Mfahamu Robert Ames. Afisa wa CIA aliyewakutanisha Yitzhak rabin P.M wa Israeli na Yasser Arafat wa palestina

Mfahamu Robert Ames. Afisa wa CIA aliyewakutanisha Yitzhak rabin P.M wa Israeli na Yasser Arafat wa palestina

mcTobby

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2018
Posts
6,499
Reaction score
18,166
Ilikuwa ni siku ya jumatatu ya mwezi wa 9 mwaka 1983. Siku ambayo anga lilikuwa angavu na bluu ikimaanisha hali ya joto kiasi ndani ya makao makuu ya nchi ya marekani Washington d.c. Hakika siku na tarehe hii ilikuwa ikisubiriwa kwa hamu kubwa na watu wengi na sio tu wamarekani bali karibia kila kona ya dunia. Watu waliamini kabisa historia mpya inaenda kuandikwa upya haswa kutokana na migogoro ya muda mrefu ikiwemo vita ,ugaidi pamoja na mauaji ya koholela pale mashariki ya kati . Na hususani mgogoro wa muda mrefu baina ya Israeli na Waarabu/wapalestina huenda ulikuwa unaandika historia mpya kabisa ya mapatano ya amani.
Sasa siku hii hapo Washington d.c kulikuwa bize sana maafisa wa ngazi za juu, waandishi wa habari na wageni maalumu walikuwa wakisubiri kutiliwa saini makubaliano ya kumaliza mgogoro kati ya Israeli na palestina.

Haya yakiendelea huko Washington d.c, siku hii pale kwenye viunga vya makao makuu ya CIA Langley Virginia yupo mmoja wa afisa wa ngazi za juu wa Shirika hilo aliwahi kufika ofisini siku hiyo kuliko kawaida akiwa ana mchanganyiko wa upweke,hasira na hali ya kuboeka. Afisa huyu hakuwa mwingine bali ni Frank Anderson mwenye umri wa miaka 51. Huyu afisa wa CIA alikuwa mkuu wa kitengo cha Clandestine operations( operesheni za siri za kijasusi)kwenye eneo la nchi za kiarabu na alikuwa na sababu ya kutabasmu kutokana na kufanikisha zoezi hili lililoratibiwa kule Washington d.c la kutia saini makubaliano ya kusitisha vita baina ya Israeli na Waarabu, lakini alikuwa hana furaha hata kidogo.

Siku hii ni kwamba rais Bill Clinton alikuwa amewaalika wageni zaidi ya 2000 kwenye ikulu ya whitehouse kwa ajili ya kushuhudia Yitzhak Rabin waziri mkuu wa Israeli na kiongozi wa kundi la kipalestina la PLO bwana Yasser Arafat wakitia saini mkataba wa amani.
file-20230907-29-w0u6nx.jpg


Sababu hii iliyomfanya huyu Anderson kutokuwa na furaha siku hii ni kutokana na ukweli kwamba kati ya wageni hawa waalikiwa, Hakuna afisa wa CIA aliyealikwa katika hafla hii. Anderson aliamini mpango huu wa makubaliano ya amani ilikuwa ni operesheni ya kijasusi ya CIA iliyoanzishwa takribani miaka kumi iliyopita pale mashariki ya kati. Anderson aliamini whitehouse haikufanya fair katika kutotambua mchango wa CIA katika mafanikio haya.

Yaani mpaka ifikie hatua ya kusaini makubaliano ya amani kati ya Israeli na palestina halikuwa zoezi jepesi hata kidogo. Katika mchakato huu wa amani hadi kufikia hapo uliratibiwa kwa kiasi kikubwa na afisa wa CIA aliyejulikana kama Robert clayton Ames miaka ya nyuma hadi mauti ilipomkuta akiwa kazini huko Beirut Lebanon tarehe 18 April mwaka 1983.

Kivipi?
Tukirudi nyuma hadi hivi mwaka 1983.kulitokea shambulizi la kigaidi ndani ya mji wa Beirut Lebanon kwenye ubalozi wa marekani ambapo gari aina ya pickup iliyokuwa imebeba bomu kuendeshwa hadi kwenye viunga vya jengo la ubalozi wa marekani hapo Beirut na baada ya muda mfupi kulipuka. Ames siku hii alikuwa mmoja wa wahanga wa huu mkasa . Tunaweza kusema alikuwa wrong place at a wrong time. Tukio hili la kigaidi liliua wamarekani 16 ambapo saba kati yao walikuwa maafisa wa CIA(Ames akiwa mmojawapo). Pia liliua zaidi watu wengine 46 wakiwa raia wa Lebanon. Shambulizi hili lilikuwa la mara ya kwanza kwa Shirika la CIA kupoteza staff wake wengi kwa wakati mmoja ( maafisa 7).
aerial-view-of-the-united-states-embassy-in-beirut-18-april-1983-after-a-bomb-destroyed-part-of.jpg


Sasa basi siku hii bwana Anderson baada ya kufika makao makuu ya CIA saa tatu kamili asubuhi , moja kwa moja alihudhuria kikao cha wakubwa wake kwa ajili ya kupeana daily briefings za siku husika. Siku hii ilipangwa kwamba baadhi ya maafisa wangetembelea makaburi ya walipozikwa maafisa wa CIA waliokufa katika ubalozi wa marekani huko Beirut ikiwemo kaburi la Ames ambaye alikuwa kama shujaa aliyefanikisha mchakato huu wa amani.
Na kweli saa nne na nusu asubuhi kwenye geti mojawapo la kuingilia makao makuu, basi lilikuwa tayari limepaki kwa ajili ya kuwabeba maafisa wa CIA na baadhi ya staff karibia arobaini wa hapo makuu kwa ajili ya kuelekea kwenye makaburi ya Arlington kutoa heshima zao ya kuwaenzi mashujaa hao ingawaje wao waliona white house haikuwatendea haki katika kuwaenzi maafisa hao wa CIA waliofanikisha mchakato wa amani hususani kwa bwana Ames.
Arlington_National_Cemetery_Seal.png

