Mengi (WATANZANIA) Vs Prof. Muhongo (WAWEKEZAJI)

Mengi (WATANZANIA) Vs Prof. Muhongo (WAWEKEZAJI)

ilboru1995

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2007
Posts
2,329
Reaction score
269
Mengi anasema kuwa Dhahabu yote ya Tanzania inathamani ya dolla 60 Billion ambapo wageni wanamiliki 99.99% Iweje Gesi yenye thamani ya dola 500 Billion iendelee kumilikiwa na wageni kwa 100%?... Mengi hapa anapoint, wananchi wa Mtwara nao wanastahili kuungwa mkono kwa nguvu zote!!! Dhahabu inakwisha, Almasi wameshaimiliki kabla ya uhuru, Tembo na wanyama wengine wanauawa, iko siku Mt Kilimanjaro nayo watailipua...sijui tutabaki na nini zaidi ya mabusha na vitumbua...Prof Muhongo pamoja na kwamba wewe ni EHM unaetumiwa na mabwana zako wa ulaya lazima utambue kuwa nchi hii inatuhusu sote...fedha za Mobutu ziko wapi? mitego ya kuwekewa fedha Uswis ni wa kishamba wanakuhadaa hao mabazazi... siku si nyingi utatukumbuka ...
 
naisi baraza lipya tunaweza kumkosa prof muhongo, coz meng ana influence kubwa sana kwa JK.
 
Muhongo hyo wizara mwsho kuongoza ni 2015 kaa na Watanzania vizuri.
Watanzania ni wakuuza juice tu?
 
Mengi asidanganye watu hajapata kitu kwenye gesi ndiyo maana anahangaika sana atupishe atuache.
 
Muhongo hyo wizara mwsho kuongoza ni 2015 kaa na Watanzania vizuri.
Watanzania ni wakuuza juice tu?

Mbali sana hiyo 2015. Jk akipiga reshuffle, jamaa atapigwa sub tu!!
 
Kutokana na upeo wako mdogo wakufikiri ndio unaona hvyo ila kwa wale tunao mfahamu Mengi tunajua anatetea maslahi ya watanzania juu ya umilikaji wa rasilimali za taifa.
Wewe unafanyia nipashe au redio one tunajua anakupa ugari huwezi kumpinga endelea na mzee wako.
 
Wewe unafanyia nipashe au redio one tunajua anakupa ugari huwezi kumpinga endelea na mzee wako.
Mkuu wewe kama wewe unaridhia wageni kumililiki rasilimali zetu kaskazini hadi kusini? Kwataarifa yako hazina kubwa ya duniani iko baharini! Mtadhibiti vipi ukwapuaji wakati sehemu yote ya bahari inamilikiwa na nchi kubwa duniani zenye nguvu za kijeshi na kiteknolojia?...
 
Mbali sana hiyo 2015. Jk akipiga reshuffle, jamaa atapigwa sub tu!!
Itakuwa ngumu sana JK kumtema huyo EHM wa USA... Alipelekwa SA kunolewa na sasa anabweka kwa niaba ya watu wa marekani ...Hataki kusikia kuwa watanzania wanatia mguu kwenye madini na nishati! Wachina walipewa ile mikataba kwa bahati mbaya sana, tumshukuru aliedakwa kule China ...
 
Mengi asidanganye watu hajapata kitu kwenye gesi ndiyo maana anahangaika sana atupishe atuache.
Mkuu mjepo, jaribu kujiongeza japo kidogo tu, au wewe ni robot? wameformat brain yako?... nikweli kuwa huoni hatari kwa rasilimali zetu kumilikiwa na wageni?
 
Hiyo conflict of interest inayo attract interest za wananchi waliowengi inaubaya gani? wewe kama wewe Kasheshe hupendelei wananchi wamiliki Rasilimali zao Dhahabu na Gesi?...


Mbona hatukumsikia akipiga kelele kama hizo kwenye uwekezaj wa madini au kwa sababu alipewa vitalu.
 
Mbali sana hiyo 2015. Jk akipiga reshuffle, jamaa atapigwa sub tu!!

Mengi Ana washabiki wake na Muhongo Ana washabiki sasa liandaliwe pambano la Ngumi uwanja wa taifa Tujue ni nani Zaidi ktk nguvu za mikono kinyume na hapo watu watashabikia malumbano ya Wazee wawili pasipo kujua hatma yake
 
Mengi ni mzee mzalendo sana. Muhongo ni msomi ambaye ana kiburi cha ufahamu. He has intellectual arrogance.
 
Haya Malumbano ya prof na Dr sidhani Kama yanawasaidia watanzania sana sana yanawafanyia promo hao wawili hii Ndio Tz zaidi ya Uijiavyo sasa watu wamekaa wakibuni hv Mara vile watu wengi ni kama hawajui wamshabikie nani Kati ya Mengi ambaye huwa na mwanachama wa Yanga na muhongo sijui ni timu gani !
 
Hivi Muhongo miaka aliyoishi Tanzania na aliyoishi nje ya Tanzania ipi ni mingi? Kama mimi kabla hajachagulia kuwa mbunge wa viti maalum nilikuwa hata simjui. Lakini Mengi tangu nipo shule ya msingi namfahamu. Hivyo akili yangu inanituma kuwa Muhongo amekaa mda mwingi nje ya nchi na pia amewahi kuukana uraia wa Tanzania na kuchukua uraia wa kigeni. Alivyoitwa kuwa mbunge wa viti maalum ili apewe uwaziri ndipo akapewa uraia wa Tanzania.Kwa mtu kama huyu je atakuwa na uchungu kwa WaTZ? ndio maana siku zote amekuwa akiendekeza dharau kwa waTZ na sisi tunamwangalia tu.
 
Mengi ni mzee mzalendo sana. Muhongo ni msomi ambaye ana kiburi cha ufahamu. He has intellectual arrogance.
Msomi yeyote mwenye kujiona msomi hawezi kuambiwa jambo la kipuuzi akalikubali kisa kasema Mzungu! Huyo atakuwa ZUZU tu...Kwanini wasomi wengi ndo wahujumu uchumi katka nchi za kiafrika?... Elimu yao inamanufaa gani kama haiwezi kuinufaisha jamii yake?
 
Back
Top Bottom