Membe kuwania urais 2015...

membe HANA SIFA!
unajua huyu wa sasa hivi kilichompa boost ni kwamba ANATIZAMIKA!he is presentable!lakini nae HANA SIFA,na hakuna kitu cha msingi sana ambacho watanzania wanajivunia kutoka kwake kabla hajawa rais!alibebwa na performance nzuri SUPERFICIALLY ya serikali ya ccm ya 'ukweli na uwazi'

lakini membe HATIZAMIKI KABISA!na yupo kwenye wakati mgumu sana,sababu yupo kwenye system wakati watu wameshaamka kifikra!na uovu wa 'ukweli na uwazi' unajidisplay sasa hivi

ccm WILL LOOSE KILA KITU
 
Siyo 2010 na wewe ni 2015. Si dhambi, ila

1. Anajionyesha "amateur" katika game.

how? naomba unifafanulie zaidi

2. Ana sink lower than Ally Karume na Hussein Mwinyi.

kwa vipi?

3. Anajianika wide open kwa mashambuklizi unnecessarily early.

Isnt that a price kila mwanasiasa ana pay kwakuwa ulingoni?

4. Anajionyesha kwamba hayuko focused kwenye kazi yake ya sasa na anaitumia tu kama stepping stone to Ikulu.

kutokuwa focused nadhani nako kunahitaji maelezo zaidi, kwa sababu kama kuna matatizo kwenye wizara yake au department kwenye wizara yake si vibaya tukafahamishana ni yepi
5. A myriad of reasons not to declare early.
its never too late though muda bado unao
 
Masatu,
Tulia tu upewe mashambulizi. Huna muda wa nini? Heee, si unataka kila habari ushinde, sasa umekutana na jamaa mvumilivu kama Mudhihr. Yeye yupo polepole tu wala hana haraka. Anakupa tu page na radio wapi ukasome, na ukirudi kumjibu, anakupa nyingine. Vumilia tu, kushinda kuko karibu YEGO!!!

Hayo mambo ya kila habari nishinde ni ya kwako. Sipo hapa kushindana kama ww upo kwenye hilo kila la kheri.

Ndio sina muda wa kupitia hizo reference zake yeye aliezipitia na kusikiliza si aseme kuna nini badala ya kusema tu "nenda kasome" nenda kasikilize" dana dana tupu hamna kitu humo.
 
Membe amekuwa akilazimisha umaarufu na kujifanya ni senior minister wakati kuna kina Malmo na kadhalika.

Masatu.
Usiwe na hasira tunaelekeza na kupeana reference.

Sina hasira na sina sababu ya kuwa na hasira. Ushauri wangu kwako ni hizo refererence unazotaka nizipitie au kusikiliza tuambie zinasema nini kwanza badala ya kurusha rusha tu.
 
"Bila shaka, bila shaka" in the context of the question hapo unaielewaje? Bila shaka nini?

Au unataka mpaka aweke sahihi azimio la kugombea urais 2015 live on national TV ndiyo ukubali?

Hakutumia fursa hii kukanusha habari hizi za kugombea urais na mpaka leo baada ya habari hizi kuchapishwa hajakanusha.

He is either dumb or cocky, and neither of the two are presidential, forget about statesmanlike.

come to think of it, he may very well be dumb and cocky, a dangerous combination.

"Bila shaka" kwanini iwe kugombea urais na isiwe kauli inayo tokana na msukumo wa maadui zake?
 
Wakuu ebu tuzungumze facts na sio kusema maneno yasiyo na maana hata kidogo..
Kwanza Mudhihir anasema Membe alikuwa mtandao -Sawa yeye alikuwa kundi gani kama sii mtandao. Mudhihir yuko kundi moja na Kikwete toka Jk akigombea uongozi na kajikata mwenyewe kuingia upande wa kina Lowassa na Rostam hiyo inajulikana (kumbukeni aliaondolewa madaraka kwa sababu zipi!)..

Yawezekana wengi mnaozungumza hapa hamfahamu kwamba huyu Mudhihir, pesa mbele ya kila kitu.. Sasa mkweli kati ya hawa wawili nani na mnafiki yupi kama sii yule anayetanguliza kulaumu pindi mambo yakigeuka wakati alikuwa mshabiki mkubwa wa uatawala wa Kikwete..Wamevurugana basi imekuwa fitna na kuvuana nguo wakati wote hawa wanaoga ktk maji machafu ya CCM.

