Mgomo wa Daladala Jijini Arusha asubuhi hii ya Julai 3, 2023

Bushmamy

JF-Expert Member
Aug 18, 2019
8,848
15,252
Madereva wa Daladala Mkoani Arusha wamegoma leo Kwa kile wanachodai kuwa ni Bajaji kufanya Kazi kama daladala.

Idadi kubwa ya wanafunzi na watu wazima wamekuwa wakitembea kwa miguu na wengine wakiwa tu vituoni wakiwa hawajui cha kufanya.
Mamia ya wakazi wa jiji la Arusha wakiwemo wanafunzi wa shule,wamekumbwa na adha ya usafiri mara baada ya madereva wa daladala Mkoani hapa kugoma kwa kile wanachodai kuwa ni Bajaji kufanya Kazi kama daladala na hivyo kuwalazimu abilia kupanda Guta na kutembea kwa miguu.








Mgomo huo ambao umeanza mapema leo ,umewaathiri zaidi wanafunzi ambao wamefungua shule leo,ambao walionekana wakiwa kwenye vituo vya usafiri wakisubiri magari mbalimbali na wengine wakilazimika kudandia pikipiki za mizigo( guta )na wengine kutembea kwa mguu umbali mrefu.



Baadhi ya madereva wa daladala eneo la kwa Mirombo walionekana wakicheza mpira huku magari yao ya usafiri wakiwa wameyaficha maeneo mbalimbali wakiwa na madai kwamba hawatapeleka gari barabarani mpaka serikali itoe tamko juu ya utaratibu mpya kati yao na bajaji ambao hautaathiri mapato yao.

====

UPDATE;

photo_2023-07-03_08-52-24.jpg




Hali ilivyo katika Kituo Kikuu cha Daladala Kilombero Jijini Arusha ambapo daladala zipo katika mgomo wa kutoa huduma wakidai Bajaj zinaingilia njia zao na hivyo kuathiri mapato yao ya kila siku.

IMG_7837.jpeg
IMG_7839.jpeg
IMG_7838.jpeg

Hali ilivyo Kwa Morombo jijiji Arusha Kwenye mgomo wa Daladala usiokuwa na kikomo madereva wakilalamikia kuongezeka kwa Bajaji jijini Arusha na Kuwaingilia kwenye Ruti zao ambapo Wananchi wametumia usafiri wa Mguta leo kuingia mjini

Daladala za kutoka Morombo kwenda Mjini, daladala za kutoka Engo kuelekea Mjini.

Daladala za kutoka Uswahili kwenda Mjini. Ngusero kwenda Mjini

Ndani ya Kituo cha Daladala cha Kilombero hakuna daladala kabisa, Bajaj na bodaboda ndo zinafanya kazi tu na hazitoshelezi abiria ni wengi.

Bajaj zimepandisha bei kutoka Tsh. 500 hadi Tsh. 1,000.

Pia soma: Arusha: Usafiri wa daladala kurejea, madereva wamaliza mgomo
 
Leo asubuhi kumetokea mgomo wa daladala zinazofanya safari za Stand kwenda Kwa Morombo sababu za kugoma ni kushinikiza bajaji ziindolewe kwenye njia Yao.

Naiomba serikali ichukue hatua kali kwa wamiliki wa hayo magari. Yaani Kila gari inayofanya safari ya abiria njia ya morombo na njia ya olasiti ipigwe faini siyo chini ya elfu 30 kwa Leo maana huo ni uhuni kutegea shule zinafunguliwa ndo wanafanya mgomo usio na mashiko! Yaani mtu anaamka tu huko kichwani anaamua kutesa abiria!

Hii inchi kama vile inachezewa Sasa! Mara nyingi ikishafika jioni hizi daladala za morombo zinapeleka abiria ngaramtoni na kuwaacha abiria wa morombo wanahangaika hasa watoto wa shule hadi usiku ndipo hujitokeza na kufanya safari za morombo. Kuondokana na kadhia hiyo pia, daladala za morombo ziindolewe kwenye njia ya ngaramtoni wabakiwe na njia ya morombo.

SERIKALI ICHUKUE HATUA KALI KWA KILICHOFANYWA NA DALADALA ZA MOROMBO LEO NA OLASITI.

