Mgao wa umeme umeanza kimya kimya Arusha

Mgao wa umeme umeanza kimya kimya Arusha

Tajiri Tanzanite

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2016
Posts
3,000
Reaction score
5,656
Hapo vip!!

Huku maeneo ya Ngulelo, Kimandolu Sekei n.k umeme umekuwa unakatwa kuanzia saa 8 nane mchana mapaka siku inayofuatwa.

Kitu ambacho wananchi wenzangu wanalalamika ni kutopewa taarifa ili wapambane na hali ya hilisi kwasababu kuna watu wanategemea umeme kuingiza kipato.

Mfano wafanyabiashara wa samaki na nyama wanategemea umeme kuifadhi bidhaa zao zisiharibike.

Tunaomba TANESCO muache madharau..
 
Hapo vip!!
Huku maeneo ya Ngulelo,Kimandolu sekei n.k umeme umekuwa unakatwa kuanzia saa 8 nane mchana mapaka siku inayofuatwa.

Kitu ambacho wananchi wenzangu wanalalamika ni kutopewa taarifa ili wapambane na hali ya hilisi kwasababu kuna watu wanategemea umeme kuingiza kipato.

Mfano wafanyabiashara wa samaki na nyama wanategemea umeme kuifadhi bidhaa zao zisiharibike.

Tunaomba TANESCO muache madharau..
Sema taarifa hazijakufikia, sio kimya kimya.
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)

TAARIFA YA KATIZO LA DHARURA-TANESCO MKOA WA ARUSHA


Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Mkoa wa Arusha,linawataarifu wateja wake kuwa,Kutakuwa na matengezo ya dharura katika kituo chetu kikubwa cha kupooza na kusambaza umeme Njiro kama ifuatavyo:-

Tarehe: 24/02/2021
Siku: Jumatano
Muda: 19:00 Jioni- Saa 22:00 usiku
Feeder: Industrial 3,Themi 1,Sakina na M5

Sababu Matengenezo ya dharura katika katika kituo chetu kikubwa cha kupooza na kusambaza umeme Njiro ili kuboresha hali ya upatikanaji wa umeme

Maeneo yanayoathirika Moshono,chekereni, boma siara,suye,baraa, olorieni,kokoriko, baadhi ya maeneo ya kijenge,Njiro PPF, Sunflag factory, Ngaramtoni Seliani, Ngaramtoni NMB, stand ya zamani Ngaramtoni, sokoni Ngaramtoni, Kimynaki, visima vya maji,Olkokora,mbuga nyeupe, Njiro nane nane,Njiro SDA, Chuo cha Uhasibu, ESAMI, Njiro kwa Tondi, Double B, Kikwakwaru A, Sunflug quarters, Njiro complex, Kambini, world vision, TBC,FFU ,Sekei yote, Olgilai, Ngiresi,Bangata, Midawe, Engokareti, Kwa mbotela, Songota, Olgilai kimeo, na baadhi ya maeneo ya jirani .

Ungozi unaomba radhi sana kwa usumbufu wowote utakaojitokeza

Kwa taarifa yoyote ya dharura tafadhali wasiliana nasi kupitia namba za simu zifuatazo:

Tanesco Arusha dawati la dharura, 0272610120 na 0758174343

Call centre: 0768985100 & 022194400

Huduma kwa wateja Arusha: 0737 894000


Imetolewa na : Ofisi ya Uhusiano na Huduma kwa wateja
TANESCO- Arusha
24/02/2021
 
Huku Morogoro yaaani ni kero kwa wiki mbili maeneo mengi tu umeme umekuwa ni shida wanaweza kata hata siku 2 bila taarifa na hata leo nilipo tumeshinda bila umeme
 
...hata huku mtoni Kijichi wilaya ya Temeke hali ndo hiyo hiyo. Yani ikifika saa tatu asubuhi kila siku wanakata umeme, bila taarifa yoyote.. Inaboa sana
Tafuteni taarifa, kwa tabia hii ndio nyie mkiitwa kwenye vikao vya watoto shule hamuhudhurii mpaka jumba bovu limwangukie mwanao.

As long as upo connected na Tanesco hakikisha una namba za huduma kwa wateja.
 
Hata hapa Mbeya kuna viashiria kwa mbali. Kwa mfano leo Jumamosi asubuhi walikata na jioni mida ya saa 10 pia. But hali siyo serious sana coz wakikata hawachukui muda wanarudisha. Lakini niwaombe tu watanzania wenzangu tuwe wavumilivu.
 
Tafuteni taarifa, kwa tabia hii ndio nyie mkiitwa kwenye vikao vya watoto shule hamuhudhurii mpaka jumba bovu limwangukie mwanao.

As long as upo connected na Tanesco hakikisha una namba za huduma kwa wateja.
Acha dharau ww mbona mgao upo na inajulikana au unadhani wote humu hawaelewi
 
Acha dharau ww mbona mgao upo na inajulikana au unadhani wote humu hawaelewi
Sijakataa kwamba kuna shida ya upatikanaji wa umeme, hoja iliyotolewa ni kuwa hakuna taarifa yoyote juu ya hili. Kuna mtu amekwenda Tanesco kuuliza? Kifurushi chako cha simu kikiisha isivyo lazima uwapigie customer care, je unamawasiliano ya customer care services za Tanesco? Dharau sio! Utabaki hewani hivyo hivyo.
 