Na kweli msafara huu ulipofika kwenye makaburi ya Arlington yaliyopo karibu na Potomac river , majira ya 5 na dakika 43 asubuhi walitazama ng'ambo ya mto huu kwa umbali kiasi ilipo ikulu ya whitehouse . Waliamini Hafla iliyokuwa ikiendelea huko ilifanikishwa kwa kiasi pakubwa na mashujaa kadhaa ndani ya CIA wakiwemo miongoni mwa waliozikwa kwenye makaburi ya mashujaa ya Arlington. Na ni muda huo ndani ya white house zoezi la makubaliano ya kusitisha vita na kutiliana saini za kusitisha mapigano yaliyodumu kwa muda mrefu lilikuwa likiendelea.
Maafisa hawa wa CIA walitoa heshima zao akiambatana na sala ya kimya kimya kwa hawa mashujaa waliozikwa kwenye makaburi hayo. Walianza na kaburi la Robert Ames lililokuwa limeandikwa maneno haya;
" Robert Clayton Ames, Central Intelligence Agency of the United States of America, March 6, 1934–April 18, 1983" na kuliwekea maua juu yake. Frank Anderson alitoa hotuba fupi kuhusiana na huyu ames jinsi alivyoweza kujenga uhusiano na Ali Hassan salameh kiongozi wa kundi la wanamgambo wa PLO na pia mkuu wa kitengo cha ujasusi cha kiongozi wa palestina Yasser Arafat. Uhusiano uliopelekea viongozi hasimu yaani yithzak Rabin na Yasser Arafat kuamua kusaini mkataba wa amani ili kumaliza mgogoro baina yao na pia kuundwa kwa serikali ya palestina inayojitawala.
Pia walitembelea na kuweka shada la mauahadi kwenye kaburi la Afisa mwingine wa CIA aliyeitwa William Buckley ambaye alikuwa CIA station chief huyu aliuawa mwaka1984 baada ya kuteswa na magaidi akiwa hapo mashariki ya kati.
Waliozikwa hapo Arlington national cemetery ambapo hawa maafisa wa CIA wakiongozwa na Frank Anderson waliweza kuwakumbuka na kuwawekea mashada ya maua ni pamoja na James na monique Lewis ambao pia walikufa pamoja na Ames kwenye mkasa wa kulipuka kwa bomu kwenye ubalozi huo wa Marekani hapo Beirut . Hawa wote walikuwa waajiriwa wa CIA.
Na mwisho walizuru kaburi la Kenneth Haas ambaye naye alikuwa CIA station chief wakati mkasa huu unatokea na mwishowe kabisa walimaliza kuweka shada la maua kwenye kaburi la Frank Johnston anbaye naye alikuwa mwajiriwa wa CIA. Ilikuwa ni siku ya huzuni sana kwa hawa maofisa wakiongozwa na Frank Anderson. Hii ilikuwa ni idadi kubwa kabisa kwa Shirika la CIA kupoteza maofisa wake kwa wakati mmoja. Lakini hii yote ni gharama ambapo marekani waliilipa kutokana na kutaka kusuluhisha vita kati Israeli na palestina . Marekani aliamini sasa Mwisraeli na mpalestina wataishi kama ndugu.. lakini haikuwa hivyo mpaka sasa mgogoro haukuwahi kuisha. Na la zaidi ni kwamba hata Waisraeli wenyewe hawakukubaliana na hili swala la kupatana na mahasimu wao.. Lakini huyu Robert Ames ni nani na mchango wake ulikuwaje katika haya yote mpaka kuwa na urafiki na kiongozi wa ugaidi Ali Hassan salameh a.k.a the red prince?
 
SEHEMU YA KWANZA

Robert Ames alikuwa ni jamaa flani poa sana. Na zaidi alikuwa anakubalika kuanzia ofisini hadi ground na maafisa wenzake wa CIA.
Huyu mdau alizaliwa march 6 mwaka 1934 kwenye mji wa philadelphia na alikulia kitongoji cha washua wa Roxborough ulioko kaskazini mwa mji huu kwenye mtaa wa 4624 pechin street kwenye nyumba ya ghorofa 2. Baba yake Ames aliitwa Albert clayton Ames na alikuwa ni mfanyakazi (inspector)wa kiwanda cha chuma cha kutengeneza ballbearing(beringi) kilichoitwa SKF ball bearing plant kilichokuwa kinamilikiwa na waswedish. Ingawaje baba yake Ames alikuwa akipokea mshahara mdogo kwenye hiki kiwanda, lakini atleast waliweza kuishi maisha standard ya kati(kishua).

Mama yake Ames aliitwa Helen frances Amorose mkatoliki mwenye asili ya italia ambaye alikuwa ni mama wa nyumbani. Huyu ames alikuwa ni mtoto wa pili kati ya watoto watatu katika familia hiyo. Na alikuwa wa kiume peke yake. Dada yake mkubwa aliitwa Patricia na dada yake mdogo aliitwa Nancy. Ames pamoja na dada zake walisoma shule ambayo haiko mbali sana na mtaa wao iliyojulikana roxborough high school. Huyu bwana Ames licha ya kuwa ni mtu muongeaji na alikuwa anakubalika sana na mademu japo hakuwahi ku date shuleni. Jamaa alikuwa ni mpenzi wa michezo basketball na alijikuta amepata scholarship ya kuendeleza masomo na kipaji chake kwenye chuo cha kikatoliki cha La salle college.
Hata kwenye masomo alikuwa akifanya vizuri hususani kwenye masomo ya sociology na psychology. Pia alikuwa akijifunza lugha ya kispaniola pamoja na kifaransa. Na alikuwa anaamini siku moja atakuja kufanya kazi kama afisa wa FBI. Hivyo aliamua kuchukua kozi ya sheria maana kwa kipindi hicho fbi walikuwa wanaajiri maafisa wengi waliosomea sheria..

