Nyumani kwetu tulikuwa tukisumbuliwa na mende kwa miaka 10 katika miaka yote hiyo tulikuwa tukifanya fumigation kila baada ya miezi sita tumekuwa waangalifu kwa usafi kwa kila namna ile lakini mende walikuwa sehemu ya wenyeji ,kila kona tupo nao jikoni ilikuwa makao makuu yao,usiku ukiwashaa taa mende unawaona wanazagaa kila kona,ilikuwa kero haina mfano.
Kuna siku tilitembelewa na mgeni kutoka Nairobi akaona mende,akatuuliza na shuida y mende humu kwenu?Tukamwambia ni kero kupita maelezo,yule Bwana akautuambia kuna dawa atatumia inaitwa BORIC ACID POWDER!
Unaichanga na unga na sukari unaweka kwenye maeneo yote yenye mende kwenye makabati ukutani nk
Katika wiki mbili hakuna hata mende mmoja tuliona waliteketea haswa,na cha ajabu huwa wakifa wanatoweka wanakimbia ,Leo mwaka 2 hatujui tena mende ,unaweza google kuhusu borci acid inavyo fanya kazi kuua mende