Mbesigwe
Member
- Sep 27, 2016
- 51
- 54
MFAHAMU MHE. HALIMA DENDEGO (RC-MTWARA).
Mhe. Halima Dendego kwa sasa ni mkuu wa mkoa wa Mtwara. Safari yake ya uongozi na harakati za kutetea haki za wananchi na raia wa Tanzania, zilianza tangu akiwa chuo kikuu cha Dar-es-salaam (UDBS-University of Dar-es-salaam Business School). Enzi hizo ilikuwa inajulikana kama Faculty of Commerce. Alikuwa miuongoni mwa wanaharakati machachali sana wa DARUSO kutokea fass kuanzia miaka ya 2001 mpaka alipomaliza elimu yake ya chuo kikuu.
Nyota yake na shauku ya kuwapigania watanzania bado iliendelea kung'aa kiasi kwamba akateuliwa kuwa Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa. Huko alijulikana sana kwa jinsi alivyokuwa karibu na wananchi ili kuhakikisha shughuli za maendeleo zinasonga mbele. Hakuona kuwa mkuu wa wilaya kuwa ni fahari kwake bali alipigania haki ya kila mwanampwapwa kwa nguvu zake zote.
Baada ya hapo alihamishiwa kilosa kwa nafasi hiyo hiyo ya ukuu wa wilaya. Ambako nako alikumbana na changamoto nyingi, kubwa ilikuwa ni vita na migogoro kati ya wafugaji na wakulima. Alitumia utashi wake kadiri alivyoweza kuweka hali sawa.
Baada ya kutoka kilosa akahamishiwa Tanga. Kabla ya kuteuliwa na Raisi kuwa mkuu wa mkoa wa Mtwara, ambako anatumikia mpaka sasa.
Falsafa yake ya kushirikiana na wananchi bega kwa bega bado aliendelea nayo. Ikumbukwe kuwa kwa kipindi ambacho aliingia mkoani mtwara ilikuwa ni kipindi kifupi tu kimepita tangu fujo zilizosabishwa na mzozo wa gesi na ujenzi wa Bomba la mafuta kuelekea DSM. Lakini hilo halikumvunja moyo, bali alihakikisha amani inaendelea kudumu ili shughuli za maendeleo zisonge mbele.
Akiwa mkuu wa mkoa wa Mtwara amefanya mambo mengi na mazuri jambo ambayo kila mwanamtwara anajivunia kuhusiana na huyu Mama. Zao la korosho amelibeba vilivyo kiasi kwamba sasa hivi tunajua thamani ya korosho jinsi ilivyo. Hakuna asiyefahamu jinsi Mhe. Halima Dendego alivyopambana na unyonyaji ambao ulikuwa unafanyika hasa kwenye hili zao la korosho, ama kwa hakika amejitoa mhanga juu ya jambo hili. Wanamtwara tushirikiane na kushikamana na mkuu wetu wa mkoa Jemedari wetu.
Mtwara ni yetu,
Nitasimama na mkuu wa mkoa wangu.
Mhe. Halima Dendego kwa sasa ni mkuu wa mkoa wa Mtwara. Safari yake ya uongozi na harakati za kutetea haki za wananchi na raia wa Tanzania, zilianza tangu akiwa chuo kikuu cha Dar-es-salaam (UDBS-University of Dar-es-salaam Business School). Enzi hizo ilikuwa inajulikana kama Faculty of Commerce. Alikuwa miuongoni mwa wanaharakati machachali sana wa DARUSO kutokea fass kuanzia miaka ya 2001 mpaka alipomaliza elimu yake ya chuo kikuu.
Nyota yake na shauku ya kuwapigania watanzania bado iliendelea kung'aa kiasi kwamba akateuliwa kuwa Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa. Huko alijulikana sana kwa jinsi alivyokuwa karibu na wananchi ili kuhakikisha shughuli za maendeleo zinasonga mbele. Hakuona kuwa mkuu wa wilaya kuwa ni fahari kwake bali alipigania haki ya kila mwanampwapwa kwa nguvu zake zote.
Baada ya hapo alihamishiwa kilosa kwa nafasi hiyo hiyo ya ukuu wa wilaya. Ambako nako alikumbana na changamoto nyingi, kubwa ilikuwa ni vita na migogoro kati ya wafugaji na wakulima. Alitumia utashi wake kadiri alivyoweza kuweka hali sawa.
Baada ya kutoka kilosa akahamishiwa Tanga. Kabla ya kuteuliwa na Raisi kuwa mkuu wa mkoa wa Mtwara, ambako anatumikia mpaka sasa.
Falsafa yake ya kushirikiana na wananchi bega kwa bega bado aliendelea nayo. Ikumbukwe kuwa kwa kipindi ambacho aliingia mkoani mtwara ilikuwa ni kipindi kifupi tu kimepita tangu fujo zilizosabishwa na mzozo wa gesi na ujenzi wa Bomba la mafuta kuelekea DSM. Lakini hilo halikumvunja moyo, bali alihakikisha amani inaendelea kudumu ili shughuli za maendeleo zisonge mbele.
Akiwa mkuu wa mkoa wa Mtwara amefanya mambo mengi na mazuri jambo ambayo kila mwanamtwara anajivunia kuhusiana na huyu Mama. Zao la korosho amelibeba vilivyo kiasi kwamba sasa hivi tunajua thamani ya korosho jinsi ilivyo. Hakuna asiyefahamu jinsi Mhe. Halima Dendego alivyopambana na unyonyaji ambao ulikuwa unafanyika hasa kwenye hili zao la korosho, ama kwa hakika amejitoa mhanga juu ya jambo hili. Wanamtwara tushirikiane na kushikamana na mkuu wetu wa mkoa Jemedari wetu.
Mtwara ni yetu,
Nitasimama na mkuu wa mkoa wangu.