Mfanyabiashara bilionea Dar es Salaam, adai kutishiwa maisha, akimbia kwa pikipiki kutoroka asiuawe hadi Arusha

Huyo mfanya biashara ni mpumbavu tu.
Yaani anaharibu maisha yake kwasababu ya 125 milioni, alafu anajiita milionea..🤔
Mkuu hujamuelewa mhusika ungesoma vizuri kuna kipengele cha kuvunja oda kwa mchina kaambiwa atalipa faini ya dola 18000 plus na hiyo millioni 129 arudishe je, huo mkataba uliosainiwa na wakakubaliana una maana gani sasa au kwasababu yeye ni kigogo serikalini. Kuna vitu vingine mtu anafosi kwasababu yupo kwenye cheo fulani na ndo maana hatuwezi kwenda popote pale kwan huo mkataba si ulisainiwa na mtu kaweka oda je unasitisha oda na ulipe faini pamoja na kurudisha hela uliyowekewa au maisha yako yaende na maji na pia uangalie hustling ulizopiga mapaka umekuwa level za kuitwa millionea ila kama huo umillionea uliupata kwa mseleleko baridi, utalipa faini pamoja na kurudisha pesa.
 
Usinifanye unaijua sana sheria mkuu, hata mimi naijua pia.
Hapa kwenye hili tukio la huyu mfanya biashara option alionayo ni kuchagua uhai/uhuru ama lolote kumtokea.
Yaani anacho kifanya kwa sasa ni kushindana na walio mzidi nguvu kwasababu anatafuta haki. Wakati mwingine tunapaswa kukubali kupoteza pesa na mali ili kunusuru nafsi zetu mkuu.
Na usisahau kwamba awamu hii mwenye nguvu ndio anahaki
Mwanaume kukubali mambo kirahisi rahisi ni dalili mbaya sana
Ndo maana tunataifa lenye mambo ya hovyo sababu hatuna wanaume wakupigania haki zao kama wewe mtu anaweza akaja akakupiga makofi mbele ya famila yako ukamwacha sababu ana nguvu

Nauhakika wewe sio mfanyabiashara ndo maana unaongea kirahis
 
Itakuwa hao watu walitaka kuiibia kampuni au kutakatisha pesa na walipata ugumu wa kuwa wanadraw hela cash 129M au kuingiza pesa kwa mtu wa kawaida.
I
kabidi sasa wanaandae nyaraka mbalimbali kuonesha wameoda malori kwa huyo bilionea na wanafanya miamala kwenda kwenye akaunti ya mfanyabiashara na mwisho wa siku wanaenda kwa mfanyabiashara kuzichukua kwa sababu yeye hatiliwi shaka na watu wa benk kwa sababu yeye ni mtu wa miamala.
Hiyo ndo nia yao kutakatisha fedha kwa hiyo hata huo mpango ni wa uongo
 
Mkuu hujamuelewa mhusika ungesoma vizuri kuna kipengele cha kuvunja oda kwa mchina kaambiwa atalipa faini ya dola 18000 plus na hiyo millioni 129 arudishe je, huo mkataba uliosainiwa na wakakubaliana una maana gani sasa au kwasababu yeye ni kigogo serikalini. Kuna vitu vingine mtu anafosi kwasababu yupo kwenye cheo fulani na ndo maana hatuwezi kwenda popote pale kwan huo mkataba si ulisainiwa na mtu kaweka oda je unasitisha oda na ulipe faini pamoja na kurudisha hela uliyowekewa au maisha yako yaende na maji na pia uangalie hustling ulizopiga mapaka umekuwa level za kuitwa millionea ila kama huo umillionea uliupata kwa mseleleko baridi, utalipa faini pamoja na kurudisha pesa.
Ndo maana nikamwambia yeye sio mfanyabiashara na kama ni mwanaume ni hasara kubwa sana kwa familia yake

Mkataba una-taratibu za kuuvunja hauvunjwi kihuni huni alafu kwenye a real man hutakiwi kukubali mambo kirahisi rahis mtu anaweza akaja akakupiga makofi mbele ya famila yako ukamwacha sababu ana nguvu

Huyo kigogo angetakiwa ampange huyo muuza magari mapema kwamba nakupa hela ila baadae utanrudishia na tunasign mkataba kila kitu
Tatizo vigogo wanatumia nguvu na akili kidogo
 
Umeniongezea kitu, kila siku ni kujifunza..

