Regia Mtema
R I P
- Nov 21, 2009
- 2,970
- 864
Ni
Taarifa ya habari chanel 10 Mgaya kakanusha, kasema kwanza yeye siyo mwanachama wa chadema.
Duu, Jamaa amekanusha.Kwani anaogopa nini?
Ni
Taarifa ya habari chanel 10 Mgaya kakanusha, kasema kwanza yeye siyo mwanachama wa chadema.
Kwa akili ya watanzania nitakubaliana na wewe lakini katika nchi nyingi mgomo ni haki ya mfanyakazi uwe unamsukumo wa kisiasa, upinzani au chochote kile, kinachotafutwa ni maslahi mazuri ya mfanyakazi haijalishi yameletwa na nani. Hata TANU ilitumia vyama vya wafanyakazi kufanikisha matakwa yake kama TAA, NUTA nk. Mimi nafikiri wafanyakazi hawana akili ndogo kiasi hicho kudhani kwa vile madai yao yanamsukumo wa siasa za upinzani basi wasidai tena au ndiyo sababu ya kumpa kura JK.
"Kwa kweli sivijui vipeperushi hivyo, na kwanza sihusiki navyo kwa sababu mimi si Nicholaus, mimi ni Nicholas Mgaya," alisema Mgaya.
Katibu wa Chadema wa Mkoa wa Tanga, Benson Mramba, ambaye alisema:
"Tumeshtushwa na hiyo taarifa, kwa sababu hatuna mawasiliano naye ya aina yoyote… mimi nilipigiwa simu na viongozi wa Chadema wa wilaya ya Muheza, wakidhani huyu jamaa amepitia mkoani hapa moja kwa moja.
"Tukapata mshituko na kutaka kuthibitisha na makao makuu nao wakasema hawana taarifa wala mawasiliano naye, lakini kama Mtanzania na mwananchi wa kawaida, anakaribishwa (Chadema) kama atafuata taratibu kwani ni haki yake ya msingi na ya kikatiba."
Kule Muheza mmojawapo wa watu wenye kutaka kugombea kule ni Balozi Andrew Daraja na Mbunge wa sasa Herbert Mntangi. Lakini siku chache zilizopita (kuanzia hii tarehe 19 Mei) kuna tetesi kuwa Katibu wa TUCTA Yusuph Mgaya ambaye alijiwa juu na Rais Kikwete anampango wa kupeleka mapambano yake ya wafanyakazi ndani ya Bunge kwa kugombea huko Muheza kwa tiketi ya Chadema. Kuna vipeperushi inadaiwa vimeenezwa vikimwaga sifa zake huko na wenye nchi yao wanashtuka.
Hata hivyo, kwa sasa Bw. Mgaya hajakiri moja kwa moja kuwa kweli anataka kugombea zaidi ya watu wengine kuwa na wasiwasi huo kwa sababu tu alienda kusalimia nyumbani kwao na kuondoka mapema na hivyo tetesi hizi kuanza.
Stay tuned.
Mi nadhani fikra zako ndizo zinaturudisha nyuma. Jamaa kakujibu kwa reference sasa nani ana fikra zinazopiga reverse?Maeneo tofauti
Sio kilakitu kina apply, hizi fikra zako pia nafikiri ndo zinaturudisha nyuma