Membe anaweza kutokuwa rais mzuri wala hafai kuchaguliwa kama mnavyodai, lakini hili sio swala la uteuzi wa kina nani watasimama kugombea urais kwa kiti cha CCM..sii kazi ya Mudhihir wala sisi hapa ni mpango wa chama na wahusika wake...Mudhihir kama ana nyodo amsubiri Membe akiwakilisha form yake kisha apige kura ya hapana (kupinga)..Jukumu ni la wajumbe wa chama CCM nani atasimama mwaka 2015 kwa tiketi ya chama, lakini majina ya watu wanaowania kugombea yanaweza kuwa hata 100. Mwkaa 2005 wamejitokeza majina mangapi wengine hata sikumbuki majina yao lakini leo kusikia jina la Membe imekuwa big deal..

Kitu kimoja tu ambacho nashuikuru sana Mungu kanijaalia ni kumbukumbu.. na mwepesi sana wa kuunganisha visa mikasa na fitna za kibgongo.. Kwa hili nitawakumbusha vizuri sana tulipotoka na mkisoma haya maandishi ya Mwanakijiji mwaka mzima ulopita mtaweza kuelewa kinachoendelea..
Nakuombeni someni mpangilio wa hoja ktk mada aloanzisha Mwanakijiji June 12, 2008 kisha tazameni tumefika hatua gani..
Bofya hapa
 
Last edited:
Well, nadhani jibu zuri angejibu mtoa mada hii!..

Usimusingizie mtoa mada hii. Hakuna mahali popote alipotoa madai ya ukristo na uislamu. alichoweka cha kwake ni swali 'Je kwani ni lazima waziri wa mambo ya nje awe raisi?'
 
jamani tuacheni kupotosha Uma, Nilimsikiliza sana Membe na kusoma magazeti ya mwananchi na mengine hakuna hata kipengere kimoja ambacho Membe alikiri kuwa ana nia ya kugombea urais licha tu ya kukiri kuwa anaamini Mudhihir anatumiwa na wabaya wake kisiasa kumchafua kwani Mudhihir anayemfahamu yeye asingeweza kusema hayo.
Naomba hii Jamii Forum itumike kuelimisha jamii na sio kuipotosha au kusema uongo itakosa maana kabisa ka ze utamu
 
Hajulikani kama ni Muislaam au Mkristu!

Membe ni mkritu mkatoliki na anavaa msalaba wa dhahabu kama Mkapa,sasa sijui kuvaa mkufu wa dhahabu kama Mkapa ndio maandalizi ya urais au laa. kwani amekuwa kama zezeta kila jambo alilofanya aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya nje na akawa rais yeye akafuata.

Membe ameshirikiana na maaskofu kuandaa maandamano kupinga OIC halafu akamzunguuka JK kuwa hili suala lina presha kubwa bora tuliache kwanza, wakati yeye ndiye aliye injinia.huu ndio unafiki wa Membe. sio mkweli unavyomuona ni tofauti na alivyo. bora rais awe Magufuri sio huyu Mnafiki
 
jamani tuacheni kupotosha Uma, Nilimsikiliza sana Membe na kusoma magazeti ya mwananchi na mengine hakuna hata kipengere kimoja ambacho Membe alikiri kuwa ana nia ya kugombea urais licha tu ya kukiri kuwa anaamini Mudhihir anatumiwa na wabaya wake kisiasa kumchafua kwani Mudhihir anayemfahamu yeye asingeweza kusema hayo.
Naomba hii Jamii Forum itumike kuelimisha jamii na sio kuipotosha au kusema uongo itakosa maana kabisa ka ze utamu
Membe ni member hapa JF mwache ajibu mwenyewe kwa jina lake la Mbopo.
 