Madhara yake ni yapi?
Madhara yake wanaweza kuchukua zote zilizomo kwenye akaunti. Kwa mfano, unashika simu yako ile tu umeweka password unaanza kutuma unapigwa na kitako cha bunduki kichwani unazimia, halafu wao wanaendelea na mchakato. Ukizinduka wanakurudisha nyumbani kiroho safi au hata kuuawa. Wakikuacha mzima kucheki salio limepungua au limeisha kabisa. Kama una ujasiri ndio utaanza kulalamika na kumuomba rais aingilie kati.
 
Ingia mkataba na taasisi ya umma say kujenga daraja, halafu usijenge simply tu umepata kazi nyingine. Halafu uone nini kitakukuta kwa mujibu wa mkataba na Procurement Act. Huwezi kuamka tu asubuhi, umeshauriana na mkeo usiku unasema nimeghairi. Wanaomuona Shami mpuuzi ni ignorants.
 
Ndo maana nikamwambia yeye sio mfanyabiashara na kama ni mwanaume ni hasara kubwa sana kwa familia yake

Mkataba una-taratibu za kuuvunja hauvunjwi kihuni huni alafu kwenye a real man hutakiwi kukubali mambo kirahisi rahis mtu anaweza akaja akakupiga makofi mbele ya famila yako ukamwacha sababu ana nguvu
Kwa picha ilivyo, mfanyabiashara akivunja mkataba kienyeji na kuwapa pesa hao watu kienyeji, ipo siku atadaiwa malori na kampuni kwa sababu nyaraka za kampuni zinaonesha wameoda magari kwa huyo mfanyabiashara.
 
Hana maelezo kwamba alitishiwa atauwawa.
Ila matendo yake amekua na hofu atauwawa.
Shamy kacheza faulo. Yeye anajinadi kila siku ana uwezo wa kuagiza malori. Watu wamemuamini. Ila anawapiga watu kalenda. Magari anayoyauza. Ukiona mtu kaagiza ujue ana tenda muhimu sana. Naa malipo sio ya kutakatisha. Watu wanatoa hela mfukoni. Wanafanya transaction according tu kipato hizo gari ni gharama. Huwezi toa tu bilioni kijinga.
Transaction iliyotakiwa ni kudeposit kwa wachina. Hela ampewa. Ila analeta ujanja anataka full payment. Huu ujanja huyo mzee anataka kuondoka na hela za watu. Watamlawiti. Si issue sijui mtu mkubwa serikalini. Hata kijana tu wa mtaani akupe hiyo hela umzingue anakulawiti wallahi
 
Ndo maana nikamwambia yeye sio mfanyabiashara na kama ni mwanaume ni hasara kubwa sana kwa familia yake

Mkataba una-taratibu za kuuvunja hauvunjwi kihuni huni alafu kwenye a real man hutakiwi kukubali mambo kirahisi rahis mtu anaweza akaja akakupiga makofi mbele ya famila yako ukamwacha sababu ana nguvu

Huyo kigogo angetakiwa ampange huyo muuza magari mapema kwamba nakupa hela ila baadae utanrudishia na tunasign mkataba kila kitu
Tatizo vigogo wanatumia nguvu na akili kidogo
Umeeleweka mkuu kabisa sio mtu kwasababu ni mkubwa serikalini ndo afanye anachotaka hapana afuate vipengele vya mkataba vinasemaje.
 
