Benard Membe unayo maswali ambayo Watanzania watahitaji majibu yake kutoka kwako kama unayo dhamira ya kugombea Uraisi ,
1,Ukiwa ni Waziri wa mambo ya nje umeshirikiana na serikali yako kuwadanganya Watanzania kwamba BALALI amekufa na kwenye maombolezo yzke watu wameingia kwa kadi na kuweka rekodi kama si kote duniani kwenye maombolezo watu kuingia na kadi kana kwamba ni sherehe,wakati wanaoingia ni viongozi tu hata ndugu wa marehemu wengine hawakuruhusiwa kuingia,kitu ambacho hata mazishi ya muasisi wa taifa hili haikufanyika hivyo
2, Yule ni kiongozi mwandamizi serikalini [Gavana] kumzika nje ya nchi ilikuwa ni kuficha nini? Na kwanini azikwe nje ya nchi wakati ana kwao na Serikali inaouwezo wa kumrejesha na akazikwa hapa kwao? Serikali ilikuwa inaficha nini?
3,Ulisema unawafahamu walioficha fedha za Tanzania Uswiss kwa majina na kwamba utawataja,mbona hadi leo haujawataja? Unataka tukupe nchi ya Tanzania si utatuuza wote?
4,Ni vipi umelishughulikia suala la mpaka wa Tanzania na Malawi na ni nini hitimisho lake? Wananchi hawajui liko katika hatua gani linatakiwa majibu
Kwa maoni yangu hata kama utajibu hayo maswali wewe ni dhaifu kama kiongozi unaetaka kumrithi haufai kuwa Raisi wa Tanzania kabisa sababu si MUWAZI hatutaki kiongozi wa aina yako hali tuliyonayo tayari tuko ICU halafu tupate tena rais muoga HAUTUFAI