Mhache
JF-Expert Member
- Jun 20, 2008
- 345
- 25
"Ni fedheha kwa kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania kumruhusu mtu anayetuhumiwa kwa ufisadi kutumia miibara takatifu kujisafisha", hiyo ni kauli ya viongozi wa kanisa waliyoitoa jana katika mkutano wao wa kujadili suala hilo.
Maswali la kujiuliza ni nani alimwalika Rastom kuwa mgeni rasmi katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Kinondoni? Na je makao makuu ya kanisa KKKT hawakuwa na taarifa kuwepo kwa shughuli hiyo?
Ndugu Rastom Azizi alialikwa na Usharika wa kanisa la Kinondoni kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Albam ya Kwaya ya Amkeni. Katika uzinduzi huo Mheshimiwa huyo aliahidi kutoa shilingi millioni tano taslim na milioni mbili kwa ununuzi wa vifaa vya kwaya hiyo.
Ninawiwa kusema kwamba KKKT inabidi kulitolea kauli suala hilo na kuwa na utaratibu wa kuwaalika watu walio safi katika uzinduzi wa shughuli nyeti kama hizo. Kanisa ni mahali patakatifu panapohitaji uchaji wa hali si kualika mtu hata anahisiwa kuwa na kosa fulani. Tumwombe Mungu atuongoze katika kutenda na kutoa maamuzi. Maji yakimwagika ni nini chakufanya.
Maswali la kujiuliza ni nani alimwalika Rastom kuwa mgeni rasmi katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Kinondoni? Na je makao makuu ya kanisa KKKT hawakuwa na taarifa kuwepo kwa shughuli hiyo?
Ndugu Rastom Azizi alialikwa na Usharika wa kanisa la Kinondoni kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Albam ya Kwaya ya Amkeni. Katika uzinduzi huo Mheshimiwa huyo aliahidi kutoa shilingi millioni tano taslim na milioni mbili kwa ununuzi wa vifaa vya kwaya hiyo.
Ninawiwa kusema kwamba KKKT inabidi kulitolea kauli suala hilo na kuwa na utaratibu wa kuwaalika watu walio safi katika uzinduzi wa shughuli nyeti kama hizo. Kanisa ni mahali patakatifu panapohitaji uchaji wa hali si kualika mtu hata anahisiwa kuwa na kosa fulani. Tumwombe Mungu atuongoze katika kutenda na kutoa maamuzi. Maji yakimwagika ni nini chakufanya.