Septem
JF-Expert Member
- Feb 14, 2018
- 313
- 404
Kwanza natanguliza wazi mimi ni Muislam wa kuzaliwa na kuamini. Pia sina lengo la kukashifu dini yoyote au imani ya mtu. Bali najaribu kuelezea mambo yanayojili katika mwezi huu wa Ramadhani ambayo , kisheria na kiustaarab hayako sawa kabisa.
Nitaelezea jambo moja. Wenyewe tumezoea kuliita kupiga daku. Hizi ni ngoma wazozunguka vijana kupiga katikaajumba kwa lengo 'sijui ni lipi'. Nasema sijui ni lipi.
Kipindi cha nyuma ilikua zaidi wanazunga majumbani usiku kuamsha watu kula chakula cha usiku mkubwa(daku). Hivyo mantiki yake ilikua ni kuamsha watu, na walioamshwa waliwapa senti kidogo kama sadaka.
Kutokana na mabadiliko ya kiteknolojia-Siku hizi kuna alarms, pia suala la usalama kuwa dogo maeneo mengi hawa wamaepungua kufanya shughuli hii.
Lakini kupiga mchana sijui hasa mantiki yake ni nini.
Kilichonisukuma kuandika uzi huu ni hiki.
Leo mida ya mchana nilikua dinning, na bi mkubwa(mwenye shida ya pressure), na baadhi ya family members. Ghafla tukasikia ngoma zinapigwa ndani kwa nguvu wakiimba. Waliimba na kupiga ngoma kwa muda wa dakika takribani kumi. Finally nikatoka na kuanza kuwaeleza kuwa wanakosea, wakaanza kulalamika kuwa siwafanyii vyema, niwape sadaka waondoke. Sikuwapa hata sh moja, wakaendelea kupiga ngoma kwa takribani dakika 20, walipochoka wakaondoka.
Hii ni tabia kwa watu waliokulia mazingira ya mikoa ya kiislamu ni common sana.
Ni mazoea sana, ni tabia za kawaida. Lakini kiundani zina athari sana. Na inapashwa ikemewe sana.
1. Kuingia nyumba ya mtu bila kuruhusiwa hiyo ni trespassing na ni kosa kisheria, ukimkuta mtu aliye 'pinda', hawa vijana watalala 'ubaoni'.
2. Ni mwanzo na dalili za wizi.
3. Inaweza kuwa ni uchoraji wa mazingira ya ujambazi. Mchana daku usiku wanarudi ujambazi.
4. Inaweza sababisha mauaji. Mfano hawajui ni nani yumo ndani na ana maradhi gani, sauti za ghafla zinaweza kuleta mauti.
5. Si kila nyumba ni waislam, na hata kama ni waislamu si wote wanataka 'kelele' hizo.
Ndugu zangu waislam(hasa), tukemee suala hili na tuache kulilea, tunatengeza vibaka, na kulemaza kuacha kufanya kazi kutegemea kupewa 'sadaka'.
Nitaelezea jambo moja. Wenyewe tumezoea kuliita kupiga daku. Hizi ni ngoma wazozunguka vijana kupiga katikaajumba kwa lengo 'sijui ni lipi'. Nasema sijui ni lipi.
Kipindi cha nyuma ilikua zaidi wanazunga majumbani usiku kuamsha watu kula chakula cha usiku mkubwa(daku). Hivyo mantiki yake ilikua ni kuamsha watu, na walioamshwa waliwapa senti kidogo kama sadaka.
Kutokana na mabadiliko ya kiteknolojia-Siku hizi kuna alarms, pia suala la usalama kuwa dogo maeneo mengi hawa wamaepungua kufanya shughuli hii.
Lakini kupiga mchana sijui hasa mantiki yake ni nini.
Kilichonisukuma kuandika uzi huu ni hiki.
Leo mida ya mchana nilikua dinning, na bi mkubwa(mwenye shida ya pressure), na baadhi ya family members. Ghafla tukasikia ngoma zinapigwa ndani kwa nguvu wakiimba. Waliimba na kupiga ngoma kwa muda wa dakika takribani kumi. Finally nikatoka na kuanza kuwaeleza kuwa wanakosea, wakaanza kulalamika kuwa siwafanyii vyema, niwape sadaka waondoke. Sikuwapa hata sh moja, wakaendelea kupiga ngoma kwa takribani dakika 20, walipochoka wakaondoka.
Hii ni tabia kwa watu waliokulia mazingira ya mikoa ya kiislamu ni common sana.
Ni mazoea sana, ni tabia za kawaida. Lakini kiundani zina athari sana. Na inapashwa ikemewe sana.
1. Kuingia nyumba ya mtu bila kuruhusiwa hiyo ni trespassing na ni kosa kisheria, ukimkuta mtu aliye 'pinda', hawa vijana watalala 'ubaoni'.
2. Ni mwanzo na dalili za wizi.
3. Inaweza kuwa ni uchoraji wa mazingira ya ujambazi. Mchana daku usiku wanarudi ujambazi.
4. Inaweza sababisha mauaji. Mfano hawajui ni nani yumo ndani na ana maradhi gani, sauti za ghafla zinaweza kuleta mauti.
5. Si kila nyumba ni waislam, na hata kama ni waislamu si wote wanataka 'kelele' hizo.
Ndugu zangu waislam(hasa), tukemee suala hili na tuache kulilea, tunatengeza vibaka, na kulemaza kuacha kufanya kazi kutegemea kupewa 'sadaka'.
