Message! Message! imeingia

Pole kaka, tena unaonekana wewe ni mlokole kama sijakosea kutokana na ID yako hapo juu. Pengine nikuulize, mna mda gani katika ndoa na ulishawahi kumuuliza hizo message zina husu nini, na jibu lililikuwaje? Vipi na maelewano yenu kila mmoja anauwezo wakuwa free na simu ya mwenzie! Baada ya hapa then tutaendelea...

Yawezekana ni born again .Lakini ajua kwamba hata kama mkewe ni born again sio exeption inavyokuja suala la mahusiano nje ya ndoa. Tizama MATENDO UTAMTABUA MWENYE HILA NA MUADILIFU.
 
Last edited:
Mkuu,
In that and other marriage issues, there are two things to decide, na vyote haviendi pamoja. You can decide to be HAPPY and forego being RIGHT. If you want to be RIGHT (kifanyike unachotaka) then forget being HAPPY. If you decide to be HAPPY (enjoy your familly) then forget about being RIGHT. yaani forget about what you want it to be.

I think that works in most cases. Me i would choose to be HAPPY and enjoy my Beer!
 
Halafu hizi message za enzi za mwalimu nilishapiga marufuku mtu kunitumia, ule nao ni ujinga mtu mzima unakaa chini kusambaza message za kipuuzi. Unateketeza hela pasipo sababu.

Unajua tena makampuni yetu ya simu,, lazima yawapate wajinga na wajinga ndio waliwao.....
 
Kinachotakiwa hapa ni kumweleza tu wife wako kuwa kitendo hicho hukipendi na akiache mara moja. Sio vizuri kukaa na jambo kama hilo moyoni wakati una uwezo wa kumwambia hupendi hiyo tabia. Kwa mtazamo wangu simu inapokuwa busy sana na mesage lazima kutakuwa na chating inaendelea, kwa hiyo asilimia kubwa ya meseji hizo itakuwa hazina maana kuliko maongezi yako na yeye.
 
Sidhani kama kutumia nguvu au vitisho ni suluhisho na pia sio kweli kwamba hizo messages zote zinahusiana na mapenzi. Inawezekana, lakini pia inawezekana tu ni mambo mengine. Ni mambo yasiyopendeza kwani yanatoa kipaumbele kwa mtu au watu wasiostahili? NDIO.
Dawa ni kumfahamisha tu mama kuwa hilo linakukwaza na hulipendi na ungeshauri aliache ili kutoa kipaumbele kwa anayestahili ambaye ni mume. Mkumbushe kuwa hata wewe unaweza kuwa na simu na ukaamua kuendekeza anayoendekeza yeye na una hakika hatapendezewa. Asilopenda kufanyiwa yeye na basi asimfanyie mwingine.
Ni muhimu kumkumbusha wajibu wake kwani sisi binadamu tunahitaji saa zingine kukumbushwa. Usije ukamuachia akapotea ukabaki unasikitika. Anaweza akawa na mazuri mengi kulinganisha na mapungufu hayo ya messages. Pia anaweza tu kuhadaika, hivyo kumuokoa kweli hilo ni wajibu wako. Sidhani kama humpenda kwani usingemuoa au usingehangaika kutaka ushauri, hivyo basi usingependa apotee na kujikuta anahangaika baadae kwa kuhadaika tu.
Ndoa ni kuleana, kukumbushana, kufundishana/kuelimishana, kueleweshana,kusikilizana, kuheshimiana na kupendana.
Utakuwa unatimiza wajibu wako kumkumbusha nani ni muhimu katika ndoa yake. Akichagua hao usiowajua basi, lakini utakuwa umetimiza wajibu wako wa kumkumbusha na pia utakuwa umepigania haki yako ya kujaliwa.
Ndoa ina mitihani mingi mno hivyo nenda taratibu.
 
Nipatie namba yake halafu tuone kama hizo message zitafululiza kihivyo unavyolalamika?!Then,nitakuja na plan B endapo hiyo haitafanya kazi.
 
Nipatie namba yake halafu tuone kama hizo message zitafululiza kihivyo unavyolalamika?!Then,nitakuja na plan B endapo hiyo haitafanya kazi.

Thnks for u r info but leta hiyo plan A+B hapa kila mtu kwenye bord aelewe nini cha kufanya
 
...wala usikereke ndugu yangu, mu ignore tu japo unakufa na tai shingoni, tafuta jambo la kuku keep busy nawewe mpaka huo mzuka wake utapotulia...!

...kumnyang'anya hicho kilonga longa wala sio suluhisho la kudumu.
dawa ya moto ni moto?
....wewe chukua kisimu chake kibamize chini vunjilia mbali sim card yake......mzuie kwa mwezi mmoja kutumia simu......kisaha mtafutie namba mpya......
 
dawa ya moto ni moto?
....wewe chukua kisimu chake kibamize chini vunjilia mbali sim card yake......mzuie kwa mwezi mmoja kutumia simu......kisaha mtafutie namba mpya......

