Kituko
JF-Expert Member
- Jan 12, 2009
- 9,555
- 9,330
Jamani kunguni wamevamia kitanda changu leo siku ya tatu.... yaani usiku wa jana sijalala kabisa wamenishambulia vibaya mno... hapa mwili wote umevimba,unawasha na unauma..
mwenye dawa ya kuua kunguni na wasirudi tena anitajie maana nshatumia dawa kibao bila mafanikio...
msaada wenu wakuu maana daaaah hawa wadudu watanitoa roho mwaka huu... wananitesa sana,nashindwa kufurahia maisha hasa inapofika usiku.
Kunguni ni wadudu wanaoishi kwenye uchafu, inaonekana kitanda chako ni kichafu sana na kina vumbi la kutosha tu, toa kila kitu nje, safisha chumba chako kila siku
fua mashuka kila mara na hakikisha kuna mwanga wa kutosha chumbani kwako