Baada ya kuhitimu kwenye chuo cha
La Salle Catholic college mwaka 1956 alihamia kwenye mji wa Orange huko Texas kwenda kufanya kazi kwenye kampuni ya ujenzi iliyoitwa Catalyic Construction company akisubiri kuitwa kwenye military service. Kikwetu huku tunaita JKT.
Na kweli ilipofika mwezi wa 8 mwaka 1956 aliitwa jeshini na kupata mafunzo ya awali (basic training) kwa muda wa wiki 13. Baada ya kufuzu mafunzo ya awali alisainiwa na kuingizwa kwenye jeshi na kusajiliwa kwenye kitengo cha U.s Middle East Signal communication Agency. Kamandi hii ya kijeshi ilikuwa ikihusika haswa na maswala ya mawasiliano kwenye eneo la mashariki ya kati. Na alipostiwa hadi afrika akiwa na kamandi hii mwaka 1957 akiwa kama mtaalamu wa vifaa vya mawasiliano yaani signal-supply specialist kwenye kituo kilichopo Eritrea kijulikanacho kama Kagnew station kilichokuwa nje kidogo ya jiji la Asmara.

Kituo hiki cha jeshi la marekani kilikuwa kinahusika na maswala mazima ya mawasiliano ya kijeshi . Kituo hiki cha Kagnew kilikuwa chini ya kamandi ya usalama ya jeshi la marekani iliyojulikana kama Fourth U.S. Arm security Agency. Na huyu ames alikuwa mwanachama wa kitengo cha kijeshi cha 9434 Signal corps
Kituo cha Kagnew kinapatikana eneo la jangwani karibu na ikweta na kilikuwa kimejengwa mahsusi kwenye eneo la mwinuko la futi 7,300 kutoka usawa wa bahari. mpaka kijengwe kwenye mwinuko huu ilikuwa ni kwa sababu ya mitambo ya mawasiliano iliyojengwa enzi zile za vita baridi kwa ajili ya kusikiliza mawasiliano ya baadhi ya nchi hususani za kiafrika na mashariki ya kati.
Kituo hiki cha kagnew kilikuwa na kambi ya kijeshi iliyokuwa ina uwezo wa kubeba wanajeshi wa Marekani zaidi ya 1000 na wafanyakazi hususani technicians kutoka kwenye idara za kiusalama kama National security Agency (NSA) pamoja na CIA.
Eneo hili la Kagnew lilikuwa limesimikwa mitambo maalumu ya kimawasiliano kwenye eneo la ekari 2,500 kwa ajili ya kuingilia na kusikiliza (intercept) mawasiliano yote ya kijeshi na kidiplomasia kwenye nchi za afrika pamoja na mashariki ya kati. Eneo hili wamarekani walilipa jina Island in the sky kwa sababu kilikuwa kituo kilichojengwa eneo la mwinuko.
Kipindi kituo hiki cha kijeshi cha Kagnew kinajengwa eneo hilo la Eritrea ilikuwa lengo kuu ni kwa ajili ya kuingilia(intercept) mawasiliano ya kijeshi na ya kidiplomasia kwenye serikali ya nchi ya misri na baadhi ya nchi za kiarabu. Hivyo basi wote waliokuwa kwenye kambi hii ya kagnew walikuwa wanafanya kazi chini ya idara ya usalama wa taifa la marekani yaani NSA kwa ajili ya ku break codes za kimawasiliano ya siri kwenye hizo nchi husika kisha zinatafsiriwa na wataalamu kutoka lugha ya Kiarabu hadi kiingereza na kurekodiwa kwenye tape recorder. Hii ndio ilikuwa kwa mara ya kwanza Bob ames kama utani amejiingiza kwenye dunia ya unjagu na maswala ya kijasusi.
Bob ames pamoja na rafiki yake kwenye kambi hii aliyeitwa John Wilson kutoka oklahoma ,kazi yao kubwa haswa ilikuwa ni kusambaza vifaa vya spea mbalimbali za mitambo ya transmitters na receiver kupitia kampuni iliyopewa jukumu kufanya kazi hiyo kwenye kambi hii ya kagnew.

Katika eneo hili la Kagnew , waliajiriwa house boys kutoka hapo Eritrea kwa ajili ya kufanya usafi kwa baadhi ya nyumba au quarters walizokuwa wakiishi wanajeshi wa kimarekani ikiwemo bob ames. Katika kambi hii ilikuwa ni full package kwa maana ya kwamba ilikuwa na kanisa dogo,bar, duka la kuuza snacks, sehemu ya kuangalia movie n.k kwa ajili ya wafanyakazi wa kijeshi eneo hilo.
Katika kambi hii ya kagnew pia wanajeshi walikuwa wanapata nafasi ya kutalii maeneo kadhaa wakiwa wapo off duty. Kwa mfano ames pamoja na wenzake walipata nafasi ya kutembelea maeneo kadhaa kama mji wa Jerusalem pamoja na cairo. Katika harakati za kutalii maeneo haya huyu bwana Ames alianza kujifunza kuongea kiarabu, moja kati ya lugha ngumu kabisa kujifunza kwa mtu anayeongea kingereza hususani wazungu.

Na kweli baada ya kukaa ndani ya kagnew station mwaka mmoja na mwezi mmoja hivi, Ames alirudi marekani baada ya kukamilisha assignment akiwa na kikosi cha 9434 signal corps. Kiufupi huyu Ames hakuonyesha interest sana na maswala ya kijeshi. Hivyo ilipofika mwezi novemba 7,1958 aliondoka jeshini rasmi(Military discharge) na kutunikiwa medali ya heshima ya honorable discharge and Good conduct .
Sasa kwa huyu Ames , kufanya kazi jeshini na kusafiri nje ya marekani kulimpa exposure ya dunia jinsi ilivyo, hivyo ule ushamba ukawa umemtoka . Na akaona ni wakati sahihi pengine kwa yeye kutafuta kazi mpya ndani ya state department of U. S.A( huku kibongobongo tunaweza sema ni wizara ya mambo ya nje na maswala ya kimataifa)kutokana na exposure aliyokuwa nayo.