Kwa picha ilivyo, mfanyabiashara akivunja mkataba kienyeji na kuwapa pesa hao watu kienyeji, ipo siku atadaiwa malori na kampuni kwa sababu nyaraka za kampuni zinaonesha wameoda magari kwa huyo mfanyabiashara.
Hio ndo point yangu na kuna jamaa nimemwambia hapo juu
Kuna siku atakuja tena atakuambia tuliingia mkataba wa million 900 wa kuleta malori na hukuleta na unatakiwa ulipe

Mambo ya mikataba hayaendi kienyeji enyeji watu wengi hawaeleweli pale hakuna ubinaadamu ni mkataba unasemaje
 
Mfanyabiashara maarufu wa Magari Jijini Dar es salaam, Samweli Shami maarufu Bilionea Shami, amedai kutishiwa maisha na watu aliodai ni vigogo wa polisi jijini humo na kulazimika kuyakimbia makazi yake kutoka dar akitumia usafiri wa pikipiki na kukimbilia jijini Arusha.

Akiongea na vyombo vya habari jijini Arusha, Bilionea Shami ambaye anamiliki kampuni ya magari ya Ongezeko Trading Co ltd,alisema amelazimika kuishi kama digidigi kwa takribani mwezi mmoja kuwakimbia polisi waliokuwa wakimsaka kwa madai kwamba wametumwa na kigogo wa serikali.

Alidai kupigiwa simu na Kamanda wa polisi kanda maalumu ya dar es salaam, Muliro Jumanne Muliro akimtaka kurejesha kiasi cha sh milioni 129 alizopokea kama Malipo ya awali kwenye mkataba wa sh milioni 958 waliokubaliana kuiuzia malori 9 ya mtumba yenye tela zake ,kampuni ya Afrinexus Logistics ltd ya mjini Mtwara baada ya kampuni hiyo kuvunja mkataba kinyume na utaratibu.

Shami alisema kampuni yake ya Ongezeko Trading co Ltd ya jijini dar es salaam, iliingia makubaliano hayo September 12, 2023 ya kuiuzia malori kampuni hiyo ya Afrinexus Logistics kwa makubaliano kwamba baada ya siku 21 za kazi malori hayo yangeingia nchini kutoka China.

Alisema baada ya makubaliano hayo, kampuni ya Afrinexus Logistics ilianza kuingiza fedha kidogo kidogo kwa awamu 6 kwenye akaunti yake ambapo siku ya kwanza aliingiziwa sh milioni 27.2,siku inayofuata sh mil 25.5, sh milioni 16.15, sh milioni 29.57, sh milioni 5.1, na sh milioni 25.5 na fedha hizo kufikia jumla ya sh, milioni 129 .

"Niliwauliza kwanini wanaingiza fedha kidogo kidogo, walinijibu ni masuala ya kibiashara, hawawezi kutoa fedha zote kwa mkupuo mmoja "

"Baada ya malipo hayo ya awali ,kampuni ya Afrinexus Logistics walinipigia simu kuniambia kuwa wameshapata malori ya haraka hivyo hawatahitaji tena,jambo ambalo ni kinyume na utaratibu "

"Niliwauliza itakuwaje na mimi nilishatoa oda China, waliniambia nisijali tutaongea,basi niliwajulisha huko mchina waliniambia walishafanya oda kwenye meli na itanilazimu wanikate dola 18,000 "

Alisema mapema mwaka huu, Februari 3,alipigiwa simu na Kamanda Muliro akimwambia afike ifisini kwake na baada ya kuitikia wito huo akiwa na mwanasheria wake,Muliro alimwambia ameagizwa na kiongozi mkubwa wa serikali(jina tunalo) arejeshe kiasi cha sh,milioni 129 huku akimsisitiza kuwa hatatoka ofisini kwake bila kutoa kiasi hicho cha fedha .

