mkaruka ataja rinu
JF-Expert Member
- Aug 27, 2016
- 3,309
- 2,218
Membe alifukuzwa kutoka CCM na si kwamba aliondoka kwa kupenda, unaposema unamkaribisha haileti mantiki, yeye akae huko huko alikoHuyu mzee wa kazi na bata ambaye alijitokeza kuchukua fomu kugombea Urais wa Tanzania ameonyesha dalili zote za kutokuwa na maandilizi na mikakati ya kutosha.
Tangu amezindua kampeni zake amekuwa anafanya mikutano yake ya kampeni mikoa ya Lindi na Mtwara na hakuna ratiba inayoonyesha atakuwa na mikutano nje ya mikoa hiyo.
Je, bwana Membe pumzi zimeshakata au anadhani yupo kwenye kampeni ya ubunge wa jimbo?
Wapinzani mnapaswa kujipanga kimkakati na kiuwezo. Au kuingia kwenye uchaguzi mkuu kuliendana na fungu la pesa kutoka nje?
Membe, nakukaribisha CCM hata kama ukitaka kurudi leo tutakupokea. Umechoka unahitaji kustaafu na kulea wajukuu huku ukishauri madiwani wa CCM kwenye wilaya yako nini maana ya uzalendo.