Mfahamu Salma Kikwete

Mfahamu Salma Kikwete

Hauna picha zake za ujanani? Wakati huo akikutana na mkulu.. Natamani sana kumuona.. Na je mbna haujawa specific sana kwenye hii hadithi yako? Na je huyo aliyekuwa mke mkubwa kwa sasa yupo wapi?
 
Na kwa nini hii taarifa inskuja leo, watu wa kusini kuweni macho...
 
phoca_thumb_l_salma-kikwete.jpg

Mama Salma Kikwete.

Salma Rashid (kikwete). alizaliwa katika wilaya ya Lindi Mjini, Novemba 30, 1963. Baba yake anaitwa Rashid Yussuf Mkwachu na mama yake ni Mwanapaza binti Shariff.

Kwa asili, baba yake anatoka Sarai, Rufiji mkoani Pwani na mama yake anatoka Lindi.

Katika familia , upande wa mama, walizaliwa watoto saba, wasichana watatu na wavulana wanne. Yeye akiwa ni wa sita, ila kwa baba ni wa pili, ana kaka yake na mdogo yake. Na pia ana wadogo zake wengine watatu ambao wanachangia baba, kati yao wavulana ni wawili na msichana mmoja.

Baba yake alikuwa mfanyakazi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyovunjika mwaka 1977 na kituo chake cha kazi kilikuwa Mtwara, wakati baba yake anafanya kazi, mama alibaki Lindi, hali ambayo ilimfanya apate elimu yake ya msingi kuanzia mwaka 1973 katika shule nne tofauti; Nnaida ya Mikindani, Mtwara, Rahaleo ya Lindi, Ligula (Mtwara) na Stadium, Lindi ndipo ambapo alimalizia elimu yake ya msingi.
Ingawa wakati ule nafasi za kujiunga na sekondari zilikuwa chache, ailikuwa miongoni mwa waliochaguliwa.

Kukutana na Kikwete.
Kila jambo hupangwa na Mwenyezi Mungu. alilikutana na atakayekuwa mume yake mwaka 1985 akiwa katika Chuo cha Ualimu Nachingwea, yeye akiwa ni Katibu wa CCM wa Wilaya ya Nachingwea.

Walipokutana kwa mara ya kwanza kitu ambacho alimwambia ni kwamba" nakupenda na nataka nikuoe" hakusema anataka awe rafiki yake au vipi, sijui kama huo ndio utaratibu wa kina baba wote, kwa sababu alimpenda, alimkubalia, ingawa uamuzi wake hakuutoa papo hapo.

Walifunga ndoa Machi 30, 1989 wakati huo yeye akiwa Naibu Waziri wa Maji, Nishati na Madini. Baada ya kufunga ndoa walifanya taratibu za uhamisho kwa mujibu wa taratibu za kikazi.

Kwa hiyo walihamia Dar es Salaam ambapo aliungana na mume wake na wakawa wanakaa Mikocheni mtaa wa Ursino.

Wamejaaliwa watoto watano kati yao wanne ni wa kiume na mmoja wa kike. Wote wanasoma, wa kwanza yuko kidato cha sita, wa pili cha nne, wa tatu cha pili, wa nne yuko darasa la tano na wa mwisho yuko darasa la tatu.

Lakini kwa ujumla wana watoto wanane, ikiwa ni pamoja na watatu ambao mume wake alipata na mke wake wa kwanza.

Hawa wakubwa mmoja ni mwanasheria, mwingine ni daktari na mwingine ni mtaalamu wa Teknohama (Teknolojia ya Habari na Mawasiliano).

Ila siku zote hupenda kusema wana watoto wanane kwa sababu hata wale wakubwa amewalea yeyetangu wakiwa na umri mdogo sana. Kwa hiyo wale ni watoto wake sawa sawa na aliowazaa yeye.

Ahsante kwa kusoma na kuelewa kwa makini.

Tupe na za mke mkubwa na yupo wapi sasa
 
Ungeeleza na jinsi alivyopata ziro form 4 na akibidi alisiti mara 3..
Unakumbuka pia walishawahi kuachana na mumewe mwaka 97 unajua kisa nini..
Na ungesema kuwa kwa jk kuwa ni ndoa yake ya 2 baada ya kuachwa na mumewe wa kwanza bwana mbaruku
 
phoca_thumb_l_salma-kikwete.jpg

Mama Salma Kikwete.

Salma Rashid (kikwete). alizaliwa katika wilaya ya Lindi Mjini, Novemba 30, 1963. Baba yake anaitwa Rashid Yussuf Mkwachu na mama yake ni Mwanapaza binti Shariff.

Kwa asili, baba yake anatoka Sarai, Rufiji mkoani Pwani na mama yake anatoka Lindi.

