Wewe Javiary ndiyo kilaza mwanaizaya mkubwa! Kama siyo kazi kubwa ya walimu wako bila shaka tusingekujua humu JF na huo utumbo wako wala tusingeuona. Hakuna serikali yoyote duniani inayoweza kupata maendeleo endelevu kwa kudharau elimu. Na unapoongelea elimu mdau wake mkubwa ni mwalimu,pasipo mwalimu hakuna zuri lolote linaloweza kufikiwa. Unajua kwanini Japan na nchi zingine za ulaya zimeendelea? Kubwa ni kwasababu wamewekeza katika elimu,nyie hapa Bongo kwa ujinga mnawekeza katika siasa. Hebu fikiria mbunge ambaye kazi yake ni kulala na kugonga meza tu pale bungeni analipwa zaidi ya Tsh 7/= milioni kwa mwezi na posho ya Tsh 200000/= kwa siku wakati mwalimu analipwa Tsh 240000/= kwa mwezi pesa ambayo haitoshi japo kwa matumizi yake ya nusu mwezi. Mwalimu huyo huyo anaomba aongezewe mshahara ili aweze kujikimu wakati anaendelea na kazi ya kuelimisha watoto wa taifa hili,jibu la Rais anadai kuwa hata walimu wagome kwa miaka nane(8) hawawezi kuongezewa mishahara. Kwa kauli hiyo ya Rais ulitaka walimu wafanye nini? Hapa nani kilaza,walimu au wale wasiotaka kuwekeza katika elimu na badala yake wanaweka vipaumbele katika mambo ambayo hayastahili? Jenga hoja acha kuleta ujinga wako.