Mfanyabiashara ashusha tuhuma nzito kwa RTO Arusha

Jembe Jembe

JF-Expert Member
Jun 9, 2016
749
1,797
Mfanyabiashara na Mmiliki wa Mabasi ya kusafirisha abiria mikoani kutoka kampuni ya KIMOTCO ,Benedict Mberesero,amewalalamikia askari wa usalama barabarani katika Jiji la Arusha,kwa vitendo vya Rushwa iliyokithiri akidai wamegeuka mamlaka ya mapato TRA.

Akiongea katika kikao cha wadau wa usafirishaji jijini Arusha,mbele ya Kamanda wa Kikosi cha usalama barabarani Nchini,(SACP)Futunatus Musilimu, alimshutumu Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani Mkoa wa Arusha ,RTO Joseph Bukombe kuwa amekuwa kinara kwa kuongoza kikosi cha askari kukusanya Rushwa kutoka kwa wasafirishaji .

Amedai kuwa vibanda vya ukaguzi wa mabasi katika eneo la kituo kikuu cha mabasi jijini hapa ,vimegeuka vibanda vya kukusanya Rushwa kwa mabasi mbalimbali yanayoelekea mikoani na fedha hizo huwasilishwa kwa wakubwa .

"Napenda niseme ya Moyoni naona watu wamekuwa waoga kusema ,ukweli ni kwamba suala la Rushwa ni kubwa kwa Trafiki hapa Arusha naomba uchunguze mwenyewe ujionee" Alisema Ben

Aliongeza kuwa hivi karibuni alibambikiwa kesi ya matumizi mabaya ya Silaha ambapo alipigwa na askari wa usalama barabarani na kutupwa selo kituo cha Polisi kwa makosa aliyodai ni ya usalama barabarani.

"Namshukuru RPC alilishughulikia suala langu na bila yeye bila shaka ningekuwa nimefungwa kwa kubambikiwa kesi za uongo kwani si kweli kwamba Mimi nilitishia askari kwa silaha" Alisema .

Alimtuhumu RTO Bukombe kutoa ushirikiano pindi anapopigiwa Simu kwa nia ya kuomba msaada.

Akijibu hoja hizo ,RTO Bukombe Alisema tuhuma zilizoelekezwa kwake hazina ukweli Bali ni chiki zilizolenga kumchafua.

Alisema mabasi ya Kimotco yanaongoza kwa kuvunja sheria za usalama barabarani na pindi anapochukua hatua inaonekana kwamba RTO Bukombe mbaya na kuanza kumchafua kwa kusema askari anawatuma kukusanya Rushwa.

Ends.....
IMG_20190703_145229.jpeg
 
Amedai kuwa vibanda vya ukaguzi wa mabasi katika eneo la kituo kikuu cha mabasi jijini hapa ,vimegeuka vibanda vya kukusanya Rushwa kwa mabasi mbalimbali yanayoelekea mikoani na fedha hizo huwasilishwa kwa wakubwa .

"Napenda niseme ya Moyoni naona watu wamekuwa waoga kusema ,ukweli ni kwamba suala la Rushwa ni kubwa kwa Trafiki hapa Arusha naomba uchunguze mwenyewe ujionee" Alisema Ben


Hi huwa najiuliza kwanini PCCB hawawakamati traffic police na wanasikia malalamiko ya wananchi kila siku, lakini pia mamlaka zinazohusika kwanini zinashindwa kuweka maeneo maalumu ya ukaguzi wa magari na maeneo hayo kufungwe CCTV cameras for transparency reasons?

Mimi naona tunatumia gharama kubwa kujifanya tynadhibiti hili mara lile wakati mambo hayo yangeweza kufanywa kisayansi zaidi ili kupunguza gharama za kuajiri wala rushwa
 
Mfanyabiashara na Mmiliki wa Mabasi ya kusafirisha abiria mikoani kutoka kampuni ya KIMOTCO ,Benedict Mberesero,amewalalamikia askari wa usalama barabarani katika Jiji la Arusha,kwa vitendo vya Rushwa iliyokithiri akidai wamegeuka mamlaka ya mapato TRA.

Akiongea katika kikao cha wadau wa usafirishaji jijini Arusha,mbele ya Kamanda wa Kikosi cha usalama barabarani Nchini,(SACP)Futunatus Musilimu, alimshutumu Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani Mkoa wa Arusha ,RTO Joseph Bukombe kuwa amekuwa kinara kwa kuongoza kikosi cha askari kukusanya Rushwa kutoka kwa wasafirishaji .

Amedai kuwa vibanda vya ukaguzi wa mabasi katika eneo la kituo kikuu cha mabasi jijini hapa ,vimegeuka vibanda vya kukusanya Rushwa kwa mabasi mbalimbali yanayoelekea mikoani na fedha hizo huwasilishwa kwa wakubwa .

