avogadro
JF-Expert Member
- Apr 30, 2013
- 8,599
- 15,383
(Mimi ni mkatoliki lialia)
1. Nchi yetu wengi tumezaliwa tukajikuta kwenye nchi nyema ya ajabu ambapo wakristu na waislamu wanaishi pamoja kwa upendo
2.Unakuta kwenye familia moja kuna mchanganyiko wa dini lakini wanashirikiana pamoja kwenye mambo ya kiukoo bila kujua mwenzake ni dini gani
3. Ni Tanzania pekee muislamu anamnunulia mtoto wake nguo mpya siku ya krismass na kusherekea na watoto wenzake wa kikristo na virse versa kwa wakristu wakati wa idd lazima pilau la nguvu lipigwe
4. Ni Tanzania pekee akiwa anachinja kitoweo lazima amwite jirani yake muislamu amchinjie
5. Ni Tanzania pekee wakati wa mfungo wa ramadhani wakristu huvaa kanzu kama wavaao ndugu zao waislamu na mara nyingi kupunguza kula hadharani kwa hiari ili kutowakwaza ndugu zao waislam
6. Ni Tanzania pekee, wakati wa mfungo vijana hupita kuwaamsha watu kwa ngoma usiku wakati wa daku hata kwenye nyumba za kikrisu lakini tunavumiliana
7. Ni Tanzania pekee ambapo siku zikikaribia mfungo kuisha , vijana hao hupita kila nyumba bila kujali dini na kuzawadiwa.
8. Kwa taarifa yako mtoa mada, wengi wanaowatunza vijana hao ni wakristu. Kwanza wanawapongeza vijana hao ambao nje ya dini ni wanajamii wenza kwa kuweza kulinda imani yao pili kinaendelea kukuza mashirikiano kati ya dini zote mbili.
9. Mimi nashauri tuendelee kutunza utamaduni huo ambao tumeuridhi kwani ni moja wapo ya vitu vinavyofanya nchi yetu kuwa na baraka na dini kuheshimiana tofauti na chi nyingine ambazo hizi dini watu wanagombana
1. Nchi yetu wengi tumezaliwa tukajikuta kwenye nchi nyema ya ajabu ambapo wakristu na waislamu wanaishi pamoja kwa upendo
2.Unakuta kwenye familia moja kuna mchanganyiko wa dini lakini wanashirikiana pamoja kwenye mambo ya kiukoo bila kujua mwenzake ni dini gani
3. Ni Tanzania pekee muislamu anamnunulia mtoto wake nguo mpya siku ya krismass na kusherekea na watoto wenzake wa kikristo na virse versa kwa wakristu wakati wa idd lazima pilau la nguvu lipigwe
4. Ni Tanzania pekee akiwa anachinja kitoweo lazima amwite jirani yake muislamu amchinjie
5. Ni Tanzania pekee wakati wa mfungo wa ramadhani wakristu huvaa kanzu kama wavaao ndugu zao waislamu na mara nyingi kupunguza kula hadharani kwa hiari ili kutowakwaza ndugu zao waislam
6. Ni Tanzania pekee, wakati wa mfungo vijana hupita kuwaamsha watu kwa ngoma usiku wakati wa daku hata kwenye nyumba za kikrisu lakini tunavumiliana
7. Ni Tanzania pekee ambapo siku zikikaribia mfungo kuisha , vijana hao hupita kila nyumba bila kujali dini na kuzawadiwa.
8. Kwa taarifa yako mtoa mada, wengi wanaowatunza vijana hao ni wakristu. Kwanza wanawapongeza vijana hao ambao nje ya dini ni wanajamii wenza kwa kuweza kulinda imani yao pili kinaendelea kukuza mashirikiano kati ya dini zote mbili.
9. Mimi nashauri tuendelee kutunza utamaduni huo ambao tumeuridhi kwani ni moja wapo ya vitu vinavyofanya nchi yetu kuwa na baraka na dini kuheshimiana tofauti na chi nyingine ambazo hizi dini watu wanagombana
