Uchaguzi 2020 Mgombea Urais CCM adhibitiwe kuhusu suala la matumizi ya lugha ya Kisukuma. Mwongozo wa lugha wanaounadi TBC ufuatwe

manafyale

JF-Expert Member
Nov 25, 2014
277
158
TBC katika taarifa yao kwa maelekezo kutoka Tume ya Uchaguzi ya Taifa wametoa maangalizo mengi lakini mimi moja ambalo nimeliona kama mgombea Urais kupitia CCM analikiuka sana.

Lile tangazo linasema kuwa kama mgombea atakuwa jukwaani anamwaga sera basi atumie lugha ya Kiswahili tu, kama kutaonekana kuna haja ya kutumia lugha nyingine yaani native ya kikabila basi atafutwe mkalimani hili afasili na kufikisha ujumbe.

Cha kushangaza leo kuazia hile mitaa ya kina Kitwanga hadi Geita hadi kwa akina Msukuma hadi mwanza. Mzee nimemwona anakandamiza Kisukuma kwa sana. Hii lugha ya watani zangu ni nzuri kusikiliza maana hujui wanatumia ule ugali mgumu au nini, maana amekuwa anakandamiza njia nzima. Pia amekuwa anamwita First Lady Mama yule mpole sana tena mwalimu naye anaanza kwanza kwa kukandamiza alafu anaomba kura kwa Rais, Wabunge na Madiwani. Kwa kifupi wamekandamiza njia nzima.

Tunaomba mwongozo kwa vyombo vinavyohusika vitoe tafsiri kuhusu hili kwani linaweza kuchochea ukabila hapa Tanzania, na pia nimponge mgombea wa Urais kupitia CCM kwa kuwa ananadi sera zake bila kutumia lugha ngumu au kutupa mitusi kama baadhi ya wagombea wengine, kwani nimewaona wanakomaa na mtu binafsi, kashfa, mitusi na kujisahau kuwa watanzania wamekusanyika kusikiliza sera atawafanyia nini pindi watakapo mchagua, wanakuta kumbe akipata uongozi atakomaa na mtu flani.
 
Lakini angeongea Kiingereza hakuna hata moja angelalamika. Watanzania tuthamini lugha zetu sisi wenyewe. Kwani kuna ubaya gani akiongea kisukuma wakati wengi wa wanaomsikiliza wanafahamu lugha hiyo. Mwachemi JPM awe JPM na nyinyi mkiwa marais muwe mna-copy and paste kama wanavyofanya kina Trumpet na vipapeti vyao.

BTW kisukuma kimesaidia kukua kwa kiasi kikubwa kwa lugha ya Kiswahili.
 
Sawa........

Ingekuwa ANACHOKIONGEA hakieleweki na HADHIRA hapo Ni tatizo....kumbe ANACHOCHOMBEZA anaeleweka na hata kina Bwashee(Maana ukiishi Usukumani Ni rahisi Sana kuvutiwa KUKIJUA).

Acheni GUBU eeee
 
Jamaa ana siasa za kishamba sana, siasa za ukabila na ukanda,, its not worth for our nation!
Tulia Dawa ikuingie Halima Mdee Alitumia Lugha ya Wahuni Kale Kawe Anasema Mchumba Sijui watoto Wa kitaaa watamwonyesha Gwaji Boy Mimi hatasikuelewa ile lugha ya kihuni
 
Lakini angeongea Kiingereza hakuna hata moja angelalamika. Watanzania tuthamini lugha zetu sisi wenyewe. Kwani kuna ubaya gani akiongea kisukuma wakati wengi wa wanaomsikiliza wanafahamu lugha hiyo. Mwachemi JPM awe JPM na nyinyi mkiwa marais muwe mna-copy and paste kama wanavyofanya kina Trumpet na vipapeti vyao.

BTW kisukuma kimesaidia kukua kwa kiasi kikubwa kwa lugha ya Kiswahili.
Sheria ya Uchaguzi imesema waongee Kisukuma?
 
Lakini angeongea Kiingereza hakuna hata moja angelalamika. Watanzania tuthamini lugha zetu sisi wenyewe. Kwani kuna ubaya gani akiongea kisukuma wakati wengi wa wanaomsikiliza wanafahamu lugha hiyo. Mwachemi JPM awe JPM na nyinyi mkiwa marais muwe mna-copy and paste kama wanavyofanya kina Trumpet na vipapeti vyao.

BTW kisukuma kimesaidia kukua kwa kiasi kikubwa kwa lugha ya Kiswahili.

Hayo Mambo ya Ukabila ndiyo yaliiangamiza Rwanda.
 
Kisheria wagombea au chama kinachoona maadili yamekiukwa kinapaswa kutoa taarifa time ya uchaguzi kuhusu ukiukwaji husika
 
Lakini angeongea Kiingereza hakuna hata moja angelalamika. Watanzania tuthamini lugha zetu sisi wenyewe. Kwani kuna ubaya gani akiongea kisukuma wakati wengi wa wanaomsikiliza wanafahamu lugha hiyo. Mwachemi JPM awe JPM na nyinyi mkiwa marais muwe mna-copy and paste kama wanavyofanya kina Trumpet na vipapeti vyao.

BTW kisukuma kimesaidia kukua kwa kiasi kikubwa kwa lugha ya Kiswahili.

Kanuni za uchaguzi zina ruhusa hayo au wewe unaongea kwa matakwa yako maana tayari zipo kanuni zinazokataza kutumia lugha nyingine zaidi ya kiswahili na endapo kuna umuhimu wa kutumia awepo mkalimani jambo ambalo halifanyiki kinyume na kanuni za uchaguzi.
 
Kanuni za uchaguzi zina ruhusa hayo au wewe unaongea kwa matakwa yako maana tayari zipo kanuni zinazokataza kutumia lugha nyingine zaidi ya kiswahili na endapo kuna umuhimu wa kutumia awepo mkalimani jambo ambalo halifanyiki kinyume na kanuni za uchaguzi.
Waliopo mkutanoni wote wanafahamu kisukuma kama hupendi kajinyonge. Hata mimi naanza kukimanya.

BTW nenda kawaambie tume ya uchaguzi kwamba rais anavunja kanuni kwa kuhutubia kisukuma kuliko Kiswahili, wakati wasikilizaji wengi ni Wasukuma na wanaifahamu ile lugha vizuri zaidi. Khe khe khe khe kheee. Mmeanza kuokoteza sababu ambazo hazima mashiko. Hivi upimbi huu mtaacha lini?
 
Lakini angeongea Kiingereza hakuna hata moja angelalamika. Watanzania tuthamini lugha zetu sisi wenyewe. Kwani kuna ubaya gani akiongea kisukuma wakati wengi wa wanaomsikiliza wanafahamu lugha hiyo. Mwachemi JPM awe JPM na nyinyi mkiwa marais muwe mna-copy and paste kama wanavyofanya kina Trumpet na vipapeti vyao.

BTW kisukuma kimesaidia kukua kwa kiasi kikubwa kwa lugha ya Kiswahili.
Unaifahamu lugha ya taifa
 
Back
Top Bottom