Sasa Bob ames baada ya kurudi kwenye mji wa nyumbani kwao wa philadelphia, alipata kazi kwenye kampuni ya bima iliyojulikana kama Allstate insurance company. Na alichukua uamuzi wa kusoma ile wanaita night study kwa ajili ya kufanya mtihani wa State department foreign Service written exam. Ikitokea umefaulu mtihani huu basi unakidhi vigezo vya kufanya kazi nje ya nchi ya marekani hususani kama mwakilishi ubalozini au kwenye taasisi za umoja wa mataifa zilizo chini ya marekani. Huyu ames hata kazi aliyokuwa akiifanya kwenye kampuni hii ya bima hakuipenda kutokana na kukaa muda mrefu sehemu moja tu wakati wote. Ames Alitamani kutembea duniani. Lakini katika ofisi hii alipatana na mrembo aliyekuwa secretary wa kampuni aliyeitwa Yvonne Blakely ambaye wazazi wake walikuwa na asili ya nchi za Scotland na Ireland na kuanza kujitetea(kutongoza).
Screenshot_20250803_080859_ReadEra.jpg
Na kweli walioana tarehe 30 mwezi wa nne 1960 ndoa yao ikifungwa kanisa la Lutheran.. ofcourse huyu Ames alikuwa mkatoliki na mkewe alikuwa mlutheri kwa hiyo kwa kuwa alikuwa ashapenda aliamua kujiunga na dhehebu la mkewe. Chezea nguvu ya mapenzi wewe.
Baada ya kuoana tu punde Ames alifanya mtihani foreign Service written exam lakini alifeli vibaya mno. Hakukata tamaa. Aliamua ku apply kazi kwenye shirika la kijasusi la CIA, na ilipofikia mwezi juni mwishoni mwaka 1960 aliitwa kufanya usahili na kusafiri hadi New York city akiwa na mpenzi wake huyu mpya Yvonne. ALIFAULU USAHILI.
 
SEHEMU YA 2
Na kweli Mungu hatumpi mja wake mwishoni mwa mwaka 1960 Bob au Robert Ames aliajiriwa na CIA huku akiwa na uhakika wa kupokea dollar 5,000 kwa mwaka. Kwa mtu kijana kama yeye hii ilikuwa ni pesa ndefu sana. Ames na mkewe Yvonne baada ya sikukuu ya krismasi kupita walihamia Washington d.c na kukodi apartment ndogo waliokuwa wakilipa kodi ya dola 150 kwa mwezi iliyokuwa eneo la1400 South Twenty-eighth Street in Arlington, Virginia. Robert Ames na mkewe walikuwa wanamiliki gari ndogo aina ya fiat.
Kikawaida watu wanaoajiriwa kwenye mashirika ya ujasusi kama CIA huwa wanaambiwa kabisa wasiseme kazi zao au wanamfanyia nani kazi. Hata ikibidi asimweleze mtu wa karibu kama mkewe. Lakini maafisa wengi wa CIA huwa wanaawaambia wake zao. Hivyo hata kwa Ames, Yvonne mkewe alikua anajua mmewe ni mtu wa kitengo. Pia baadhi ya ndugu wa Ames walijua ndugu yao ni mtu wa kitengo sio kwa kuambiwa bali walipata picha huenda ndugu yao ni afisa wa CIA kutokana na kuhamia Washington d.c haswa kwenye mtaa wa Arlington Virginia.
Maisha ya Washington d.c yalikuwa ni ya uchangamfu sana kwa hii couples hususani ni mwaka ambao John f. Kennedy alikuwa anatarajiwa kuapishwa kuwa rais Januari 1961 hivyo kulikuwa na amsha amsha na harakati za hapa na pale.

Mwaka huo huo Robert Ames alijiunga na shirika la CIA kama junior officer trainee (JOT)na alipaswa kufanya kozi maalum kwa junior officers wanaojiunga iliyojulikana kama Operation course-11.
Hiyo namba 11 ilimaanisha shirika la CIA lilikuwa na miaka 11 ya kutoa course hizi za junior officers tokea kuanzishwa kwake 1947 na ni course ya 11 kufanywa na JOT iliyokuwa inachukua mwaka karibia mmoja kuikamilisha.
Sasa katika course hii ilikuwa na Junior officers 45 ambao wengi ni wanaume ikiwemo Ames pamoja na mwanamke mmoja. Katika mafunzo ya kozi hii ilikuwa ukimaliza unafanya kazi kwenye kitengo cha mipango na mikakati ndani ya CIA yaani directorate of Plans(DP), ambapo ilikuja kubadilishwa na kuitwa directorate of Operations na sasa inajulikana kama National Clandestine Services yaani idara ya CIA inayohusika na operesheni za siri za kijasusi kwa kukusanya taarifa za kijasusi kwa njia ya siri. Na endapo junior officer akikamilisha mafunzo yanayochukua karibu miaka miwili wangepanda ngazi na kuwa case officers na kutumwa kufanya kazi nje ya marekani hususani kwenye balozi zake wakiwa na diplomatic cover. Diplomatic cover ina maanisha hivi marekani inaweza ikamleta mwakilishi au balozi wake let's say Hapa Tz ambaye ni mwanadiplomasia lakini kiundani ni CIA agent akiwa na cover ya balozi au mwakilishi. Na ikitokea serikali ya nchi husika imemgundua kuwa ni jasusi wa CIA hawezi kufunguliwa mashtaka ya makosa ya kijasusi ila atafukuzwa tu ndani ya masaa 24 au 48 awe ameondoka nchi hiyo kwa kuwa hatakiwi. Kwa lugha ya kilatini wanasema Persona non Grata.

Sasa kwa hawa JOT ikiwemo ames walikuwa wakifundishwa mafunzo maalum ya ujasusi (tradecrafts) hususani namna ya kutafuta maagent na kuwaajiri kwenye nchi husika wanazokwenda kukusanya taarifa za kijasusi ambao watawatumia na kuwasimamia.
Na kweli ilipofika mwishoni mwa 1961 tokea Kennedy aingie madarakani shirika la CIA lilikuwa na maafisa wapya zaidi ya 16,000 . Na ilikuwa ni kipindi ambacho shirika la CIA lilikuwa likijiandaa kuhamishia makao makuu yake yaliyokuwepo Ohio drive karibu na mto Potomac hapo Washington d.c hadi Langley, Virginia. Ni kipindi hiki ambapo shirika lilikuwa likiongozwa na mkurugenzi wake mkuu jamaa lenye misimamo yake Allen Dulles ambaye pia alikuwa ni mshauri wa maswala ya kijasusi wa rais wa marekani.

Sasa wakiwa katika mafunzo haya ya junior officers trainees(JOT) kama kawaida Ames alikuwa ameshapata marafiki wapywa kwa kuwa alikuwa ni mtu mcheshi sana ambao tunaweza kusema ni wale watu ambao ni Extroverts. Katika mafunzo haya maafisa hawa walikuwa wanatenganishwa wale waliooa na mabachela . Lengo la kufanya hivi ilikuwa kwa ajili ya kuchuja na kupata wale ambao ni the best wanaoweza kufanya vizuri wakiwa field . Kuna msemo walikuwa wanaambiwa na wakufunzi wao kwamba "Mixed drinks were very much still in vogue, and beer and wine might accompany a meal, but they never preceded it.🤣🤣” Kutokana na jinsi walivyokuwa wakitenganishwa wakati wa mafunzo.


Na hatimaye mwishoni mwa mwezi march 1961 Ames akiwa na wenzake walipelekwa sehemu inayojulikana kama "Farm" eneo la shamva lililokuwa linamilikiwa na CIA ambalo lilikuwa ni kambi ya mafunzo iliyojulikana kama Camp Peary iliyokuwa karibu na mto York uliopakana mji mdogo wa williamsburg huko Virginia . Kwenye mageti ya kuingilia kambi hii ya Peary kulikuwa na walinzi waliovalia sare za kijeshi ili ionenakane kama ni kambi ya kijeshi kwa wapita njia lakini hiyo ilikuwa ni kama cover. Kiuhalisia ilikuwa ni kambi ya mafunzo kwa maafisa wa CIA yaani CIA training facility.
Awali eneo hilo ilikuwa ni kambi ya mazoezi ya kijeshi yaani "Armed Force Experimental training Activity" na waliopata mafunzo hapo walikuwa wanapaita jina la utani 'Farm' Yaani shambani🤣.

Eneo hili la camp Peary lilikuwa linatoa mafunzo kadhaa ikiwemo combat skills,kutumia silaha na pia kutegua mabomu. Kwa mfano Ames ma wenzake walikuwa wanapewa mafunzo ya paramilitary trainings, namna ya kutumia silaha mbalimbali kama pistol, A-K 47 na pia M-16. Pia walikuwa wanajifunza kulenga shabaha kupitia silaha hizi kwenye target zinazotembea na pia wakiwa kwenye gari. Pia walikuwa wanafundishwa mazoezi ya kikomando kama vile kupanda kwenye kamba,kuruka vizuizi vya seng'enge na pia kutambaa kwenye mitaro au trenches, kusoma ramani na pia kutengeneza vilipuzi kwa kutumia mbolea( yeah mbolea inaweza kutumika kutengeneza vilipuzi .refer beirut explosion)n.k.

Ni Kipindi hiki ambacho ames na wenzake wakiwa eneo hili la Farm kulikuwa na uvamizi wa Bay of pigs huko cuba na ikatokea kwamba uvamizi ulioratibiwa na CIA kumpindua fidel castro kufeli.
Na wiki tatu baada ya uvamizi huu baadaye Ames alipata ruhusa ya kutoka kwenye kambi hii ya mafunzo kwenda kwa mkewe Yvonne kumjulia hali kwa kuwa alikuwa akikaribia kujifungua . Na kweli tarehe 11 mei 1961 mkewe alijifungua mtoto wa kike waliempa jina la Catherine.
Baada ya hapo siku chache baadaye Ames alirudi tena kuripoti kwenye kambi ya Farm kwa ajili ya kuendelea na mafunzo. Na aliporudi sasa waliingia kwenye aina nyingine ya mafunzo ambayo ndio yaliyokuwa lengo kuu la kupelekwa hapo Camp Peary au Farm. yalikuwa ni mafunzo ya Namna ya kuajiri na kuwatumia mawakala wa nchi husika ili kupata taarifa za siri za kijasusi kutoka nchi hiyo. Nikupe mfano kidogo. Yaani mtu tuseme raia wa kigeni anaweza akaja sehemu kama tanzania au kenya akatafuta mtu au wakala ambaye anaweza kumtumia kupata taarifa za kijasusi kutoka kwenye nchi hiyo. Na huyu mtu mgeni anaweza kumuajiri mtu akawa wakala wa ujasusi kutoka kitengo au taasisi yoyote ile ndani ya serikali. Wakala huyu anaweza akawa ni mfanyakazi wa wa kawaida kama cashier wa benki au hata mlinzi wa rais au hata mtoto wa rais au hata Rais mwenyewe. Huo ni mfano tu.
Sasa kwenye kambi hii ya Peary Ames na maafisa wenzake walikuwa wanafundishwa namna ya kuajiri mawakala wa aina hiyo. Na kumbuka kumuajiri mtu wa nchi husika umtumie kama chanzo cha taarifa za kijasusi sio kazi nyepesi hata kidogo. Na one mistake unaweza ukapotea au kumpoteza huyo wakala na ikazusha mgogoro baina ya nchi na nchi endapo mpango uki backfire.

Sasa katika mafunzo haya kila Junior officers alipewa kitabu ambacho kinaelezea nchi ya kusadikika ambayo haipo popote yaani fictional. Sasa kitabu hiki kilikuwa kinaelezea historia ya nchi ,geografia,pesa wanayotumia lugha, tamaduni pamoja na viongozi wake wakuu na wa taasisi pamoja na viongozi ambao ni wapinzani n.k. yaani kila kitu kuihusu hiyo nchi ya kufikirika kiliandikwa kwenye hicho kitabu ambapo afisa wa CIA anaweza kukutana nayo kwenye nchi halisi. Sasa wakaambiwa wa memorize key points kwenye kitabu hicho.
Sasa hawa junior officers walitengwa kwenye vikundi vya watu wa tano au sita na kila kikundi kikiwa na msimamizi au mentor ambao walikuwa ni staff wa hapo kambini. Na hapo hawa staff wangejifanya kama CIA station chief(yaani msimamizi mkuu wa operesheni za CIA kwenye nchi husika)aliyeko nchi ya kigeni na hao maafisa junior trainees wangejifanya ni Case officers au spy handler ambao ndio wanaoingia field kutafuta mawakala na kuwaajiri kisha kuripoti kwa station chief .
Sasa hapa kila walichokisoma kwenye kitabu hicho cha fictional walipaswa kukiripoti kulingana na assignment waliyopewa. kumbuka hapa kila kikundi kilipewa assignment yake mfano unakuta kundi moja limepewa assignment ya kuwatambua viongozi wa kisiasa wote wa hiyo nchi ,tabia zao n.k kisha kuripoti kwa station chief. Na kuripoti hizi taarifa sio kwamba anaenda kichwa kichwa .Lazima wapange sehemu ya kukutania kati ya case officer na station chief pasipo kugundulika na mwenzako. Haya maeneo ya kukutania yalikuwa ni lazima yawe ya siri na assignment ilikuwa inafanyika hata nje ya kambi hii ya Camp Peary. Hapa kwenye hatua hii walikuwa wanafundishwa kitu kwenye ujasusi kinaitwa "dry-cleaning" yaani namna ya kukwepa kufuatiliwa yaani kukwepa surveillance. Na vilevile hapa walikuwa wanafundishwa kitu kinaitwa "Dead drops" yaani namna ya kuacha alama ya kutoa signal kati ya wakala wa ujasusi na case officers sehemu ya kukutania au kumpa ujumbe pasipo kujulikana. Mfano dead drops inaweza kuwa ni shimo kwenye mti ambalo limefichwa ujumbe kama barua au pesa. Au inawezekana ni dirisha la choo cha umma au hata msumari uliokunjwa kwenye jumba bovu n.k.
Hatua hii ya namna ya kuwaajiri mawakala, hawa junior officers walikuwa wanafundishwa kutengeneza mahusiano ya kiurafiki kati ya case officer na wakala wa kijasusi wa hiyo nchi husika ambayo hayawezi kuzusha hali ya wasiwasi.

Ngoja nikupe mfano kisa kimoja wa mahusiano ya aina hii kati ya case officer/Spy handler na wakala wa ujasusi yanavyotengenezwa.

Huko Russia wakati wa vita baridi miaka ile iliwahi mtuma jasusi wa KGB hadi ufaransa miaka ya 1960 kwa ajili ya kukusanya taarifa za siri aliyeitwa Vladimir Vetrov. Huyu bwana akiwa ufaransa tayari naye alikuwa ameshawekwa kwenye rada za shirika la kijasusi la Ufaransa na ikajulikana ni jasusi wa KGB. Sasa baadaye baada ya kumsoma na kufuatilia nyendo zake pamoja na tabia zake waliamua kumuajiri yeye awe sasa anawapa wafaransa siri za urusi. Namna ya walivyomuajiri hawakumfuata direct eti tunataka kukuajiri utuuzie siri za urusi No. Walianza mahusiano naye taratibu kama mtu anayemenya kitunguu.
Sasa Siku moja huyu afisa akiwa barabarani anaendesha gari lake alitokea mtu mwingine aliyekuwa akiendesha gari kugonga gari ya huyu afisa . Katika harakati za kuomba msamaha huyu mtu ambaye ni mfaransa alimwambia huyu afisa wa KGB kwamba angegharamia kutengeneza gari ya huyu afisa na hapo ndipo mahusiano yao yalianza ya kirafiki na kumbe huyu mfaransa alikuwa ni afisa wa shirika la kijasusi la Ufaransa na alitumwa kama case officer/spy handler ili kutengeneza mahusiano na huyu afisa wa kgb.. Na kweli huyu Vladimir Vetrov baadaye aliajiriwa na ufaransa kama wakala au double agent akiuza siri za urusi kwa wafaransa hadi aliposhtukiwa miaka ya mwanzoni 80s na kuhukumiwa kifo (ofcourse kisa hiki niliwahi kukielezea humu).




Sasa tuendelee....


Maafisa hawa kwenye hii Camp Peary walikuwa pia wanafundishwa namna ya kuandaa aina ya malipo watakayopewa au kulipwa hawa mawakala wanaoajiriwa (double agents) yeah kila kazi ina mshahara. Hata mshahara wa dhambi ni mauti.....Malipo haya yanaweza kuanzia mamia ya dollars au hata "six figure" kulingana na aina na hadhi ya huyo wakala. Na pia account ya kupokea fedha hizo lazima ifunguliwe kwenye benki mojawapo ndani ya marekani. Pia walifundishwa wakala huyo lazima apewe life insurance. Yaani hakikisho la usalama wa maisha yake lazima liwe kipaumbele kupindi chote akiuza taarifa nyeti. Pia hawa maafisa walifundishwa kwamba hawa mawakala watakaoenda kuwaajiri lazima wasaini fomu maalumu inayohusiana na maswala ya makato ya kodi inayosema hivi nanukuu:
" certification … stating briefly that U/1 [jina la uficho la siri la huyu wakala au double agent] understands that no federal or state or social security taxes would be withheld from his RTACTION [jina la siri la mwajiri ambaye ni CIA] compensation during this period of employment.”
Kopi ya hii fomu ilikuwa inasainiwa na kuhifadhiwa huko Langley ambapo kopi hii ingekuja kutumika kama Reference baadaye ambapo kama kungezuka maswali kuhusiana na maswala ya ukwepaji kodi au utakatishaji fedha n.k. Ikumbukwe pia CIA bajeti yake lazima ijulikane pamoja na matumizi yake bungeni .

Hii pia ilikuwa inamaanisha hata kama hawa mawakala wanaoajiriwa kama majasusi kwenye hizo nchi ni raia wa marekani lazima pia wangelipa kodi kwa kile watakachokipokea kama malipo ya kazi zao.

Pia hawa junior officers walikuwa wanafundishwa kuandika ripoti ya kina kila watakapokutana na hao mawakala walioajiriwa huko field katika ukusanyaji wa Taarifa za siri. Ripoti hii lazima iwe na vipengele kama mkutano umefanyika wapi,mazungumzo yalikuwaje,lini na ni taarifa gani za kijasusi huyu mtu ambaye ni wakala alitoa na kumpatia case officer/spy handler.
Na la zaidi walifundishwa namna ya utambulisho wa awali (introduction) . Hawa junior officers walifundishwa namna ya kutambulika kwa majina ya bandia (alias)na huyo wakala au agent. Na pia kutengeneza uhusiano wa uamnifu ambapo huyo agent angekuwa anamtegemea huyu case officer karibia kila kitu ikiwemo usalama wa maisha yake. Hii haikuwa assignment rahisi hata kidogo.
Katika mafunzo haya Ames alikuwa mmoja wa waliopata maksi za juu na aliona taaluma hii ya CIA kuwa ni ya kisanaa zaidi kuliko ya kisayansi. Yes ofcourse spycraft is an Art.

Baada ya muda wa mafunzo mazito na magumu kwenye kambi hii ya "Farm' hatimaye walifuzu wote akiwemo Ames. Lakini ilitokea option au notice nyingine wakiwa hapo kwamba, kama kuna junior officer angetaka kujitolea kupata mafunzo mengine ya ziada ya jungle warfare paramilitary training kwenye kambi ya kijeshi ya Fort Sherman iliyopo karibu na mfereji wa panama kwenye nchi ya panama nafasi zipo. Wengi wa junior officers waliofuzu na Ames walikataa lakini ames alikubali.
Mafunzo haya ya ziada yalihusisha kozi kadhaa ikiwemo kuruka zaidi ya mara tano kutoka kwenye ndege kubwa ya kijeshi aina C-47 kwa kutumia parachuti hadi kutua chini. Pia mafunzo mengine yalihusisha matumizi ya silaha ambazo ni advanced na za kisasa.
Na mafunzo ya mwisho yalijulikana kama solo jungle survival skills ambapo Ames na baadhi ya maafisa wengine walipaswa kuruka na ndege hadi katikati ya misitu iliyoko panama kisha kushushwa na kuachwa huko wakiwa na kisu kidogo cha mkononi pamoja na compass pekee ambapo walipaswa kutafuta namna ya kuweza kutoka kwenye msitu huo salama hadi kwenye hiyo kambi ya fort Sherman kila mmoja akiwa Peke yake ndani ya siku tatu. Haya yalikuwa ni mazoezi ya kujitoa haswa . Na hatimaye Ames alifanikiwa kumaliza kozi hizi na kufuzu mwezi novemba mwaka 1961.



Sasa wengi wa maafisa au tuseme classmates wa Ames walipewa assignment na kwenda kufanya kazi kwenye nchi za Kisovieti na western Europe . Na baadhi yao walikuwa wanaendelea kupata mafunzo ya lugha ya ki Russia . Na kiuhalisia nchi za Kisovieti ndio ilikuwa lengo kuu la sehemu ya kukusanya taarifa za kijasusi na ikumbukwe miaka hiyo ndio.ile vita baridi katika ya Urusi na USA ipo kwenye peak yake.
Lakini kwa bwana Ames yeye alikuwa yupo interested na nia ya kufanya kazi kwenye nchi za Uarabu yaani mashariki ya kati.
 
Sehemu ya 03

Mwaka 1962 ndio mwaka Ames alipata assignment yake ya kwanza kwenda kufanya "kazi" Uarabuni kama CIA case officer. 1960s kipindi amabacho shirika la CIA lilikuwa linaanza kuajiri watu ambao wangeweza kutumia watu wengine katika kupata taarifa za kijasusi maeneo mbalimbali duniani. Na katika kutafuta na kupata"human sources " case officer au spy handler alipaswa awe mvumilivu haswa. Na asiwe mtu wa kukurupuka katika kutafuta hawa human sources au potential agents wa kuwapa au kuwauzia siri.

Na kweli mwkaa 1962 majira ya kiangazi Bob ames ,Yvonne na mwanao wa kwanza Catherine walifika kwa mara ya kwanza kwenye mji wa Dhahran Saudi Arabia. Hakika ilikuwa mara yao ya kwanza kukutana na hali ya hewa yenye joto kali inayofikia nyuzi joto 48 na upepo wenye mchanga wa jangwani. Eneo hili Ilikuwa kama ovena ya Uarabuni.

Walipokelewa na kuendeshwa na gari umbali wa maili nne hivi hadi ulipo ubalozi wa marekani ambao ulijengwa huko Saudi mwaka wa 1947-1951. Eneo hili lilikuwa na ofisi za wafanyakazi wa ubalozini, makazi ya balozi mwenyewe pamoja na majengo mengine ya ziada. Eneo hili la ubalozi lilikuwa generator yake ya umeme, kisima cha maji pamoja na mfumo wa septic tank. Pia Eneo hili lilikuwa pia limezungushiwa fensi ya mawe yenye urefu wa futi nne kwa ajili ya kuzuia ngamia na mbuzi kuingia kwenye ua au compound ya eneo hili la ubalozi.
Ubalozi huu ulikuwa unalindwa na vikosi vitano vya makomando wa U.S Marine ambao hawakuwa mbali sana na eneo hili la ubalozi wa marekani.
Eneo hili la ubalozi lilikuwa pia lina makazi ya raia 35 wa marekani, ikwemo wafanyakazi wa wizara ya mambo ya nje ,makarani pamoja na familia zao.

Sasa huyu ames katika ubalozi huu alikuwa ni afisa wa pekee wa pili wa CIA kuwepo hapo. Mwingine aliyetangulia kuwepo katika huu ubalozi alikuwa ni Bob carlson ambaye ndio aliyempokea Ames ambaye hapo kabla awali alikuwa amefanya kazi Beirut na Damascus kabla ya kuhamia Saudi Arabia.
Ikumbukwe kwamba mpaka ubalozi huu kuwepo kwenye huu mji wa Dhahran, ni kwamba serikali ya Saudi Arabia ilikataa ofisi yoyote inayohusiana na mambo ya nje kujengwa kwenye mji wa Riyadh kutokana na kwamba mji huu mkuu wa saudia ulikuwa ni makazi rasmi ya familia ya kifalme ya Saudi Arabia ya wahabbi roho ngumu yaani, Nedj. Hivyo basi eneo hili la ubalozi lilijulikana kama CIA Base na sio station .
Sasa katika assignment hii mpya hapo ubalozini,official cover ya Bob ames alitambuliwa kama commercial officer. Na kitabu maalumu chenye namba za staff wa ubalozi huo zilisomeka kwamba ames ni afisa wa kibiashara hapo ubalozini.
Hata huyu boss wa ames bwana bob Clarkson alitambulika kama "consul-political officer " kama official cover ambapo kazi yao haswa ina dili kukusanya taarifa za kiintelejensia hususani za kisiasa kwenye serikali ya Saudi pamoja na maeneo kimuungano ya Emirati (united Arab Emirates). Lakini lengo kuu haswa ni kukusanya taarifa za kijasusi ambazo labda ni vikwazo ambavyo vingeweza kuzuia maslahi ya marekani katika kuyafikia maeneo yanapochimbwa mafuta ghafi na pia kujenga uhusiano wa karibu na house of saud yaani familia ya kifalme ya Saudi.
Kama maafisa wengine wa CIA, huyu ames alipewa jina la bandia kwa ajili ya shughuli za kijasusi. Jina lake lilikuwa RAMES BIEDENKOPF. Na jina hili angelitumia katika kutuma au kupokea jumbe za siri hadi makao makuu ya CIA Langley Virginia.

Mazingira ya kazi hapa Dhahran hayakuwa ya kufurahisha sana na ilibidi Ames azoee . Uzuri ni kwamba alikutana na afisa mwenzake ambaye alimsaidia kupata experience kama junior officer wa CIA.

Sasa siku moja bwana Ames akiwa katika majukumu yake aliitwa na mwakilishi wa ubalozi mdogo wa marekani kwenye huo mji wa Dhahran bwana jack Horner kwenye ofisi yake. Lengo la kumwita ames ni kutaka kumwakilisha kwenye tukio la kukatwa kichwa kwa mtuhumiwa aliyoalikwa na Emir saud bin jiluwi kiongozi wa eneo hilo. Hivyo ames alipaswa kwenda pamoja na msaidizi wake jack Horner aliyeitwa Patrick theros. Ames aliamini chance kama hizi zingemsaidia katika kujuana na watu na kutengeneza connection muhimu ili zimsaidie katika harakati zake za ujasusi.

Na kweli siku ilipowadia waliendesha gari umbali wa maili 9 hadi Dammam square ambapo walikutana na umati wa watu uliokusanyika. Ames na theros walipofika walichokishuhudia ni mtu kuuawa kwa kukatwa kichwa kutokana na makosa aliyoyafanya tukio hili likiongozwa na saud bin jiluwi mwenyewe. Kwa mara ya kwanza walishuhudia hukumu inavyotolewa kwenye nchi ya Saudi Arabia. Na baadaye waliondoka. Ames alijifunza kitu kama jasusi wa CIA.
Maisha yakiendelea kama kawaida ndani ya Saudi Arabia, Yvonne na ames walipata tena mtoto wa pili wa kike waliyempa jina adrienne mwaka 1963 mwezi june. Na mwaka 1965 mwezi wa pili wakapata mtoto wa kike tena alipewa jina la kristen jumla watatu.
Ndani ya Saudi Arabia familia hii haikukaa sana , hatimaye bob na mkewe Yvonne walihamia hadi mji wa Beirut mwaka 1966 majira ya kiangazi. Apartment yao ilikuwa magharibi ya mji huu wa Beirut kwenye eneo la ras Beirut. Ni kipindi hiki ambapo Ames alikuwa anajifunza na kukielewa kiundani lugha ya Kiarabu ipasavyo.
Eneo hili la Ras Beirut ndilo eneo maarufu kwenye mji huu. Na Ames pamoja na familia yake walipata nafasi ya kukaa kwenye apartment ya ghorofa ambapo iliwapa nafasi ya kufurahia mandhari ya bahari ya Mediterranean .
Screenshot_20250805_055708_ReadEra.jpg
 
How are you
Me!
Do you understand English
Who me?
Are you jocking
Where!
Are you ok!, or we can meet another time.
When
See you
Where you going?
 
Wadau narudi soon.. tunajenga taifa kwanza
20250305_121803.jpg
 
Back
Top Bottom