Last edited:
In fact mtu kama membe hafai hata kidogo kushika hata nafasi alinayo kwa sasa! maana anaonekana kuwa mtu wa visasi ,hasira, chuki na kibaya zaidi yupo tayari kutumia njia yoyote iwe halali au haramu kufanikisha malengo yake. nasema tena Membe hafai
 
Hii habari wala haikukaa sawa zaidi ya kuzungumzia maudhi ya Mudhihir..Kinachonishinda kuelewa ni kwamba Membe pia ni Mbunge wa Mtema huko Lindi iweje awe mtu asiyependa maendeleo ya Lindi?..Hicho kiwanda cha saruji ambacho wanadai Membe anakiwekea ngumu, tuambiwe sababu basi! na kinajengwa na nani na kwa kibali gani hata Membe aweze kuzuia uwekezaji huo..

Ni vizuri tukipata story nzima ya hicho kiwanda ya yanayohusika maanake tunaweza kusema Zitto alikuwa na roho mbaya nyoka mbaya sana tena Koboko! kwa kuzuia mkataba wa Buzwagi.. Wapo kina Adam Malima waliounga mkono na kudai kama Karamagi anaweza kuwaletea wawekezaji kwao afanye kama alivyofanya atapokelewa..Lakini tulipokuja ufahamu ukweli kila mmoja wetu alikubaliana na Zitto..Leo hii huyo Karamagi yuko wapi!.. hivyo Mudhihir pia atuambie huu mkataba wa kiwanda cha sarujji unahusu shirika gani na kwa nini Membe kauzuia hali unajengwa ktk mkoa wake mwenyewe.. Huo Ubinafsi kwani Membe anajenga kiwanda hicho nyumbani kwake?.. Au ubinafsi una maana mbili tofauti!
Kwa hiyo msitegemee sisi wote hapa JF tunawez kuamini yote yanayozungumzwa kwa vishoka maanake habari nzima inajaa FITNA..

Huyo Membe anasifiwa kwa Ukatoliki wake kisha huyo huyo anaelezewa kukubali Tanzania kujiunga na OIC pamoja na Mahakama ya kadhi pia kupata mjisaada toka Arabuni.. Hizi ni chuki kubwa za watu binafsi ambao wanataka kutumia wao dioni kama kigezo cha kuifikisha hoja yao lakini wanadunda..Kwani toka lini bungeni mbunge hukatazwa kutoa maoni yake, akikubaliana na waislaam basi kisha kuwa puppet!..Hee kisha mnadai sisi wote ni Watanzania hali mkitumia maneno ya wakristu wana msimamo mkali kwani nani kasema hamna msimamo ikiwa mtakubaliana na Membe au wazo la OIC..hamuoni nje zaidi ya mipaka ya kanisa utafikiri Ma Ayatollah wa kiafrika.

Kwa mwenye uwezo mzuri wa kufikiri atajua fika mada hii haihusiani na swala la Membe kugombea Urais mwaka 2015 bali ni kuhakikisha fikra zake za kugombea zinapigwa vita..Hizi ni fikra tu kila mtu anaweza kufikiria kugombea na sii kazi ya gazeti wala Mudhihir kuchambua uwezo wa Membe..Yeye huyo Mudhihir tumesikia mangapi?.. hadi watu walisema ajali yake imetokana na kulaaniwa, na aliponea chupuchjupu.... iwe leo Membe kuwa Nyoka!..Basi nasi tutaamini kwamba Mudhihir kweli alilaaniwa kweli maanake kuna mengi alofanya wala hayafurahishi..Kaingia uwaziri wala hakukaa kaingia Ufisadi, Kikwete mshikaji ewenyewe kamtolea nje basi imekuwa Membe ndiye mfitini...Tunajua fika, where Mudhihir anajaribu kuficha ukweli.. gubu limemjaa kuona alipigwa chini bila kutegemea..
Jamani upuuzi huu utakwisha lini..Basi yaonyesha hata kuchaguliwa kwa Asha Rose Migoio UN ni mbinu za Membe ili apate kushika Uwaziri..

Watasema sana lakini sisi wengine tunajua kwamba Membe hakupelekwa nje kwa sabnabu yeye ndiye Mbinafsi..Hapana huyu alikuwa shushushu ambaye alionekana kuwa hatari kwa Mafisadi.. na Mkapa ahakumpenda wala wale shemeji zake waliokuwa Mabalozi Canada hawakumpenda.. Sisi tuliokuwepo hapa tunayajua haya na tumeyaona kwa macho yetu visa na vitimbi alivyokuwa akifanyiwa lakini pamoja na yote hayo Membe alikuwa karibu sana na Watanzania..Naweza kusema hakuna muda au wakati Ubalozi wa canada umekuwa karibu na wananchi wake kama wakati wa Membe, Aziz na mama Chipungahelo.. hawa ni watu ambao wakazi wa Canada kamwe hawatawasahau..Sasa fikirieni tu haya yamekuwa ugenini huyu mtu anaweza kufanya mangapi akiwa ndani Tanzania nchi yake mwenyewe..

