Membe Turufu Pekee Ya CCM Uchaguzi Mkuu 2015

Membe Turufu Pekee Ya CCM Uchaguzi Mkuu 2015

Ukana Shilungo

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2012
Posts
3,041
Reaction score
2,423
Wakuu heshima kwenu,

Baada ya kutafakari kwa kina,kutokana na CCM kuonekana hakuna mtu anayefaa kwa urais kadiri ya wanajamvi wengi,mimi leo nadiriki kusema Mh Benard Membe Ndio turufu pekee ambayo CCM wanaweza Kumtumia angalau chama kikauzika kwa kiasi kidogo,japo kuwa atakuwaa na kazi kubwa Mbele Ya DR SLAA endapo CHADEMA itamsimamisha.

Mgombea mwingine nje ya Membe ni kujitakia CCM Ishindwe kwa kishindo.

Nawasilisha.
 
Nadhani mtoa mada unafanya utafiti au umetumwa na membe mwenyewe..amekulipa kiasi gani kwa kazi hii?mnajisumbua kuandika eti huyu ana faa yule hafai..njia nyeupe kwa CDM 2015
 
Possibly mleta mada ndiye Membe mwenyewe;
Membe urais wa Tanzania siyo wa Kikwete family & co.
 
Dah.. Kaka Membe unapima hali ya hewa et? We ni familia ya kikwete na hatutaki kuirudisha familia ile madarakani. Kukuchagua wewe ni kwamba raisi kikwete atakuwa anaendelea kuitawala tena nchi kwa remote control ambayo ni wewe
 
Wakuu heshima kwenu,

Baada ya kutafakari kwa kina,kutokana na CCM kuonekana hakuna mtu anayefaa kwa urais kadiri ya wanajamvi wengi,mimi leo nadiriki kusema Mh Benard Membe Ndio turufu pekee ambayo CCM wanaweza Kumtumia angalau chama kikauzika kwa kiasi kidogo,japo kuwa atakuwaa na kazi kubwa Mbele Ya DR SLAA endapo CHADEMA itamsimamisha.

Mgombea mwingine nje ya Membe ni kujitakia CCM Ishindwe kwa kishindo.

Nawasilisha.

mtandao umeanza kufanya kazi naona busy kutafuta vijana waliotumia 2005 naona umeingia kwenye mtandao mkuu.mkumbushe akilala akiamka bado tunasubiri maadui 11.hivi membe na bro wake kunatofauti gani if i may ask mkuu?
 
Possibly mleta mada ndiye Membe mwenyewe;
Membe urais wa Tanzania siyo wa Kikwete family & co.

mkuu yaani jamaa anavyopiga jaramba na gea anayotumia kuwarubuni vijana kuingia kwenye camp yake ni kuwa yeye ndiyo presida coz amekuwa endorsed with outgoing presida.hofu yangu kakitika kutekeleza adhama yake basi kucha za watu zitajaa makontena
 
Ikitokea CCM wakamsimamisha Lowasa kama mgombea wa urais, then naweza kurudisha imani kidogo na hiki chama lakini si mgombea mwingine. Nani ana nafuu kumzidi tukiweka itikadi zetu za kichama pembeni? Kuna mmoja wa wana jf aliwahi kusema hata kama jamaa alikua fisadi then alikua anakula mwenyewe akimaanisha kwa utendaji kazi wake, watu wa chini yake waliwajibika kuliko ilivyo sasa. Ifike muda tutafakari jambo hili kwa umakini na sii kumpa tu mtu nchi kisa chama, tuangalie utendaji wake ukoje la sivyo maisha tuliyoishi ktk huu utawala uliopo yatazidi kuwa magumu kuliko tunavyodhania. Kwa hiyo wito wangu ni huu, bila kujali chama, tumpe nchi mtu mwenye uwezo wa kusimamia jambo au kuchukua maamuzi mazito kwa masrahi ya nchi. By the way, ile homework ya ziwa Nyasa kaimaliza au kafikia wapi? Lazima tupime mafanikio yake? Wizara yake imefanikiwa kwa kiasi gani toka apewe? Balozi zetu nje zina hali gani?

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Wakuu heshima kwenu,Baada ya kutafakari kwa kina,kutokana na CCM kuonekana hakuna mtu anayefaa kwa urais kadiri ya wanajamvi wengi,mimi leo nadiriki kusema Mh Benard Membe Ndio turufu pekee ambayo CCM wanaweza Kumtumia angalau chama kikauzika kwa kiasi kidogo,japo kuwa atakuwaa na kazi kubwa Mbele Ya DR SLAA endapo CHADEMA itamsimamisha. Mgombea mwingine nje ya Membe ni kujitakia CCM Ishindwe kwa kishindo. Nawasilisha.
Umejuaje kama dr Slaa ndiye atakayegombea 2015?
 
Membe hana kitu ushahidi ni wizara anayoongoza haina hadhi kama enzi za Mkapa, kuna kashfa kibao.
 
Huyu ni ndugu na Kikwete,huu uongozi sio wa kifamilia..actually ana udhaifu kama wa jk.Hata hivyo kuwa candidate wa magamba sina shida nae ila Ikulu mbele ya cdm uwanjani,atapigwa kipigo cha mbwa mwizi.
 
Atapata kura za riz, baba riz, mama riz/shem wake,lakn miraji wa jk atapiga kwa dr.Slaa, kwnn ni mzalendo wa kweli.
 
Nilitegemea mleta mada atatupa sifa za msingi za nani anafaa kuwa mgombea wa urais kupitia CCM kwa sasa, badala yake naona anatupa jina la mtu anayedhani yeye binafsi anafaa kuwa rais wa Tanzania!!!

Poor CCM!!!
 
Swali kuu, je ni nani atawateulia wanaCCM mgombea urais 2015?

*Jibu la swali hilo ndilo litakalotoa mgombea wa urais wa CCM 2015
 
Wakuu heshima kwenu,Baada ya kutafakari kwa kina,kutokana na CCM kuonekana hakuna mtu anayefaa kwa urais kadiri ya wanajamvi wengi,mimi leo nadiriki kusema Mh Benard Membe Ndio turufu pekee ambayo CCM wanaweza Kumtumia angalau chama kikauzika kwa kiasi kidogo,japo kuwa atakuwaa na kazi kubwa Mbele Ya DR SLAA endapo CHADEMA itamsimamisha. Mgombea mwingine nje ya Membe ni kujitakia CCM Ishindwe kwa kishindo. Nawasilisha.
mimi naona mwigulu, nape, wasira ama lusinde wanafaa kuwa raisi 2015
 
Ndugu Membe angeona jitihada zako angekutoa kidogo kitu cha Mpesa, ila nina wasiwasi kama anakufahamu keep it up tafakari zaidi umewahi muno kutueleza.
 
Tutashuru sana CCM wakimpitisha! Membe ni muungwana na ikiwa ameshindwa yeye atakubali kirahisi matokeo kuliko EDO japokuwa endo anahistoria ya kuachia ulaji kirahi kama alivyo utema U-PM!...
 
Back
Top Bottom