Mfungwa aliyepata digrii akiwa gerezani, Haruna Pembe Gombela alifanya nini mpaka akafungwa?

Kumbe jamaa katoka. Jamaa katusua kweli bila shaka atajikita katika uwakili
 
Nilikuwa naangalia taarifa ya habari Channel Ten asubuhi leo wakimtaja Haruna Gombera ambaye alipata degree akiwa gerezani (kifungo cha maisha?) mwaka 2007, na sasa anafanya shahada ya juu akiwa "huru". Kuna yeyote anayejua kisa cha yeye kufungwa? Ni km alionewa akaamua kusomea sheria. Tafadhali napenda kufahamu kuhusu mtu huyu=
===========================================


Kwa wasio mjua wanaweza wakapitia hapa;

Mfungwa aliyepata digrii akiwa gerezani, Haruna Pembe Gombela alifanya nini mpaka akafungwa?
 
Niliendelea kudadisi mpaka nikakutana na hii habari. Pole sana Gombela kwa yote.


Na Happiness Katabazi
HATIMAYE Mahakama ya Rufani nchini imemfutia adhabu ya kifungo cha miaka 20 jela yule mfungwa aliyepata Shahada ya kwanza ya Sheria katika Chuo Kikuu Huria(OUT) akiwa gerezani,askari mpelelezi wa Jeshi la Polisi E.6937 D/C Haruna Pembe Gombela baada ya kubaini huku zote zilizotolewa na mahakama za chini zilimtia hatiani kimakosa.


Uamuzi huo wa Mahakama ya Rufani nchini unatokana na rufaa Na.44/2006 iliyokatwa mahakamani hapo na mrufani Gombela ambaye alikuwa akiishi katika Gereza Ukonga dhidi ya Jamhuri aliyoomba mahakama hiyo ya juu nchini itengue hukumu ya ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam iliyotolewa na Jaji Katherine Orioyo Oktoba 31 mwaka 2005, ambayo pia nayo ilikubaliana na hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Wilaya ya Ilala katika kesi ya unyang'anyi wa kutumia silaha Na.1426/1990 ambazo hukumu zote hizo zilimtia hatiani kwa kosa hilo na kumhukumu kwenda jela miaka 20.

Jopo la majaji watatu wa mahakama ya rufani waliokuwa wakisiliza rufaa ya Gombale ambalo lilikuwa likiongozwa na jaji Eusebio Mnuo,Steven Bwana na Sauda Mjasiri walisema hawana sababu ya kutofautiana na upande wa Jamhuri kwasababu jopo hilo limeridhika kuwa gwaride la utambulisho lilofanywa kumtambua mrufani halikuacha mashaka.

Jaji Mnuo alisema mahakama za chini zilimtia hatiani mrufani huyo kwa kuegemea ushahidi maelezo ya onyo yaliyotolewa kama ushahidi dhidi ya mrufani na ambapo mshtakiwa huyo wa tatu alishachiwa huru na mahakama za chini, ambapo jaji huyo alisema kwa mujibu wa kifungu cha 33(2) cha Sheria ya Ushahidi ya Tanzania ya mwaka 2002, vinasema ushahidi utakaotolewa na mshtakiwa mmoja dhidi ya mshtakiwa mwenzake ambao wanakabiliwa katika kesi mmoja, haupaswi kutumiwa na mahakama kumtia hatiani mshtakiwa mwingine ambao ushahidi huo ulimtaja.

"Kwa hiyo jopo hili linatamka wazi kuwa linatengua hukumu ya Mahakama Kuu iliyomtia hatiani Gombale kwasababu mahakama hiyo ya chini ilimtia hatiani kimakosa kwani mahakama hiyo ilimtia hatiani mrufani huyo kwa kuegemea ushahidi wa maelezo ya onyo ya mshtakiwa mwenzake na mrufani kwasababu kifungu cha 33(2) cha Sheria ya Ushahidi, kinakataza mshtakiwa mmoja kutiwa hatiani kwa ushahidi wa maelezo ya onyo ya mshtakiwa mwenzake ambaye anashtakiwa naye kwenye kesi moja na tuna amuru mshtakiwa huyo aachiriwe huru. "alisema Jaji Mnuo.

Gombela na wenzake ambao siyo wahusika katika rufaa hiyo, walifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala na kufunguliwa kesi unyang'anyi wa kutumia silaha Na.1426/1990 ambapo yeye alitiwa hatiani na wenzake kuachiliwa huru. Lakini Mkurugenzi wa Mashtaka nchini alidai adhabu hiyo ni ndogo na hivyo DPP alikata rufaa katika Mahakama Kuu ambayo ilipewa Na.155/1992 kwamba kosa walilotiwa nalo hatiani kisheria inapaswa wafungwe jela miaka 30 lakini akadai anashangwa na mahakama hiyo kuwafunga miaka 20 jela.

Wakati Mkurugenzi wa Mashtaka akiwasilisha rufaa hiyo Mahakama Kuu, pia Gombale alikata rufaa dhidi ya hukumu hiyo ambayo ilipewa Na. 84/1992 ambayo hata hivyo mahakama Kuu iliitupilia mbali ili kuruhusu warufani waudhulie katika rufaa Na.155/1992 ambayo nayo pia haikufanikiwa.

Ndipo Gombela alifikia uamuzi tena wa kukata rufaa katika Mahakama ya Rufaa ambao alitoa sababu nane za kukata rufaa ambapo alidai hukumu zilizotolewa dhidi yake na mahakama za chini ambazo zote zilimhukumu kwa kutumia ushahudi wa mshtakiwa mwenzake, mahakama ya wilaya ya Ilala haikufanya usikilizwaji wa awali wa kesi hiyo (PH) jambo ambalo ni kinyume na cha kifungu cha 192 cha Sheria ya Makosa ya Jinai ya mwaka 2002.

Itakumbukwa kuwa miaka ya hivi karibuni Gombale aliandika historia mpya ya kuwa mfungwa aliyefungwa gerezani lakini wakati akitumia adhabu yake katika gereza la Ukonga alipata fursa ya kujiendeleza kielimu ambapo alikuwa akijisomea Shahada ya Sheria katika Chuo Kikuu Huria (OUT) jijini Dar es Salaam, na kutunikiwa shahada hiyo, hali iliyofungua ukurasa mpya katika Magereza ya Tanzania, kuwa mtu kuwa mfungwa siyo kigezo cha kushindwa kujiendeleza kielimu.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi,Juni 18 mwaka 2011.
 
Hivi mtu ukifungwa jela ukatumikia miaka mingi kimakosa, ukija kushinda rufani serikali/mshitaki inakulipa fidia?!!
 
Back
Top Bottom