"Napenda niseme ya Moyoni naona watu wamekuwa waoga kusema ,ukweli ni kwamba suala la Rushwa ni kubwa kwa Trafiki hapa Arusha naomba uchunguze mwenyewe ujionee" Alisema Ben

Aliongeza kuwa hivi karibuni alibambikiwa kesi ya matumizi mabaya ya Silaha ambapo alipigwa na askari wa usalama barabarani na kutupwa selo kituo cha Polisi kwa makosa aliyodai ni ya usalama barabarani.

"Namshukuru RPC alilishughulikia suala langu na bila yeye bila shaka ningekuwa nimefungwa kwa kubambikiwa kesi za uongo kwani si kweli kwamba Mimi nilitishia askari kwa silaha" Alisema .

Alimtuhumu RTO Bukombe kutoa ushirikiano pindi anapopigiwa Simu kwa nia ya kuomba msaada.

Akijibu hoja hizo ,RTO Bukombe Alisema tuhuma zilizoelekezwa kwake hazina ukweli Bali ni chiki zilizolenga kumchafua.

Alisema mabasi ya Kimotco yanaongoza kwa kuvunja sheria za usalama barabarani na pindi anapochukua hatua inaonekana kwamba RTO Bukombe mbaya na kuanza kumchafua kwa kusema askari anawatuma kukusanya Rushwa.

Ends.....View attachment 1145584
Kama Muslim haamua kumlinda huyu RTO naungana na Ben.. Trafiki Arusha ni tatizo kubwa. Na hii inachangiwa na wingi wao barabarani. Yaani kutoka kwa Morombo kwa mfano, hadi ufike posta mpya kuna vituo vya askari wa usalama barabarani zaidi ya saba. Unajiuliza hivi kuna umuhimu gani wa vituo vyote hivyo? Zaidi ya usumbufu.. Na kuongeza foleni. Kwa rushwa niseme kwa Tanzania nzima Trafic Arusha wanaongoza. Huwezi kusimamishwa hata kama huna kosa usiwaachie polisi chochote. Inahitajika mageuzi makubwa sana trafiki Arusha. Nazunguka maeneo mengi Tanzania lakini Arusha ni kiboko kwa rushwa na usumbufu usio na maana. rto asiseme kuna chuki.
 
Mtu akiniambia eti sasa hivi rushwa imedhibitiwa huwa namuona hajui asemalo. Kwa sasa rushwa imeshika kasi, bali kinachofanyika ni kutoripotiwa na vyombo vya habari ili serikali ipakwe mafuta kwa mfano mgongo wa chupa kwamba inafanya kazi. Ukweli ni kuwa rushwa iko palepale bali haitangazwi. Ushahidi wa rushwa kwamba bado ipo sana, ni ile majuzi wafanyabishara walipokutana na rais na kuamua kufunguka. 90% walionyesha kwamba rushwa ipo. Namuunga mkono huyo Mberesero kwani kasema ukweli.
 
Ukweli ni kwamba Jeshi la Polisi na TRA baeo ni vinara wa rushwa. Nitaamini kuwa PCCB inafanya kazi siku nitakapoona inashughulika na Polisi na TRA. Mpaka sasa sijaona jitihada zozote za PCCB dhidi ya taasisi hizi mbili vinara wa rushwa.

PCCB siku hizi inaongozwa na Mapolisi. Hii limefajika makusidi ili iwe rahisi kuihibiti na ipoteze uhuru wa kufanya kazi zake kulingana na sheria ya chombo hicho. Badala yake katika zama hizi PCCB inatakiwa kufanya kazi kama idara ya serikali tu na kwa maelekezo ya wanasiasa. Nadhani hii ndiyo ilikuwa sababu ya kumwondoa yule mkurugenzi mbobezi wa sheria. Kuna vyombo pendwa vya serikali ambavyo rushwa ndani yake imeongezeka maradufu na PCCB ķamwe haiwezi kuwagusa bila kuelekezwa.
 
Kama Muslim haamua kumlinda huyu RTO naungana na Ben.. Trafiki Arusha ni tatizo kubwa. Na hii inachangiwa na wingi wao barabarani. Yaani kutoka kwa Morombo kwa mfano, hadi ufike posta mpya kuna vituo vya askari wa usalama barabarani zaidi ya saba. Unajiuliza hivi kuna umuhimu gani wa vituo vyote hivyo? Zaidi ya usumbufu.. Na kuongeza foleni. Kwa rushwa niseme kwa Tanzania nzima Trafic Arusha wanaongoza. Huwezi kusimamishwa hata kama huna kosa usiwaachie polisi chochote. Inahitajika mageuzi makubwa sana trafiki Arusha. Nazunguka maeneo mengi Tanzania lakini Arusha ni kiboko kwa rushwa na usumbufu usio na maana. rto asiseme kuna chuki.