"Nilifika ofisi ya Kamanda Muliro nilimkuta akiwa katika hali ya kupaniki akawa ananifokea sana kuniambia kunatuhuma kutoka kwa mtu mkubwa sana serikalini kuwa wewe ni tapeli umefanya biashara za kitapeli lipa pesa za watu,nilijitahidi kumuuliza iwapo kama ameona mkataba wa mauziano aliniambia hahitaji mkataba lipa pesa za watu"

"Baada ya mabishano ya muda mrefu sana Kamanda Muliro aliniambia ndugu yangu Samweli wewe ni mdogo wangu usibishane na dola ukishaambiwa mtu ameshika mpini wewe umeshika makali hauta muweza, nakushauri kama mdogo wangu nenda kalipe hizo fedha na kuanzia sasa hutatoka hapa mpaka utuambie utalipaje hizo fedha"

Nikiwa hapo ofisini walinibana sana na kushikilia gari yangu na baadaye waliniambia nijidhamini nilienda nyumbani na kesho yake nilirejea ofisini kwa kamanda Muliro, waliendelea kunibana nikapiga simu kwa rafiki yangu akanikopesa milioni 20,tulienda benki usiku na askari polisi tukachukua pesa na kuziingiza kwenye akaunti ya Afrinexus Logistics na baadaye walinirejeshea gari yangu kwa masharti nikalipe fedha hizo"

Alisema askari hao wakiongozwa na Kamanda Muliro waliendelea kumpigia simu yeye pamoja na mke wake wakimwambia kwamba asipolipa hizo fedha watamfungulia kesi yoyote na wamekamata lori lake lililokuwa Mkoani Simiyu wakishinikiza alete pesa na wametishia kuliuza iwapo ataendele kukaidi .

"Wameingilia mawasiliano yangu ya simu na akaunti zangu za benki kila pesa inayoingia wanaona na wametishia kuzima WhatsApp yangu niliamua kwenda kulala hotelini ila walinifuatilia na kuja kuzingira hoteli niliyolala"

"Nilifanikiwa kutoroka kwa kutumia usafiri wa bodaboda hadi mto Wami nilipofanikiwa kupata usafiri mwingine wa kuja Arusha"

Alisema kwa sasa anajipanga kulifikisha suala hili mahakamani na tayari ameanza mchakato wa kukutana na mwanasheria wake ili likaamuliwe kisheria kuliko utaratibu unaotumiwa na upande wa pili wa kutumia nguvu ya polisi.

"Kwa sasa polisi wananitishi maisha wanasema hao unaosikia wanaonekana kwenye viroba ni watu kama wewe"

Samweli alimwomba Rais Samia Suluhu Hassan kuingilia kati suala hili kwa kuwa yeye ni Mfanyabiashara anayetambulika ili suala hili liamuliwe kisheria.

Kamanda Muliro hakuweza kutoa ushirikianao baada ya kupigiwa simu akidai yupo kwenye msiba wa Hayati ALLY HASSAN MWINYI.


Ends..
Jamani jamani jamani. Hakuna aliye salama kwenye utawala huu. Uwe tajiri uwe fukara mambo ni yale yale. Ni suala la muda tu. Suluhisho pekee ni kuungana pamoja na kudai katiba mpya ambayo itawatoa CCM na vibaka kama kina Muliro. Mwenye kusikia na asikie.
 
Umeeleweka mkuu kabisa sio mtu kwasababu ni mkubwa serikalini ndo afanye anachotaka hapana afuate vipengele vya mkataba vinasemaje.
Hata kama Huna kitu au huna mamlaka usikubali kuwa zoba kwenye maisha

Unaweza ukatumia ubinadamu kumbe watu wanaroho mbaya kinoma
Na unaweza vunja mkataba kienyeji sababu hao watu ni wahuni
Kuna siku atakuja tena atakuambia tuliingia mkataba wa million 900 wa kuleta malori na hukuleta na unatakiwa ulipe

Mambo ya mikataba hayaendi kienyeji enyeji watu wengi hawaeleweli pale hakuna ubinaadamu ni mkataba unasemaje na maslai
 
Back
Top Bottom