Membe: Wasiomtakia mema Rais Kikwete wananuna ujio wa Rais Obama!

JEMEDARI .H.

JF-Expert Member
Oct 29, 2012
341
54
Waziri Bernard Membe amesema wasiomtakia mema rais kikwete wananuna ujio wa Raisi wa Marekani Obama hapa Tanzania.

-------------------------

Kwa mujibu wa Benard Membe, viongozi wooote wa East African Community wamealikwa kutokana na ujio wa Obama huku Membe akijaribu kusisitiza kwamba hapo ndipo Kagame anapotakiwa kuja kutoa msimamo wake, bial shaka kutokana na suala la ushauri aliopewa wa kufanya mazungumzo na FDLR!

Aidha, ni kama vile ameshauri wana-Dar es salaam kuangalia upya ratiba zao kipindi ambacho Obama atakuwa Dar kwani ni kama Tanzania/Dar itasimama!!
Source: CLOUDS FM

Leo waziri wa mambo ya nje ametoa kauli tata ikiwa ni mwendelezo wa kauli tata za watawala wa CCM baada ya kuwataka watanzania wasiende DSM kwasasa maana pamejaa. Ameendelea kusema anaomba waende DSM baada ya wageni kuwa wameondoka. Haya ameyasema akiwa anahojiwa na kituo cha habari cha ITV. Nae Kamanda wa kanda maalum DSM Kamanda Kova amewaomba watanzania wawe na ushirikiano na wageni hawa, na kama watasahau vitu kama Laptop, simu na vitu vingine vya thamani amewaomba watanzania wawarudishie.
 
Kwa mujibu wa Benard Membe, viongozi wooote wa East African Community wamealikwa kutokana na ujio wa Obama huku Membe akijaribu kusisitiza kwamba hapo ndipo Kagame anapotakiwa kuja kutoa msimamo wake, bial shaka kutokana na suala la ushauri aliopewa wa kufanya mazungumzo na FDLR!

Aidha, ni kama vile ameshauri wana-Dar es salaam kuangalia upya ratiba zao kipindi ambacho Obama atakuwa Dar kwani ni kama Tanzania/Dar itasimama!!
Source: CLOUDS FM
 
Wazir membe amesema wasiomtakia mema rais kikwete wananuna ujio wa obama hapa Mtanzania anaongea clouds fm asubuh hii.

Duh! Viongozi wa Tanzania ni vichekesho vitupu! Hivi waziri mzima unakaa kwenye vyombo vya habari na kuzungumzia mambo ya kuonewa wivu kisa Obama kutembelea Tanzania!!!???? Badala ya kuongelea maendeleo na kuondoa umasikini ambao hawajui ni kwa nini upo Tanzania, wanaongelea mipasho na taarabu kama kawaida!!

Membe! Tunataka habari za maendeleo na si mipasho ya eti raisi wenu anaonewa wivu kisa Obama. Wenzetu wana piga hatua za kimaendeleo nyie mnakaa na kutuletea siasa za vidole juu ambazo hazi saisii lolote!!!
 
Wakuu bado najiuliza concept ya obama kuwazuia wananch wasienda dar julai 1 na 2 kisa ujio wa Obama je anawatendea haki wananchi na je anapandisha au anashusha uchum?
 
Wamenuna watuna sana, sisi hatuna muda na kushugulikia eti uchumi, eti reli, kwanza tumemleta wa china, na sasa tunamleta Obama, usisahau kina Bush. na upande wa kinamama hatuko nyuma kuna Booooonge la mkutano, lazima wenzetu wanune sana kwa ujiko wa kimataifa tunaoupata.

- Kwanza nani kati yao nani amepanda mkokoteni wa kuvutwa na farasi? jibu ni hakuna watabaki kununa
- kati yao nani amepanda bembea? jibu ni hakuna watabaki kununa
- kati yao nani ametembelea nchi nyingi zenye nguvu? jibu ni hakuna watabaki kununa

sasa kuwakomesha tumlete kabisa na malkia Elizabeth hapo ndio watapasuka.

RELI, RELI na uchumi kitu gani mbele ya ujio wa Obama? amegoma kwenda kwao amekuja kwetu...

yamewashuka shuuuuuuu......
 
membe anapenda sifa sana na sidhani kama viongozi wa eac kama wataudhuria kwenye hicho kikao kwa sisi wakazi wa dar na ata wanajeshi wetu tunaonekana kama wakimbizi ndani ya nchi yetu trace ujio wa bush 2008.
 
Duh! Viongozi wa Tanzania ni vichekesho vitupu! Hivi waziri mzima unakaa kwenye vyombo vya habari na kuzungumzia mambo ya kuonewa wivu kisa Obama kutembelea Tanzania!!!???? Badala ya kuongelea maendeleo na kuondoa umasikini ambao hawajui ni kwa nini upo Tanzania, wanaongelea mipasho na taarabu kama kawaida!!

Membe! Tunataka habari za maendeleo na si mipasho ya eti raisi wenu anaonewa wivu kisa Obama. Wenzetu wana piga hatua za kimaendeleo nyie mnakaa na kutuletea siasa za vidole juu ambazo hazi saisii lolote!!!

ametumia muda mwingi sana kueleza vipi tutanufaika na ujio wa obama na watu wake,wewe umemsikiliza huyo aliemua kuchukua sentensi moja kati ya nyingi alizoongea membe kama ndio topic aliyokuwa anazungumza,dont you guys have sense of humour???
 
Tanzania has become a Western Countries lap-dog if my facts serve me right.This doesn't bode well with our neighbors
 
Wazir membe amesema wasiomtakia mema rais kikwete wananuna ujio wa obama hapa Mtanzania anaongea clouds fm asubuh hii.

Jana viongozi wa East Africa Kagame, Museveni na Uhuru Kenyata walikuwa na kikao nimeona kidogo BBC wakisema wamemtenga Kikwete hii imekaaje jamani, mbona uhusiano wa kikwete na marais jirani zake haujakaa vizuri? nimesikia Pia Rais wa Zambia na Marawi pia wanamponda wazi wazi Raisi wetu, what's is Wrong with Kikwete?
 
Bora niwahi kijijini nikajipumzishe kuliko kusubiri bugudha na kadhia inayokuja
 
Wakuu bado najiuliza concept ya obama kuwazuia wananch wasienda dar julai 1 na 2 kisa ujio wa Obama je anawatendea haki wananchi na je anapandisha au anashusha uchum?

Mheshimiwa waziri ( rais mtarajiwa) alishauri kwa kuepuka usumbufu sasa ukiona kama ushauri haufai, nenda wewe katikati ya jiji jumatatu na jumanne.
 
Wakuu bado najiuliza concept ya obama kuwazuia wananch wasienda dar julai 1 na 2 kisa ujio wa Obama je anawatendea haki wananchi na je anapandisha au anashusha uchum?

usipotoshe jamii.....amesema kama mtu anasafari ya dar na anaweza kuja baada ya siku tano bila kuathiri mambo yake aahirishe,maanake kama una mambo yako muhimu unaweza kuja tu ila tegemea usumbufu,hata nyinyi wa dar siku anakuja obama kama huna shughuli muhimu ni afadhali ubaki nje ya mji tu vinginevyo utasumbuka sana na mafoleni,ni ushauri tu hakuzuia mtu asije dar,tusipende kupotosha au kutwist kauli za watu.
 
Back
Top Bottom