Hata hapa Mbeya kuna viashiria kwa mbali. Kwa mfano leo Jumamosi asubuhi walikata na jioni mida ya saa 10 pia. But hali siyo serious sana coz wakikata hawachukui muda wanarudisha. Lakini niwaombe tu watanzania wenzangu tuwe wavumilivu.
Ninachoona hapa Ni watu wamemiss enzi za mzee wako Edoo wa RichMavocco....
 
Huku Morogoro yaaani ni kero kwa wiki mbili maeneo mengi tu umeme umekuwa ni shida wanaweza kata hata siku 2 bila taarifa na hata leo nilipo tumeshinda bila umeme
Lukobe ni noma, siku mbili hakuna umeme,bora kua nzia jana kuna nafuu
 
Naliport live kutoka Ubungo Kibangu. Jana tokea saa 1 hadi saa 12 jioni.

Leo unakuja tunachaji simu asilimia 10 unasepa.
 
Hapa Moshi mda huu ni giza tuu. Haipiti siku mbili umeme haujakatika kwa masaa 3-5
 
Sijakataa kwamba kuna shida ya upatikanaji wa umeme, hoja iliyotolewa ni kuwa hakuna taarifa yoyote juu ya hili. Kuna mtu amekwenda Tanesco kuuliza? Kifurushi chako cha simu kikiisha isivyo lazima uwapigie customer care, je unamawasiliano ya customer care services za Tanesco? Dharau sio! Utabaki hewani hivyo hivyo.
Sawa RCRo nimekupata
 
Hapo vip!!
Huku maeneo ya Ngulelo,Kimandolu sekei n.k umeme umekuwa unakatwa kuanzia saa 8 nane mchana mapaka siku inayofuatwa.

Kitu ambacho wananchi wenzangu wanalalamika ni kutopewa taarifa ili wapambane na hali ya hilisi kwasababu kuna watu wanategemea umeme kuingiza kipato.

Mfano wafanyabiashara wa samaki na nyama wanategemea umeme kuifadhi bidhaa zao zisiharibike.

Tunaomba TANESCO muache madharau..
Nyamagana tumeshazoea
 
Sema taarifa hazijakufikia, sio kimya kimya.
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)

TAARIFA YA KATIZO LA DHARURA-TANESCO MKOA WA ARUSHA


Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Mkoa wa Arusha,linawataarifu wateja wake kuwa,Kutakuwa na matengezo ya dharura katika kituo chetu kikubwa cha kupooza na kusambaza umeme Njiro kama ifuatavyo:-

Tarehe: 24/02/2021
Siku: Jumatano
Muda: 19:00 Jioni- Saa 22:00 usiku
Feeder: Industrial 3,Themi 1,Sakina na M5

Sababu Matengenezo ya dharura katika katika kituo chetu kikubwa cha kupooza na kusambaza umeme Njiro ili kuboresha hali ya upatikanaji wa umeme


Maeneo yanayoathirika Moshono,chekereni, boma siara,suye,baraa, olorieni,kokoriko, baadhi ya maeneo ya kijenge,Njiro PPF, Sunflag factory, Ngaramtoni Seliani, Ngaramtoni NMB, stand ya zamani Ngaramtoni, sokoni Ngaramtoni, Kimynaki, visima vya maji,Olkokora,mbuga nyeupe, Njiro nane nane,Njiro SDA, Chuo cha Uhasibu, ESAMI, Njiro kwa Tondi, Double B, Kikwakwaru A, Sunflug quarters, Njiro complex, Kambini, world vision, TBC,FFU ,Sekei yote, Olgilai, Ngiresi,Bangata, Midawe, Engokareti, Kwa mbotela, Songota, Olgilai kimeo, na baadhi ya maeneo ya jirani .


Ungozi unaomba radhi sana kwa usumbufu wowote utakaojitokeza

Kwa taarifa yoyote ya dharura tafadhali wasiliana nasi kupitia namba za simu zifuatazo:

Tanesco Arusha dawati la dharura, 0272610120 na 0758174343

Call centre: 0768985100 & 022194400

Huduma kwa wateja Arusha: 0737 894000


Imetolewa na : Ofisi ya Uhusiano na Huduma kwa wateja
TANESCO- Arusha
24/02/2021

Sio kweli! Chuga ngoma hamna tangu kitambo tu mbona! Wanakata hadi wanakera!
 
Hapa mbeya Kila siku kukatiwa umeme uhakika tunaenda wiki ya pili sasa
 
Tafuteni taarifa, kwa tabia hii ndio nyie mkiitwa kwenye vikao vya watoto shule hamuhudhurii mpaka jumba bovu limwangukie mwanao.

As long as upo connected na Tanesco hakikisha una namba za huduma kwa wateja.
...Asante mkuu kwa ushauri, but nishawapigia na majibu yao ni kuwa wanafanya maintenance..Lakini kiustaarabu hata kama ni maintanance inafanyika, kama wateja tuna haki ya kujulishwa in advance
 
Back
Top Bottom