Nakubaliana na wewe kabisa.
Pia ile kozi inayoendeshwa pale polisi mess, unalipa
1.10,000 kiingilio na kitabu na alama za barabarani
2.85,000 cheti
3. 3,500 kiti ulichokalia

Inasikitisha sana
 
Ukweli ni kwamba Jeshi la Polisi na TRA baeo ni vinara wa rushwa. Nitaamini kuwa PCCB inafanya kazi siku nitakapoona inashughulika na Polisi na TRA. Mpaka sasa sijaona jitihada zozote za PCCB dhidi ya taasisi hizi mbili vinara wa rushwa.


!
!
Uwepo Wa Rushwa Unaweka Uhalali Wa Kuwepo Wa PCCB. PCCB Haiwezi Kuichukua Rushwa. Wapo Kwa Ajili Ya Rushwa
 
Kama Muslim haamua kumlinda huyu RTO naungana na Ben.. Trafiki Arusha ni tatizo kubwa. Na hii inachangiwa na wingi wao barabarani. Yaani kutoka kwa Morombo kwa mfano, hadi ufike posta mpya kuna vituo vya askari wa usalama barabarani zaidi ya saba. Unajiuliza hivi kuna umuhimu gani wa vituo vyote hivyo? Zaidi ya usumbufu.. Na kuongeza foleni. Kwa rushwa niseme kwa Tanzania nzima Trafic Arusha wanaongoza. Huwezi kusimamishwa hata kama huna kosa usiwaachie polisi chochote. Inahitajika mageuzi makubwa sana trafiki Arusha. Nazunguka maeneo mengi Tanzania lakini Arusha ni kiboko kwa rushwa na usumbufu usio na maana. rto asiseme kuna chuki.
Naunga mkono hoja yako,kuna wale Matrafiki wanawake wazee Anna (matege)na Rehema,ukilogwa ukawapa leseni,hawakuachii bila Ten.Lazima wakulazimishie kosa
 
Yaani arusha ukifika nibora uache gari utembelee pikipiki,ni usumbufu kila hatua unasimamishwa!! Inaonesha mabosi was trafiki wanawatuma vijana pesa ndefu sana hiyo RTO apunguze hikitu. Tunajua matrafiki polis walivyojenga mijumba mikubwa isiyolingana na vipato vyao tens hawana hats biashara yakuzugia,sikuizi wanatembelea gari binafsi ili kujifichamo kwakweli toka waruhusiwe pesa ya kubrash viatu imekuwa ni shida saiv wanabrashi migorofa
 
Tangu awali matraffic wa Arusha ni walaku sana, huyu rto wasasa amewanyoosha matajiri wengi sijui kama watambakiza
Yaani arusha ukifika nibora uache gari utembelee pikipiki,ni usumbufu kila hatua unasimamishwa!! Inaonesha mabosi was trafiki wanawatuma vijana pesa ndefu sana hiyo RTO apunguze hikitu. Tunajua matrafiki polis walivyojenga mijumba mikubwa isiyolingana na vipato vyao tens hawana hats biashara yakuzugia,sikuizi wanatembelea gari binafsi ili kujifichamo kwakweli toka waruhusiwe pesa ya kubrash viatu imekuwa ni shida saiv wanabrashi migorofa
 
Rushwa ina njia mbili, aidha UNALAZIMISHWA utoe rushwa ili uachiwe kwa sababu unamakosa au unataka mambo yako yaende haraka au UMELAZIMISHWA utoe rushwa kwasababu umebabikiwa makosa au pia wanakukwamisha ili utoe rushwa.
Sasa wenye mabasi ya magari tuseme hawataki kutoa rushwa basi wahakikishe hawana makosa kwenye magari yao na Kama yanamakisa wkubali kutoa faini tu na sio zaidi. Na wenye mabasi wakizungushwa na kukwamishwa basi inabidi wafanye mgomo wa angalau siku mmoja tu. Na wenye mabasi wote waungane, ikitokea kwamba wamelazimishwa kutoa rushwa au wanazungushwa na kucheleweshwa hadi watoe rushwa basi hapo wafanye mawsiliano na wagome. Hilo suala nina uhakika litashughulikiwa mara mmoja. Na wakivabikiwa makosa wajitahidi kushibitisha kwamba hawana makosa, siku hizi kuna njia kibao ya kumnasa mtu. Si lazima umchukue video unaweza ukarekodi kwenye simu yako pia.
 
Back
Top Bottom