinyi. elimu zenyewe mmesoma za kudesa sasa mnaleta kiburi!!!!!!!!!!!!!!! mkigoma siku mbili tu mmeanza kupiga simu za kulalmika hamna hela kwakua mmezoea kuomba rushwa hata za wagonjwa mahututi ili muwaongeze damu.
 
kifupi wanaowatumia kuleta machafuko au kuifanya serikali isiwe stable ni wapuuzi kama mlivyo nyinyi. elimu zenyewe mmesoma za kudesa sasa mnaleta kiburi!!!!!!!!!!!!!!! mkigoma siku mbili tu mmeanza kupiga simu za kulalmika hamna hela kwakua mmezoea kuomba rushwa hata za wagonjwa mahututi ili muwaongeze damu.

Wewe utakuwa MGONJWA WA AKILI, na 1 ya sifa zao kubwa ni KUKATAA WAO HAWAUMWI Pale wanapoambiwa ni WAGONJWA wao husema ni wazima. na kwa kuthibitisha hili utakataa sasa hivi,


NAKULIZA SASA: WEWE NI MGONJWA WA AKILI?
WAHI MIREMBE UKACHUKUE DAWA MAKE NAHISI ZIMEKWISHA.
 
ALUTA CONTINUA....Mtaongea sana tu, ila hii si siasa, tunachohitaji is so simple,WAJIUZULU!!! Tuwe wajinga, hatuna huruma n.k but kama hawatojiuzulu na sisi haturudi kazini..FULL STOP
 
wazo jema kabisa. madaktari mmepata mkate wenu katika mgomo wa kwanza angalau kidogo, watu wamekufa, leo tena mnadai wafukuzwe mawaziri, jamani nahilo tu watu wafe. hapana hamna haki hata kidogo. Tunawapenda sana madaktari na roho zetu ni zenu!!
jiulize ni wangapi wanakufa na kupata maradhi mapya kwa kuwepo huduma mbovu?
 
ALUTA CONTINUA....Mtaongea sana tu, ila hii si siasa, tunachohitaji is so simple,WAJIUZULU!!! Tuwe wajinga, hatuna huruma n.k but kama hawatojiuzulu na sisi haturudi kazini..FULL STOP

Fahamu kuwa huyo anayeathirika na mgomo wako hana mamlaka ya kumwajibisha waziri wako.Mwenye hayo mamlaka hata akiugua hatakutafuta wewe either umegoma au upo kazini,atawahi India.Kubalini tu kuwa mnayemkomoa kwenye hili ni mwananchi wa kawaida asiye na hatia"innocent bystander".
 
Hakuna suala la ugaidi hapa. Ni kwa vile tu binadamu tuna utashi na akili na tunajua kusikia na kusikiliza na kuongea. Kifupi tuna ufahamu. Hivi vinajenga nusu ya kwanza. Nusu ya pili inajengwa na silika, na ndicho kinachotokea sasa. Ukweli mwingine ni kuwa hakuna jambo jema lisilo na mapito. Chukulia mzazi, chukulia mmea, chukulia madini (yanapitia kwenye moto ndipo yawe vito). Kifupi hakuna kkitu bora kisicho na mchakato wa shuruba. Kinachotokea sasa ni lazima kitokee kwa kuwa silika ni maisha yetu. Lazima watu waumie ndipo nidhamu ipatikane. La sivyo leo tusingekuwa na sheria na miongozo. Hii inatokana na kadhia zilizoamsha fikra za nini cha kufanya. Ni ukweli ulio mchungu kuwa hakuna mwenye makosa kati ya hizi pande mbili zinazovutana. Ni nature inafanya kazi na mwisho wa siku wingu litatulia na muafaka kupatikana. Paradoxically, war is peace
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom