Shadow7
JF-Expert Member
- Sep 28, 2020
- 13,773
- 20,165
Nkosana Makate ni raia wa Afrika Kusini ambaye alivumbua huduma maarufu ya ‘Please Call Me’ ama ‘Tafadhali Nipigie ‘, uvumbuzi ambao mpaka sasa kesi bado ipo mahakamani kufuatia kutokukubaliana fidia na mtandao wa simu ya Vodacom.
Makate anadai jumla ya bilioni 75 za Kitanzania ikiwa ni kama fidia kutoka katika kampuni hiyo ya Vodacom nchini Afrika Kusini
Kampuni ya Vodacom mwanzoni ilikuwa imekubali kulipa Makate Milioni 354 za Kitanzania ambayo mvumbuzi huyo wa Please Call Me alikataa.
Mzozo wa kampuni hiyo na mvumbuzi Makate upo Mahakamani. Huduma ya ‘Tafadhali Nipigie’ ililetwa sokoni kwa mara ya kwanza mnamo 2001.
Hii ni huduma ya sms ya bure ambayo inaruhusu wateja kutuma ujumbe kwa mtumiaji mwingine anayeomba apigiwe simu. Mvutano kati ya Makate na Vodacom umekuwepo kwa zaidi ya miaka 20 sasa.
Mahakama imetakiwa kutathmini upya fidia aliyopewa kama ilivyohesabiwa na Mtendaji Mkuu wa Vodacom Shameel Joosub. Hii ilifuata uamuzi wa Mahakama ya Katiba mnamo 2016 ambapo Vodacom iliamriwa kufanya mazungumzo na Makate ili kupata fidia ya haki.
Makate anadai jumla ya bilioni 75 za Kitanzania ikiwa ni kama fidia kutoka katika kampuni hiyo ya Vodacom nchini Afrika Kusini
Kampuni ya Vodacom mwanzoni ilikuwa imekubali kulipa Makate Milioni 354 za Kitanzania ambayo mvumbuzi huyo wa Please Call Me alikataa.
Mzozo wa kampuni hiyo na mvumbuzi Makate upo Mahakamani. Huduma ya ‘Tafadhali Nipigie’ ililetwa sokoni kwa mara ya kwanza mnamo 2001.
Hii ni huduma ya sms ya bure ambayo inaruhusu wateja kutuma ujumbe kwa mtumiaji mwingine anayeomba apigiwe simu. Mvutano kati ya Makate na Vodacom umekuwepo kwa zaidi ya miaka 20 sasa.
Mahakama imetakiwa kutathmini upya fidia aliyopewa kama ilivyohesabiwa na Mtendaji Mkuu wa Vodacom Shameel Joosub. Hii ilifuata uamuzi wa Mahakama ya Katiba mnamo 2016 ambapo Vodacom iliamriwa kufanya mazungumzo na Makate ili kupata fidia ya haki.