Kuna root wamejianzishia kutoka morombo stand hadi dampo wanachukua jero za watu huo ni wizi na sijui kama Sumatra au latra wanajua hiyo root? Sijaona daladala zimesajiliwa hiyo root lakini zinapakia pale na traffic wapo! Abiria akitoka mjini analazimika mara zingine ashuke morombo apande tena daladala ya dampo kama anaishia hapo katikati!

DALADALA ziindolewe njia ya morombo na njia ya uswahilini hadi east Africa road ziwekwe Costa kupunguza jam na njia ya olasiti. Ziende majengo, kisongo, na kwingine kwenye abiria wachache
 
Hao watu wa Dalala wamekurupuka vibaya

Watu tunaishi kwa kutegemea na kugawana rizki ni sehemu ya maisha

Wao wanaona bajaji zina faidi sana wakati hata wao wananufaika pia, wanadai Bajaji zinaleta Jam kitu ambacho hakimake sense

Jiji la Arusha bara bara nyingi nyembamba na hazina Viwango magari mengi watu wengi Jam lazima iwepo, mtu unaweza ukakaa barabaran hata lisaaa kwasababu ya Jam tuu magari mengi

Nadhani utaratibu uwekwe Bajaji/Daladala zoote vifanye kazi na sio Bajaji zipigwe marufuku hii itakuwa ni uonevu.
 
Kweny usajili huo waliambiwa wao tu ndo wana hati miliki ya uchukuz ndan ya hizo route ? Je unampangia abiria?
Hivi umeelewa ninachomaanisha? Hakuna aliyeambiwa kuwa ana hati miliki ya uchukuzi. Nimeuliza, wamesajiliwa kufanya shughuri za uchukuzi?
 
Hao watu wa Dalala wamekurupuka vibaya

Watu tunaishi kwa kutegemea na kugawana rizki ni sehemu ya maisha

Wao wanaona bajaji zina faidi sana wakati hata wao wananufaika pia, wanadai Bajaji zinaleta Jam kitu ambacho hakimake sense

Jiji la Arusha bara bara nyingi nyembamba na hazina Viwango magari mengi watu wengi Jam lazima iwepo, mtu unaweza ukakaa barabaran hata lisaaa kwasababu ya Jam tuu magari mengi

Nadhani utaratibu uwekwe Bajaji/Daladala zoote vifanye kazi na sio Bajaji zipigwe marufuku hii itakuwa ni uonevu.

Hakuna mtu anayesema bajaji zisifanye kazi, tatizo ni utitiri wa bajaji na kutokuwa na mpangilio wa njia/barabara zipi wapite
Sheria ilikuwa bajaji zitumike kwa kokodisha kama taxi, sasa zinafanya kazi ya kubeba abiria kama daladala, tatizo lingine hazipakiii wanafunzi, kitu ambazo kinafanya wanafunzi wengi wapakie daladala. Unakuta daladala imejaa wanafunzi tu, na hivyo kufanya gharama za uendeshaji daladala kuwa kubwa kwani wanafunzi wanalipa 200/= tu.


Kumaliza ili tatizo, ni vizuri mamlaka husika zichukue hatua na kuamuru bajaji zitumike kama taxi tu kama sheria iliyowasajili inavyo wataka.
 
Bajaji zinateka sana abiria, mbeya kidogo saizi bajaji na daladala wanagawana riziki baada ya bajaji kupigwa pin baadhi ya njia.

Bajaji usipowacontrol huwa wanaenda popote. Bajaji za mbeya hazina ruti maalum ni kama boda tu, ukimkuta mahali anakuuliza unaenda wapi, anapiga hesabu zake pale then twende.

Zinawasaidia sana abiria maana ni chap kwa haraka unafika uendako.

Kwa huko Arusha huenda kuna baadhi ya njia waachiwe hao wa daladala na nyingine hasa za mitaani ndo zitekwe na bajaji.
 
Sasa nani fala? Serikali na mamlaka zake zinazotoa vibali na kushindwa kuvisimamia kisheria, Wamiliki wa Daladala, Wamiliki wa bajaji au abiria?
Hilo limkute mhusika ambae hana grades za kuheshimu hadhi ya mji wa kitalii Arusha Manispaaa ni ndogo sana na Iko bize sana.
 
Back
Top Bottom