Yes Membe anaweza kuwa na mapungufu yake kama kiongozi. Ni utawala wa kiafrika ambao hatutegemei pepo lakini siku kwa siku tunapokuwa nam mtu mwenye moyo na ukaribu na watu haasa ktk madaraka basi bila shaka sisi wananchi ndio waamuzi wa haki na sio hawa wabunge ambao ugonvi baina yao ktk meza kuu na hawajui kinachoendelea ktk maisha ya walalahoi..
I'm for Membe....


Kama kuna Mzandiki kati ya Membe na Mdhihiri basi ni Mdhihiri!! Jamaa ni mtu asiyejiamini!! Nakumbuka nilipomaliza chuo nilienda kwa Mdhihiri wakati akiwa ni waziri wa kazi. Nilienda pale kwa ajili ya kofia zake mbili, Ni mbunge wangu ( Mchinga) na alikuwa ni waziri wa kazi. Bahati mbaya jina langu la ukoo inaelekea alishawahi kulisikia. Basi ile nagusa ofisi yake tu, mazungumzo yetu yalikuwa hivi:
Mdhihiri: Unataka ni kijana?
NasDaz: Mheshimiwa mimi naitwa......!
Mdhihiri: Sema Unataka ?
In short hakutaka hata nijitambulishe!!!!
Hata pale nilimweleza shida yangu kama angeweza kunisaidia kwa namna yoyote, majibu yake yalikuwa : " Sikiliza wewe kijana, nani kakuambia ofisi hii ina kazi ya kuwatafutia kazi watu? Mimi mwenyewe mwanangu kasoma India kaja hapa hamna kazi nimempeleka Uganda kusoma!! Kuna mwanangu mwingine ameamua kuwa mkurugenzi wa Mchinga Sound! hamna kazi hapa....!" Akabwabwaja sana!!
Nikajiuliza sijui mambo ya wanawe mimi yananihusu nini!!! Anyway, inawezekana sikuwa na sababu za kwenda kuomba msaada kama huo lakini nilitarajia basi angalau angenijibu kiungwana!! Ajabu, pale tulienda watu wawili. Yule mwenzangu aliongea nae kwa zaidi ya nusu saa wakati mimi sikutumia hata dakika tatu, akanitoa baru!!! Niliporudi home na kumsimulia uncle wangu, akaniambia hakutaka tu kuniambia kwavile ingekuwa kama ananikatisha tamaa na kwamba alijua hatatoa ushirikiano!!! Nilipomuuliza ni kwanini akasema kwamba mdhiri ana bifu na watu wa bush kwangu kwavile wa2 wa bush kwetu chaguo lao lilikuwa ni Merehemu Mama wa Tondoa!!! Aidha, alikuwa na wasiwasi na huyu uncle wangu kwamba anataka ubunge wa Mchinga kv alikuwa na tabia za kutaka kuwasaidia wa2 pale bush!! Akawa na bifu nae wakati uncle na siasa ni vi2 viwili tofauti!!! Kwahiyo, ni mtu ambae hana confidence!! Asikuambie mtu, wenyewe watu wa Lindi tunajua Membe ni nani kuliko huyo Mdhiri na si kwa sababu ni minister!!!

Tukija kwenye hoja ya kiwanda, hata kama kweli Membe alitaka kukitoa kiwnda Mchinga basi alikuwa right kwavile am sure alitaka kiwe Lindi Mjini. Mji wa Lindi wa Lindi unakufa kifo cha kawaida kwahiyo vinahitajika vitu vitakavyosaidia mji huu, na viwanda ndio vitu muhimu. Likewise, ikiwa Wabongo hata hapo Lindi Town hawataki kwenda je, mchinga? Naamini hata kama ni kweli basi Membe alitumia busara badala ya kuangalia siasa!!
 