Katika familia , upande wa mama, walizaliwa watoto saba, wasichana watatu na wavulana wanne. Yeye akiwa ni wa sita, ila kwa baba ni wa pili, ana kaka yake na mdogo yake. Na pia ana wadogo zake wengine watatu ambao wanachangia baba, kati yao wavulana ni wawili na msichana mmoja.

Baba yake alikuwa mfanyakazi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyovunjika mwaka 1977 na kituo chake cha kazi kilikuwa Mtwara, wakati baba yake anafanya kazi, mama alibaki Lindi, hali ambayo ilimfanya apate elimu yake ya msingi kuanzia mwaka 1973 katika shule nne tofauti; Nnaida ya Mikindani, Mtwara, Rahaleo ya Lindi, Ligula (Mtwara) na Stadium, Lindi ndipo ambapo alimalizia elimu yake ya msingi.
Ingawa wakati ule nafasi za kujiunga na sekondari zilikuwa chache, ailikuwa miongoni mwa waliochaguliwa.

Kukutana na Kikwete.
Kila jambo hupangwa na Mwenyezi Mungu. alilikutana na atakayekuwa mume yake mwaka 1985 akiwa katika Chuo cha Ualimu Nachingwea, yeye akiwa ni Katibu wa CCM wa Wilaya ya Nachingwea.

Walipokutana kwa mara ya kwanza kitu ambacho alimwambia ni kwamba" nakupenda na nataka nikuoe" hakusema anataka awe rafiki yake au vipi, sijui kama huo ndio utaratibu wa kina baba wote, kwa sababu alimpenda, alimkubalia, ingawa uamuzi wake hakuutoa papo hapo.

Walifunga ndoa Machi 30, 1989 wakati huo yeye akiwa Naibu Waziri wa Maji, Nishati na Madini. Baada ya kufunga ndoa walifanya taratibu za uhamisho kwa mujibu wa taratibu za kikazi.

Kwa hiyo walihamia Dar es Salaam ambapo aliungana na mume wake na wakawa wanakaa Mikocheni mtaa wa Ursino.

Wamejaaliwa watoto watano kati yao wanne ni wa kiume na mmoja wa kike. Wote wanasoma, wa kwanza yuko kidato cha sita, wa pili cha nne, wa tatu cha pili, wa nne yuko darasa la tano na wa mwisho yuko darasa la tatu.

Lakini kwa ujumla wana watoto wanane, ikiwa ni pamoja na watatu ambao mume wake alipata na mke wake wa kwanza.

Hawa wakubwa mmoja ni mwanasheria, mwingine ni daktari na mwingine ni mtaalamu wa Teknohama (Teknolojia ya Habari na Mawasiliano).

Ila siku zote hupenda kusema wana watoto wanane kwa sababu hata wale wakubwa amewalea yeyetangu wakiwa na umri mdogo sana. Kwa hiyo wale ni watoto wake sawa sawa na aliowazaa yeye.

Ahsante kwa kusoma na kuelewa kwa makini.

Kwahuyu Sitii Neno Kwani Namheshimu Mno Na Sana ILA Haziband Wake Ndiyo Tatizo Langu.
 
Bongo hagiography tushazoea.

Tumedanganywa sana kwamba Nyerere ndiye Mtanganyika wa kwanza kusoma Uingereza mpaka watu wakakubali.

Tumedanganywa Nyerere ana degree ya pili (ana Masters ya graduate school) mpaka kajifia tumekubali.

Endeleeni kutoa historia nusunusu tu.

Ila Babu Seya alivyofanya vitu vyake msiache kusema.
 
Mama yetu nasikia alikua na kakijana serengeti boy alikua anamtolea vipele mgongoni,kalikua kanafanya kazi pale ccm lumumba sijuia katakuwa wapi kwa sasa na kaliwezeshwa usafir
 
Mkuu mleta uzi, kwenye aya ya nne umenichanganya kabisaaa....!!! Nanukuu:

"...Ingawa wakati ule nafasi za kujiunga na sekondari zilikuwa chache, ailikuwa miongoni mwa waliochaguliwa." mwisho wa kunukuu.

Naomba ufafanuzi wa maelezo hayo....je, huyo mama alisoma shule ipi ya sekondari kabla ya kujiunga na chuo cha ualimu Nachingwea !?
 
Nikimsikiliza huwa ninamwona mbumbumbu sana haikosi ni mwalimu wa UPE
 
Ungeeleza na jinsi alivyopata ziro form 4 na akibidi alisiti mara 3..
Unakumbuka pia walishawahi kuachana na mumewe mwaka 97 unajua kisa nini..
Na ungesema kuwa kwa jk kuwa ni ndoa yake ya 2 baada ya kuachwa na mumewe wa kwanza bwana mbaruku

He! Hii kama vile ni genuine
 
Back
Top Bottom