Fidel80
JF-Expert Member
- May 3, 2008
- 21,947
- 4,445
UDSM ni wa UVCCM
Na Rehema Mwakasese
JESHI la Polisi nchini limesema mwanafunzi raia wa Uganda, Bw. Odong Kefa Odwar anayetuhumiwa kuwa kinara wa migomo mingi kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ni mwanachama hai wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) baada ya upekuzi aliofanyiwa kubaini kuwa na kadi ya umoja huo.
Kutokana na hali hiyo jeshi hilo linafanya uchunguzi aidi kubaini mtu aliyempatia mgeni huyo kadi hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkuu wa Kitengo cha Makosa dhidi ya Binadamu, Bw. Peter Kivuyo alisema kuwa mwanafunzi huyo alipatiwa kadi hiyo katika tawi la Chuo Kikuu mwaka 2006.
Bw. Kivuyo alisema kuwa namba ya kadi hiyo ni 711818 ambayo inaonesha kuwa ilitolewa Oktoba 25 huku pia upekuzi huo uliofanyika kwenye nyumba alikokuwa akiishi Mikocheni, Dar es Salaam, ukionesha kuwa Bw. Odwar alipatikana na daftari ambalo limeandikwa maneno yanayoashiria alikuwa anajihusisha na masuala ya kisiasa hapa nchini.
Bw. Kivuyo alisema katika uchunguzi walioufanya wamegundua kuwa mwanafunzi huyo alikuwa kinara wa kushawishi migomo ambayo ilikuwa imetokea katika vyuo vya hapa nchini.
Aidha alisema jeshi la polisi liliamua kumrudisha nchini kwao Uganda lakini Ofisi ya Uhamiaji ya Uganda imemzuia katika uwanja wa ndege wa nchini humo kwa sababu wanasubiri taarifa zaidi kutoka Tanzania ili hatua za kisheria zichukuliwe mkondo wake.
Naye Kaimu Kamishina wa Uhamiaji, Uthibiti, Huduma za Mipaka na Ukaguzi, Bw. Philo Nombo alisema kuwa walimpatia, Bw. Odwar kibali cha kuishi nchini kama mwanafunzi na akapatiwa taratibu zote zinazohusu kuishi nchini lakini kwa sababu amevunja sheria hana tena ruhusa ya kuishi nchini.
"Tulipata maelekezo kutoka Serikalini kuwa Bw. Odwar ameondolewa nchini mara moja kwa sababu amevunja taratibu za kuishi nchini nasi tulitekeleza agizo hilo," alidai Bw. Nombo.
My take;
Huyu jamaa angepatikana na card ya CHADEMA sijui wangemfanyaje maanake huo moto wake sijui!maana walikuwa wanasema CHADEMA wanahusika na migomo inayotokea sasa.
Na Rehema Mwakasese
JESHI la Polisi nchini limesema mwanafunzi raia wa Uganda, Bw. Odong Kefa Odwar anayetuhumiwa kuwa kinara wa migomo mingi kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ni mwanachama hai wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) baada ya upekuzi aliofanyiwa kubaini kuwa na kadi ya umoja huo.
Kutokana na hali hiyo jeshi hilo linafanya uchunguzi aidi kubaini mtu aliyempatia mgeni huyo kadi hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkuu wa Kitengo cha Makosa dhidi ya Binadamu, Bw. Peter Kivuyo alisema kuwa mwanafunzi huyo alipatiwa kadi hiyo katika tawi la Chuo Kikuu mwaka 2006.
Bw. Kivuyo alisema kuwa namba ya kadi hiyo ni 711818 ambayo inaonesha kuwa ilitolewa Oktoba 25 huku pia upekuzi huo uliofanyika kwenye nyumba alikokuwa akiishi Mikocheni, Dar es Salaam, ukionesha kuwa Bw. Odwar alipatikana na daftari ambalo limeandikwa maneno yanayoashiria alikuwa anajihusisha na masuala ya kisiasa hapa nchini.
Bw. Kivuyo alisema katika uchunguzi walioufanya wamegundua kuwa mwanafunzi huyo alikuwa kinara wa kushawishi migomo ambayo ilikuwa imetokea katika vyuo vya hapa nchini.
Aidha alisema jeshi la polisi liliamua kumrudisha nchini kwao Uganda lakini Ofisi ya Uhamiaji ya Uganda imemzuia katika uwanja wa ndege wa nchini humo kwa sababu wanasubiri taarifa zaidi kutoka Tanzania ili hatua za kisheria zichukuliwe mkondo wake.
Naye Kaimu Kamishina wa Uhamiaji, Uthibiti, Huduma za Mipaka na Ukaguzi, Bw. Philo Nombo alisema kuwa walimpatia, Bw. Odwar kibali cha kuishi nchini kama mwanafunzi na akapatiwa taratibu zote zinazohusu kuishi nchini lakini kwa sababu amevunja sheria hana tena ruhusa ya kuishi nchini.
"Tulipata maelekezo kutoka Serikalini kuwa Bw. Odwar ameondolewa nchini mara moja kwa sababu amevunja taratibu za kuishi nchini nasi tulitekeleza agizo hilo," alidai Bw. Nombo.
My take;
Huyu jamaa angepatikana na card ya CHADEMA sijui wangemfanyaje maanake huo moto wake sijui!maana walikuwa wanasema CHADEMA wanahusika na migomo inayotokea sasa.