Kama kuna Mzandiki kati ya Membe na Mdhihiri basi ni Mdhihiri!! Jamaa ni mtu asiyejiamini!! Nakumbuka nilipomaliza chuo nilienda kwa Mdhihiri wakati akiwa ni waziri wa kazi. Nilienda pale kwa ajili ya kofia zake mbili, Ni mbunge wangu ( Mchinga) na alikuwa ni waziri wa kazi. Bahati mbaya jina langu la ukoo inaelekea alishawahi kulisikia. Basi ile nagusa ofisi yake tu, mazungumzo yetu yalikuwa hivi:
Mdhihiri: Unataka ni kijana?
NasDaz: Mheshimiwa mimi naitwa......!
Mdhihiri: Sema Unataka ?
In short hakutaka hata nijitambulishe!!!!
Hata pale nilimweleza shida yangu kama angeweza kunisaidia kwa namna yoyote, majibu yake yalikuwa : " Sikiliza wewe kijana, nani kakuambia ofisi hii ina kazi ya kuwatafutia kazi watu? Mimi mwenyewe mwanangu kasoma India kaja hapa hamna kazi nimempeleka Uganda kusoma!! Kuna mwanangu mwingine ameamua kuwa mkurugenzi wa Mchinga Sound! hamna kazi hapa....!" Akabwabwaja sana!!
Nikajiuliza sijui mambo ya wanawe mimi yananihusu nini!!! Anyway, inawezekana sikuwa na sababu za kwenda kuomba msaada kama huo lakini nilitarajia basi angalau angenijibu kiungwana!! Ajabu, pale tulienda watu wawili. Yule mwenzangu aliongea nae kwa zaidi ya nusu saa wakati mimi sikutumia hata dakika tatu, akanitoa baru!!! Niliporudi home na kumsimulia uncle wangu, akaniambia hakutaka tu kuniambia kwavile ingekuwa kama ananikatisha tamaa na kwamba alijua hatatoa ushirikiano!!! Nilipomuuliza ni kwanini akasema kwamba mdhiri ana bifu na watu wa bush kwangu kwavile wa2 wa bush kwetu chaguo lao lilikuwa ni Merehemu Mama wa Tondoa!!! Aidha, alikuwa na wasiwasi na huyu uncle wangu kwamba anataka ubunge wa Mchinga kv alikuwa na tabia za kutaka kuwasaidia wa2 pale bush!! Akawa na bifu nae wakati uncle na siasa ni vi2 viwili tofauti!!! Kwahiyo, ni mtu ambae hana confidence!! Asikuambie mtu, wenyewe watu wa Lindi tunajua Membe ni nani kuliko huyo Mdhiri na si kwa sababu ni minister!!!

Tukija kwenye hoja ya kiwanda, hata kama kweli Membe alitaka kukitoa kiwnda Mchinga basi alikuwa right kwavile am sure alitaka kiwe Lindi Mjini. Mji wa Lindi wa Lindi unakufa kifo cha kawaida kwahiyo vinahitajika vitu vitakavyosaidia mji huu, na viwanda ndio vitu muhimu. Likewise, ikiwa Wabongo hata hapo Lindi Town hawataki kwenda je, mchinga? Naamini hata kama ni kweli basi Membe alitumia busara badala ya kuangalia siasa!!

Wizara ya kazi haihusiki na kutoa ajira,ulitakiwa usome magazeti na uombe kazi, pia ulitaka akupe kazi kwa kujuana? naona kama imeandikwa na Membe kwani anajulikana kwa fitna za magazeti na mitandao.

Mudhihir alikuwa ana kazi nyingi kama alikupa dakika tatu mshukuru kwani ulikuwa huna appointment nae na pia unapoteza muda wa Taifa kwa kutaka upewe kazi kwa kujuana au kiukabila KUMBUKA HAKUWA WAZIRI WA WATU WA MCHINGA AU LINDI,jee kwani ulipokwenda kwa Membe alikupa kazi kwa kigezo cha kujuana?

Mtoto wa Mudhihir aliamua kujiajiri na sio kutaka ajiriwe kwa jina la baba yake kama tunavyolia na watoto wa vigogo BOT.
 
Back
Top Bottom