Mgao umeisha hadi Januari - SERIKALI

Mgao umeisha hadi Januari - SERIKALI

Bajabiri

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2011
Posts
9,728
Reaction score
1,209
Serikali kupitia naibu waziri wa nishati na madin imesema kuwa kuanzia sasa mgao wa umeme umeshaisha hadi mwezi january,amesema kuwa hilo limesababishwa na kujaa kwa baadh ya mabwawa na pia kuna kampuni(jina nimelisahau)imeweza kuingza megawati kadhaa kwenye gridi ya TAIFA!
Je hapo ulipo kuna umeme?
Sosi:radio ONE
 
Kwahiyo siyo mgao umeisha bali wamepostpond tatizo..waache tu tutawanyonga hawa tena kama Gaddafi
 
Hao mafisadi tumeishawazoea kwa ahadi hewa. Hapo kachomekea neno MEGAWATT akidhani ataendelea kutuchanganya kumbe tumeishazoea saizi hilo neno. Huku kwetu Ngeleja wanamwita megawatt.
 
he, makubwa sasa sijaelewa kwa hiyo wamepospone hadi january, sasa huu mgao uliokuwepo si walisema unaisha desemba? mwe hii serikali jamani, kazi ipo, haya ngoja tusubiri tuone, i wish kama watanzania tungekuwa na maamuzi kama ya wazambia.
 
Mgao umeisha wapi! Huku tangibovu mbez beach mbona wamekata toka saa 2 na hatujui utarud saa ngap. Hi SERIKALI INABOA KINYAMA na ww Ngeleja kaa kimya
 
Stelling wa hii movie bwana ngeleja kafa nini? sasa naona amengia bwana Malima na hii tamdhilia ya Megawati party two! This is Kanumba movie party two ngoja tuone!
 
Hivi Viongozi wa Nchi hii wameenda Shule kweli??!!, Hivi inawezekana kweli Kiongozi ngazi ya Waziri wa Nchi hii unasimama kuitangazia Dunia kwamba mgao wa Umeme umeisha mpaka Januari, hii maana yake ni nini, kwamba miezi hii miwili ndio umeme utakuwepo then baada ya hapo tunarudi tena gizani. Ndio kusema kwamba ile mipango ya dharura ya kuleta Umeme wa Uhakika waliokuwa wakiinadi pale Bungeni ilikuwa ni kiini macho!!!.
Damn this Country
 
Ukitaka kujua kua viongozi wa nchi hii ni vilaza kumbuka kua Ngeleja katudanganya weeeeee sasa kaona hii ngoma ngoja ampigie pasi brotherman Malima, sasa Malima kaingia na vigezo vya kuwahadaa wananchi kua mgao hautakuwepo mpaka January mwaka kesho! baada ya hapo natumaini baraza la mawaziri litakua limebadilishwa kutokana na uongo huu wa Megawati halafu tena hii ngoma atachukua mtu mwingine na hii itatokana na vigezo vya ukame wa mvua mabwawa hayana maji! Happy 50 years ya uhuru wa wadanganyika.
 
Mtwara umeme hauna mtumiaji, mpaka kwenye mikorosho ukiegemea mkorosho umenasa!! Ila nasikia mpango umekamilika gesi itapelekwa Dar kwa bomba.. Hapo chacha!!
 
Msijali umeme wa kumwaga. Huko mbezi na tangi bovu si mnajua tunajenga barabara usiku na mchana. Kesho upo
 
Yaani amesema kwa miez mitatu tutakua free from MGAO!
 
Hahahaha Ngeleja anaunguzwa masaburi na Tanesco yake! Mbezi Bch hatuna umeme!
 
Yaani dk 20 baada ya maneno ya malima ktk taarifa ya habari umeme ukakata mpaka dk hii.....yule mh megawatt naona leo yuko off...,,blood megawatt*&%~.co.mteravijijini..!
 
achamatusi ya nguoni tumelala gizani tangu jana usiku na mpaka tunaondoka akuna chai sababu ya umeme
atutake radhi huyo mbwa
 
Serikali kupitia naibu waziri wa nishati na madin imesema kuwa kuanzia sasa mgao wa umeme umeshaisha hadi mwezi january,amesema kuwa hilo limesababishwa na kujaa kwa baadh ya mabwawa na pia kuna kampuni(jina nimelisahau)imeweza kuingza megawati kadhaa kwenye gridi ya TAIFA!
Je hapo ulipo kuna umeme?
Sosi:radio ONE
Huyo naibu waziri na waziri wake wanafiki tu. hakuna lolote. wanaogopa kisago bungeni maana Kikao cha Bunge cha mwezi wa 11 ndiyo kimekaribia. hawana lolote hao wajiuzuru tu. hamkumbuki wakati wa kupitisha bajeti ya wizara ya Nishati na madini? Umeme uliwaka mfululizo tukadhani tatizo limekwisha kumbe walitaka bajeti yao ipite!
 
Back
Top Bottom