No!

...ndio hapo naye atapoibamiza chini na kuisambaratisha laptop/desktop yako kwa sababu ya addiction yako kwa Jamiiforums na mitandao,....!


"usipo ziba ufa utajenga ukuta..." siamini huyo mwanamama anajifanya hamnazo bure bure tu na hicho kilonga longa chake. Kuna 'chanzo' kinachompelekea huyo madame sasa kuamua kufanya ujeuri, ambao Mkuu hajatuelezea hapa!

Kama Mkuu alikuwa akirudi nyumbani yeye ni mtandaoni tu, au magazetini, au sijui kukamata remote kuangalia mechi kwenye TV. Mwanamke anapojiona hapati attention, naye anaamua kutoa somo, Matokeo ndio haya...

Mind games ndugu yangu, mind games, ...bahati mbaya/nzuri, wanawake ni wastahmilivu sana..
 
Kama Mkuu alikuwa akirudi nyumbani yeye ni mtandaoni tu, au magazetini, au sijui kukamata remote kuangalia mechi kwenye TV. Mwanamke anapojiona hapati attention, naye anaamua kutoa somo, Matokeo ndio haya...
hii JF mkuu itakuja kuvinja ndoa za watu.....kama jamaa alikuwa anakomaa kwenye jukwaa la siasa anajisahau kumpa mkewe....
 
hii JF mkuu itakuja kuvinja ndoa za watu.....kama jamaa alikuwa anakomaa kwenye jukwaa la siasa anajisahau kumpa mkewe....

Ndo hapo sasa...everything has a bignning, and the biginning has and end. Ndugu yangu kaa chini tafakari ni nini chanzo cha yaho yote! then anzia from the mizizi kusolve the problem. Upo hapo ndugu katika bwana! ALL THE BEST
 
dawa ya moto ni moto?
....wewe chukua kisimu chake kibamize chini vunjilia mbali sim card yake......mzuie kwa mwezi mmoja kutumia simu......kisaha mtafutie namba mpya......

Duh! ndo maana tulikukimbiaga wengine...hii ni balaa my shem to balata (beibberry), mwee mbona jazba hivyo...ingekuwa ndo wewe sijui...huruma to my wifi kama yupo au to be. lol.:(
 
Siku ya kwanza najiunga na shule ya Upili miaka ya 80 nilikutana na swali. Ni swali ambalo siku hizo nililiona la ajabu na lislo na maana kabisa; swali la kipuuzi, lakini siku hizi ni moja ya njia zangu za kudharau watu na kuachana na mambo yao. Swali ni hili
Kuna utumwa na utumwa. Kuna utumwa wa kutumwa na utumwa wa kujituma; kuna wa mwili na utumwa wa akili. Mradi kuna utumwa na utumwa; Jadili. Kwa ufupi iwapo unachosema ni sahihi mkeo ni mtumwa wa teknologia ya mawasiliano na la maana ni kumpa ushauri wenyewe wanaita USHAURI NASAHA naamini atakuelewa, asipokuelewa hebu akapumzike kwao kidogo
 
Siku ya kwanza najiunga na shule ya Upili miaka ya 80 nilikutana na swali. Ni swali ambalo siku hizo nililiona la ajabu na lislo na maana kabisa; swali la kipuuzi, lakini siku hizi ni moja ya njia zangu za kudharau watu na kuachana na mambo yao. Swali ni hili
Kuna utumwa na utumwa. Kuna utumwa wa kutumwa na utumwa wa kujituma; kuna wa mwili na utumwa wa akili. Mradi kuna utumwa na utumwa; Jadili. Kwa ufupi iwapo unachosema ni sahihi mkeo ni mtumwa wa teknologia ya mawasiliano na la maana ni kumpa ushauri wenyewe wanaita USHAURI NASAHA naamini atakuelewa, asipokuelewa hebu akapumzike kwao kidogo


Kivipi awe mtumwa wa mawasiliano? mimi nadhani yeye yuko busy na mtu huyo anayewasiliana naye kwa hizo sms.
 
Acha Mkuu siku hizo kulikuwa na wanachama wachache lakini hapa palikuwa bomba sana na akina dada pia walikuwa wachache sana lakini waliokuwepo walikuwa wanachangia sana mambo ambayo kwa kweli yalifanya mijadala hapa kuwa bomba sana na iliyoenda shule. Watu wengi walikuwa hawataki hata kukosa sekunde ya kutokuwepo hapa, halafu MODS nao walikuwa wakichapa kazi mtindo mmoja hakuna kurusha tusi ukirusha tusi tu kibano cha wiki nzima au hata mwezi mzima. Na mtu akija na tatizo lake kuomba ushauru watu walikuwa wanampa ushauri muhimu ambao unaweza kumpa ndugu au rafiki wa karibu siyo kumzodoa.

mkubwa upo wapp
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom