Mengi awaponda wanaomwandama

Ushauri nasaha kwa Mzee Mengi Watanzania hatuna haja ya kutaka kujuwa Urafiki wake wa karibu na watokea zamani kwa Rais Kikwete sisi hautusaidiii ni yurafiki wenu na mnajuwana wenyewe au mtajuwana wenyewe kwani Mtaka nyingi nasaba hupata mwingi msiba wahenga walinena. Towa ushahidi Mahakamani wa Mafisadi PAPA nasi tuko Nyuma yako, lakini ikiwa sio kweli umesimama kwa ajili ya Kukashifu wenzako kwa mitizamo ya kiushindani wa Kibiashara basi tarajia kupata laana ya Walalahoi tuliowengi ndani ya Nchi yetu, tumechoka kusikia kila uchao nyimbo hii ya UFISADI Sisi tuliowengi tunasubiri kuona hatuwa dhidi yao zikichukuliwa harakiza kwenda Mahakamani hivi sasa ili haki itendeke na ionekane kuwa inatendeka.


Hivi kweli wewe kutoka ndani ya moyo wako unaona kweli alio wataja Mengi si mafisadi wanao liangamiza taifa letu?

Anza na nafsi yako kuona ukweli ulipo.. hizo siasa na propoganda ndizo zimetufikisha hapa tulipo, haya majamaa ni mafisadi mabaya sana na mabinafsi makubwa ambayo hayafai kabisa katika jamii ya wanyonge watanzania wano taabika kwa kufisadiwa kila kilicho chao!
 
mzeee mengi vipiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii????????????????????? usiwasikilize sana washauri wako wanakupotosha sasa. unaongea mno mzee wangu. hebu rudisha ile busara yako ya kila siku usiwasikilize wapambe mzee wangu. UNATUANGUSHA SASA
 
source ni taarifa ya habari ya 1 june 2009 saa 2:00 usiku ITV. Ilikaa hewani kwa muda wa kutosha, na Baba Askofu akampongeza na kumwambia aendelee kufanya kazi ya Mungu asitishike wala asiogope waumuni na waTz wako nae. Na alimbariki sana. Ilikuwa nikwenye kanisa moja huko Moshi
 
Mwacheni Mzee wetu Mengi akautoe ushahidi wake mahakamani. Anazijua na anaziheshimu sana mahakama kwani ndiko hasa chimbuko la utajiri wake wa sasa. Kesi yake na NBC yetu ndio iliyombadilishia maisha. Jana pekee amemwaga milioni 400 hapo kijijini kwao kwa miradi mbalimbali. La kumuuliza labda ni kama anajua mchakato mzima wa Urais wa JK mwaka 2005?
 
Wakuu,

Televesioni ya ITV ilikuwa ikitanganza (since Monday) kuwa jana usiku wangeonyesha Kipindi maalum, but kwa sababu zilizokuwa nje ya uwezo wao "ghafla bin vuu" wakasitisha kukionyesha!

Kwa walio na rekodi huru na sahihi ni nini hasa kilichotakiwa kuonyeshwa na ni kwa sababu gani wakasita ghafla?
 
Mkurugenzi mtendaji wa IPP Bw Reginald Mengi amewaponda Jeshi la Polisi, Takukuru, kamati ndogo ya usalama wa taifa kwa kumuhoji na kumwagiza apeleke ushadi juu ya mapapa aliowataja katika kituo chake cha Tv cha ITV, vile vile amewaponda Sophia Simba kwa kumkejeli kuwa amechemka na Bw Mkuchika kwa kumuita kuwa ni racist, amehoji ni nani yuko juu ya sheria baada ya waziri mkuu kutoa tamko la kwamba mahakama iachiwe ifanye kazi yake.

CORRECTION- hajawaponda Takukuru kawasifu na kusema ni taasisi pekee inayomtendea haki.Kuna muda Waislamu walishambuliwa sana kwa kuchanganya dini na siasa,sasa Mengi kila kukicha kusimama kanisani na kuongelea siasa 1.atawatenga waislamu na kuziona juhudi zake ni za kikristo, 2.kuchanganya dini na siasa, 3.kwakuwa mwenyewe kasema swala liko mahakamani na hawezi kuongea na vyombo vyo dola basi naye aachie mahakama swala hili.
 
Probably walitaka kumuonyesha Mengi alivyo ongea juzi na lawyers wake wakamshauri asifanye hivyo.
 
Hivi huko kanisani kuna nini mpaka kila mtu akimbilie?

tunakoenda ni kubaya zaidi na watu watatumia dini kutugawa


nimesoma hapo nyuma,eti Rafiki wa Mengi ni Jk?duh...Kazi ipo!
 
Mzee mengi si mjinga kama wengine humu wanavyofikiri kirahisirahisi, yuko timamu anajipanga vema tu kabla haongea kitu.
 
Labda walitaka kurusha live ile ya moshi...marangu huko alipoenda kuomba msaada wa kusaidiwa na kuonewa huruma na waumini ............kupitia jukwaa la kanisa....mmm mbona RA walimponda hadi kanisa likatoa tamko???mbona yeye amekwenda kusemea huko..???
 
wakuu,

televesioni ya itv ilikuwa ikitanganza (since monday) kuwa jana usiku wangeonyesha kipindi maalum, but kwa sababu zilizokuwa nje ya uwezo wao "ghafla bin vuu" wakasitisha kukionyesha!

kwa walio na rekodi huru na sahihi ni nini hasa kilichotakiwa kuonyeshwa na ni kwa sababu gani wakasita ghafla?


wamedilu (wamegwaya) kumuonyesha mengi akiongea na maaskofu wa uchagani kuhusu ufithadi babangu bwashee
 
Ninyi ndio mnaoipeleka Tz bapaya kwa uwoga wenu. Biblia inasema heri mtu mmoja kufa na wala sio taifa zima kuangamia wewe bado unaendekeza mambo ya kijinga na upumbafu, kwani matatizo/ kifo si ameumbiwa mwanadamu. Mengi sio mjinga kuzungumza bila data. Nchi hii inahitaji ujasiri wa KIPALESTINA NA TAMIL TIGERS wa kuvaa mabomu na kulipuka na watu kama afanyavyo Mhe Mengi

Hatari iliyopo juu ya ujasri wake in kwamba ataangamia yeye mwenyewe na kuwaangamiza wengine ambao siyo walengwa kama tunavyoona kwa wale wanaojitoa muhanga; ninamfanaisha Mengi na Mrema katika harakati zake za miaka iliee..!!. Unaweza kuwa na nia njema katika kutekeleza jambo fulani lakini ukakosa mipango sahihi katika utekelezaji wake. Nia ya Mrema haikutimia juu ya Taifa hili. Mimi sifurahishwi na taarifa zinazotolewa juu ya watu wachache kutumia raslimali za Taifa letu kwa manufaa yao, lakini wasiwasi wangu ni harakati zilizoanzishwa na Mzee Mengi kutokuzaa matunda. Mimi nafikiri huu sio wakati wa kuendelea kumtafuta mchawi aliyetufikisha hapa tulipo, badala yake Mzee Mengi angeendelea kuwahamasisha vijana katika elimu na uhamasishaji katika uzalishaji mali na kutoa mbinu mbadala zilizomfikisha yeye hapo alipo. Ninaamini kinachotusumbua ni huu ujinga wetu na unyonge uliotawala katikati ya watanzania wengi.
 
Labda walitaka kurusha live ile ya moshi...marangu huko alipoenda kuomba msaada wa kusaidiwa na kuonewa huruma na waumini ............kupitia jukwaa la kanisa....mmm mbona RA walimponda hadi kanisa likatoa tamko???mbona yeye amekwenda kusemea huko..???


Mzee Mengi hataki huruma ya mtu yeyote. Kwa nini afuatwefuatwe wakati analisemea taifa na uozo wake kupitia mafisadi ambao wameifikisha nchi katika umaskini unaotokana na pesa ya walipa kodi kulipia gharama za wezi badala ya kujenga uchumi. Mengi alinisemea mimi na kizazi changu pamoja na watanzania wazalendo wote ambao wana uchungu na nchi hii. Hata kama RM angekuwa ni fisadi papa au nyangumi lakini faida za ufisadi wake tunazipata wote hapa. Mafisadi wote wa Kihindi, Kiarabu na Kiirani si wote wana account zao main nje ya nchi, to name a few Uswiss, Dubai (a new destination), Uingereza, nk. ???

Jana nilifurahi sana wakati alipokuwa anaongea na kufahamisha umma jinsi ambavyo serikali na dola imemwandama eti kwa kusema ukweli. Serikali na dola ingetakiwa impe Mengi Nishani kwa kuwa shujaa. Keep up Mzee wetu Mengi na wale wote ambao wako nyuma yake kumtia nguvu na shame to Mafisadi na kibaraka wao mkuu Serikali na Dola. shiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiit.
 
Tuwe makini na taarifa au mada tunazozitoa ili kulinda heshima za watu wengine au mnataka kusema hayo yote mliyosema yanamaadili.Lete mada vizuri tuchangie.Tusiwachonganishe watu.Hata kama ni rafiki yake mkuu kuna tatizo gani?au na ninyi mafisadi papa?
 
unafikiri wao wajinga, juzi hapa si tuliletewa humu barua ndeeeefu toka tcra wanamuuliza kwa nini asishtakiwe? na akaitwa kule trca kutoa maelezo.
 
Sakata hili linanikumbusha ile hadithi ya bwana yesu alipowataka wana wa uyahudi watupe mawe dhidi ya mama aliyetuhumiwa kwa uzinzi alipoinuka akakuta wote wamesambaa
 
kuna mvutano mkubwa sasa hivi kati ya mengi na serikali na ndio maana serikali inafanya mpango wa kuleta sheria mpya itakayo mfanya mtu hasimiliki zaidi ya chombo kimoja cha habari.hapa serikali inajaribu kujiandaa na uchaguzi kwa kuwanyamazisha watu sana sana mengi .sasa kufungia vyombo vya habari hapa serikali wanashindwa kufikiria kwamba watanzania watapoteza kazi zao? au hilo kwao hawafikirii? je tatizo ni kuwa na vyombo habari vingi au tatizo ni habari zinazotelewa na hivyo vyombo vya habari? manake kama unafungia chombo cha habari kwa vile kinaandika habari ya ufisadi hata chombo kimoja cha habari atakacho miliki huyo mtu ataweza kuandika hio habari.serikali inafanya makosa kwa hilo swala ni je hio habari ni ya ukweli au sio ya kweli? kama chombo cha habari kimetoa habari ya uongo kwanini usiende mahakamni kushitaki habari hio?
na je hio sheria ya kila mtu amiliki chombo kimoja cha habari ni kwa watu binafsi tu au na wao serikali? manake serikali ina vyombo vingi tu vya habari.je hii ni haki au ni ubabe wa serikali kama kawaida yao?
 
kuna mvutano mkubwa sasa hivi kati ya mengi na serikali na ndio maana serikali inafanya mpango wa kuleta sheria mpya itakayo mfanya mtu hasimiliki zaidi ya chombo kimoja cha habari.hapa serikali inajaribu kujiandaa na uchaguzi kwa kuwanyamazisha watu sana sana mengi .sasa kufungia vyombo vya habari hapa serikali wanashindwa kufikiria kwamba watanzania watapoteza kazi zao? au hilo kwao hawafikirii? je tatizo ni kuwa na vyombo habari vingi au tatizo ni habari zinazotelewa na hivyo vyombo vya habari? manake kama unafungia chombo cha habari kwa vile kinaandika habari ya ufisadi hata chombo kimoja cha habari atakacho miliki huyo mtu ataweza kuandika hio habari.serikali inafanya makosa kwa hilo swala ni je hio habari ni ya ukweli au sio ya kweli? kama chombo cha habari kimetoa habari ya uongo kwanini usiende mahakamni kushitaki habari hio?
na je hio sheria ya kila mtu amiliki chombo kimoja cha habari ni kwa watu binafsi tu au na wao serikali? manake serikali ina vyombo vingi tu vya habari.je hii ni haki au ni ubabe wa serikali kama kawaida yao?

Serikali inatakiwa siku zote ijali wazalendo wake. Serikali inatakiwa iwawezeshe wazalendo wake (indeginous empowerment) in all spheres, especilly owenrship of the economy. I doing so, policies and Acts must safe guard the long term and sustainable efforts of the citizens, especially indegionous. Je Tz inafanya hivyo??? Iko tayari kutetea interest za fisadi kwa kuwa anachangia siasa badala ya kutete interest za locals ambao wanachangia na kutetea sustainable and real economy??? Leo hii mifisadi yote na jamaa zao wa karibu wana uraia zaidi ya moja, sasa huyo ni sustainable!!!! ???Nachelea kusema hatuna serikali ya watanzania kwa manufaa ya watazania wazalendo, bali tuna serikali ya mafisadi tu. Samahani sana kwa wale ambao nawaudhii ila msimamo wangu ndiyo huu na si msimamo wa Uongozi wa Jamii Forums, its Founder, and any other member.

Ningekuwa naweza ningebadili uraia, au kuhamia nchi nyingine, ningekubali kuwa uhamishoni kama akina Kambona. Ila tu huko ugenini ningekuwa treated as a fifth class resident wakati Tanzania mgeni is a first class citizen (not resident), kuna tofauti hapo tena kubwa tu. Tunahitaji mapinduzi ya haraka.
 
Back
Top Bottom