Mfumo wa udhibiti ubora na ufanisi kazini: Utendaji wa watumishi wa umma wengi ni upuuzi, lazima udhibitiwe

Ģ moningiiii

"Watanzania kila mtu anakwambia ukingiia kwenye system tu bhas muhimu kuingia" kila Mtanzania hasa maskini ndoto zao ni kufanya kazi serikalini si kwasababu ya ubora wa mwajili tu ila ni kwasababu ya udhaifu wa mwajiri, serikalini huko ndo unaweza kuwa mlevi na usifukuzwe kazi ukashushwa vyeo tu lakini pia huko hakuna uangalizi mkubwa sana wa matumizi ya anayeshikilia ofisi mtu kujenga kibanda cha mlinzi kwa 20m ni kawaida na uulizwii.

Wafanyakazi wa baadhi ya mashirika ni pasua kichwa huduma mbovu lakini pia hawajali wanao wapa huduma kabisaa yanii ukiwa mfanyakazi serikalini hata uwe chizi unaweza fanya kazi hadi unastaafu kama meneja na wasikujue.

Wananchi million 60 tunakatwa kodi kusaidia kuendesha shughuli za serikali sisi ndo waajiri wa wao lakini hatuna uwezo wa kuwajibisha kiongozi mmoja mwenye madaraka yote anaweza mlinda yoyote na asisikilize walipa kodi wanaotoa mapato yao ili wao wapate v8 new model kila mwaka kufanya shughuli zao.

Kwa kiasi kikubwa wananchi tunajitaidi kutekeleza wajibu ili serikali iwe na nguvu na watendaji wake wapate ujira kuendelea kuwajibika kwa manufaa yetu sote, lakini ni kama wanajitenga na sisi na kuona sisi si sehemu yao wanafanya majukumu yao si kwa manufaaa yetu sote.

KWANINI SASA TUSIWE NA MFUMO WA DATA UTAKAO PIMA UTENDAJI NA UFANISI WA WATENDAJI WA JUU WA KILA ENEO NA KUTOA RATE YA PERFOMANCE KWA MWAKA NA WANANCHI WAWEZE KUONA PERFORMANCE KWA KILA ENEO KULINGANA NA UBORA WA UFANISI UTAKAO WEKWA.

Yani hapa naamanisha tuwe na kitengo cha ubora chini ya ofisi ya raisi kitakachokuwa kimeandaa mfumo maalumu wa DATA ANALYSIS utakao kuwa umepanga standards , malengo,dira, wajibu na nia za kila nafasi kubwa kama mawaziri, ceo wa mashirika, RC,DC,wakurugenzi, then waweke indicators kupima kila kilichopangwa na standards zake.

Kwa mfano, waziri mkuu awe amewekewa lengo la kugundua matatizo yanayorudisha nyuma ufanisi wa serikali na uondoaji wa tatizo husika na uboreshaji wa shughuli za serikali then tuseme kwa mwaka awe angalau amedetect matatizo 25 na ameyatatua na kutoa njia mpya katika maeneo hayo matatizo yaliyopotokea.

Mfano pia mkuu wa shirika la labda Tanesco awekewe lengo la kuvumbua njia mpya zitakazoweza kuzalisha umeme katika maeneo ya mkoani ili kufanya kila mkoa kuzalisha umeme na kuchangia katika gridi ya taifa na baada ya mwaka awe ameweza kutoa walau njia za uzalishaji katika mikoa 3.

Nb. Hii ni mifano tu ili mnielewe nachojaribu kuwaza ili kuongeza uwajibakaji na ufanisi na kupunguza wazembe

kupitia mifano hiyo kwa kila nafasi kulingana na rasilimali zinavyo ruhusu mwisho wa mwaka tuone performance labda waziri mkuu performance yake ni 60% kwasababu moja mbili tatu na itungwe sheria mfanyakazi asiyefika 50% atakatwa 25% ya mshahara wake kwa mwaka ujao wa fedha, akifanya chini ya 50% kwa miaka miwili mfufulizo atafukuzwa kazi na kutoruhusiwa kuomba kazi yoyote serikalini kwa kipindi cha miaka mitatu.

Na mfumo huu uwe wa wazi online kila mwananchi (waajir) waweze kuona ufanisi wa waliowapa dhamana .

Sijui nmewaza vyema au hangover inanisumbua.
Hili ni kweli ofisi karibu Zote za sirikali na mashirika ya umma , huduma ni mbovu
 
Siku zote mtoto anajifunza tabia mbaya kutoka kwa wakubwa zake. Kama viongozi wa juu wanavurunda, ndiyo utegemee wale wa chini yao kufanya vizuri?
Mfumo unahusu viongozi wa juu hasa wenye dhamana nzito kama waziri mkuu pia
 
Umenikumbusha Jumapili nilienda kwenye training ya mfumo utakaochukua nafasi ya OPRAS. Comments nyingi zilikuwa zinahusu unapotaka kumdhibiti mtu, kwanza boresha maslahi yake.

Kifupi, nilichokisikia pale ni kuwa mfumo utahujumiwa kama vilivyohujumiwa vingine.
WANANCHI ndio wa hovyo mfumo kama huo wa uwajibakaji hauwezi kuhujumiwa kwa nchi kama wananchi wanapambania haki zao, raisi akiwa weak wananchi watakuwa mwiba kila Mtu ataogopa.
 
Wazo zuri.
Hata mfumo huu uliopo upo vizuri Sana.

Shida inaanzia hata mazingira ya waajiriwa asilimia kubwa ni mabovu kupindukia.

Ni Sawa unataka Performance ya 100% wakati hata wewe commitment yako haivuki 50%.

Huwezi kupata matokeo unayotaka.
 
Wanahitaji kutafutiwa tiba na nguvu ya wananchi sema wananchi wenyewe ndo hamna bongo
Lakini wanaotakiwa watu wa Kwanza kwenye uthibiti ubora ni viongozi wao sehemu za kazi , lakini ndio hivyo tena
 
Wazo zuri.
Hata mfumo huu uliopo upo vizuri Sana.

Shida inaanzia hata mazingira ya waajiriwa asilimia kubwa ni mabovu kupindukia.

Ni Sawa unataka Performance ya 100% wakati hata wewe commitment yako haivuki 50%.

Huwezi kupata matokeo unayotaka.
Unajua tusiwaangalie watumishi wadogo em tuwaangalie hawa mapapa walio kwenye maeneo nyeti, resources izo ndogo zinatumika kweli ipasavyo kaka?
 
Unajua tusiwaangalie watumishi wadogo em tuwaangalie hawa mapapa walio kwenye maeneo nyeti, resources izo ndogo zinatumika kweli ipasavyo kaka?
Kwa hilo sikupingi, Kwa hao wakubwa ni sahihi Kabisa Kwa sababu resources zote wanazo na haki zote wanazostahili wanapata.

Ila Kwa hawa wa chini Kwa mazingira ya Sasa watawaonea tu.
 
Kwa hilo sikupingi, Kwa hao wakubwa ni sahihi Kabisa Kwa sababu resources zote wanazo na haki zote wanazostahili wanapata.

Ila Kwa hawa wa chini Kwa mazingira ya Sasa watawaonea tu.
Halmshauri zina ufujajj wa kila aina na wakurugenzi ma DC ma Rc WaPo miaka nenda miaka rudi, utasikia wanakwambia huo ni mfumo upo toka uhuru ukileta ujuaji watakuondoa.
 
Back
Top Bottom