Membe: Magufuli asiwaendee pupa wafanyabiashara

Membe: Magufuli asiwaendee pupa wafanyabiashara

Aliyekuwa waziri wa Mambo ya nje Mh.Membe ameonya kuwa wafanyabiashara wasiendewe kwa pupa.Ametanguliza kuwa anaunga mkono mikakati ya ukusanyaji kodi lakini isiwe katika hali ya kukatisha tamaa na kudidimiza uchumi.Membe ameonya hayo kufuatia malalamiko ya wafanyabiashara kulalamika kuwa baadhi ya mikakati inaelekea kuwadidimiza.Haya yameandikwa katika magazeti ya leo
Suluhisho ni kubadilisha sheria za kodi kila mtu alipe kodi inayostahili na inayolipika, sheria ya kuruhusu afisa wa kodi akadirie anayoona inafaa ndio inawalazimisha wafanyabiashara watoe rushwa kwa hawa maafisa wanakupiga kodi ya juu makusudi, ijulikane kama in kontena la matairi na limenunuliwa kwa sh.100 kodo ni asilimia ngapi na kama ni gari imenunuliwa kwa sh50 kodi ni asilimia ngapi kwa sasa unaagiza gari wanakupigia hesabu ya kodi,ukileta bandarini kodi inapanda hii si sawa, Apeleke mswaada wa sheria ya kodi bungeni ibadilishwe, hii iliwekwa ili watu wapige pesa na kuwapendelea watu wachache, na wafanya biashara waache kujipendekeza kwa cccmmm, wasimamie na sheria zitakazowezesha kufanya biashara kwa uhuru sio kutegemea kubebwa na wanasiasa.
 
Mungu mkubwa amembadilisha Membe kutoka ufirauri hadi kuwa kondoo mwema, umeamua kuungana Na mamilion ya watanzania kwa ajili ya Tanzania mpya, tupo nawe
 
Ben Maembe amepanikiiii,anawayawaya kisha amekosa nafasi katika Serikali ya awamu ya 5.Watajibeba mwaka huuu ni Opetation tumbua majipu.
 
Membe Membe !!!@@@ tulia baba nchi tumempa mwingine. Kama unataka kufanya biashara fuata utaratibu wa nchi hii na kama unataka kwenda nchi nyingine pia huzuiwi, wewe unajua nchi nyingi dunia hii so chagua moja ukamalizie umri huko, mtaji unao watu waliona zile dola za marehemu . Na uache mkuu wa nchi afanye marekebisho japo kidogo. Nchi inaendeshwa na Rais si wafanya biashara. Hapa sio Columbia
 
Bora wajumbe wa team Lowasa walichomfanyia,maana huyu angekuwa Raisi hii nchi ingekuwa ni shamba la wasioona na siyo la bibi tena

Kumbe unatambua uwepo wa Lowasa huwa unajitoa ufahamu tu
 
Support huyu Membe ni tajiri wa kutupa. Lazima atetee maslahi yake. Mungu epusha shetani angekuwa Rais. Vyote vibovu lkn angalau JPM ana nia ya dhati moyoni
 
Membe shushushu mstaafu...ametumwa na nani toka idarani kuja kumkosoa Rais? Au kuna sehemu ameguswa?
 
Yaani kwanamna nyingine tunaweza kusema,kuwa Dr.Magufuli apunguze kukurupuka.
Wewe ni lofa kabisa! Unataka wafanyabiashara wasilipe kodi? Huyu Bw Membe si vema akakaa kimya tu. Yeye anafurahia mabilioni kutapanywa kwenye mahoteli kwa shughuli zisizo na tija??
 
huyo ndio alitaka kuwa rais wetu mungu atuepushe na huyu shetani , aliyelaaniwa
Tena shetani mbaya sana huyu jamaa...maana naona kama amekuwa mpinzani wa juhudi za rais...atakuwa shetani wa mguu mmoja
 
Huyu mzee mstaafu si atulize boli lakini?
Mbona kutwa kigulu na njia kwenye media kumkosoa prezda? Anakera sana!
 
Back
Top Bottom