Mgema akisifiwa tembo, hutia maji

Mgema akisifiwa tembo, hutia maji

Nchi Kavu

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2010
Posts
4,289
Reaction score
2,472
Mgema ni mvunaji wa pombe na tembo bila shaka ni aina ya pombe, sio tembo mnyama katika muktadha huu, sasa mi ni prefessional videographer. Huwa pia nafanya video za sherehe kama harusi mengi huwa tunayaona na kuyasikia sasa juzi hapa katika ndoa fulani mchungaji akawa anasifia mno umahiri wa mwanamke katika tasnia ya ndoa.

Akampamba hadi Delila mpaka basi, Samsoni akapondwa akaonekana tu nasi wanaume tukajiona mabwege tu mbele ya mwanamke, kiukweli mahubiri ya mchungaji yule mwanaume bila shaka yalimwingia vizuri mdada maana aliambiwa kuwa mwanamke ni kila kitu na uhai wa mwanaime uko mikononi mwa mwanamke MC nae ukumbini kama walikuwa na mchungaji vile.

Sasa sherehe ikaisha wiki haijaisha mume anaanza kulalamika nje kuwa mkewe anampangia masharti kadha wa kadha ikiwa ni pamoja na aina ya vyakula vyakupikwa home. Jamaa anakuwa mbogo sasa na anataka kuweka heshima kwenye ndoa yake changa tutajua tu ni nani zaidi kati ya Delila na Samsoni japokuwa Samsoni wetu ni 'jitu la mraba mmoja.
 
Ukitaka maisha ya ndoa na ndoa yenyewe idumu lazima mmoja ajifanye ---- asee...Mimi nimekubali kuwa boya na life linaenda ile mbaya.Tayari kwa mfano umeshapata watoto ni nin tena unatafuta huko kama heshima mtu hakufunzwa kwao wewe utamfunzaje? Utapiga utaua bureeeee.
 
Ukitaka maisha ya ndoa na ndoa yenyewe idumu lazima mmoja ajifanye ---- asee...Mimi nimekubali kuwa boya na life linaenda ile mbaya.Tayari kwa mfano umeshapata watoto ni nin tena unatafuta huko kama heshima mtu hakufunzwa kwao wewe utamfunzaje? Utapiga utaua bureeeee.

sawa kaka. Ni kweli mafahali wawili hawakai zizi moja
 
Back
Top Bottom