joseph1989
JF-Expert Member
- May 4, 2014
- 15,194
- 31,834
Kuna watu waliwaponda wakakodi mpaka Chopa kukagua vyanzo vya umeme, walikuwa na mbwembwe matokeo yake wameharibu mazuri waliyo ya fanya wenzao.Ukweli usemwe:
Enzi za uongozi wa Medard Kalemani na Tito Mwinuka kukatika kwa umeme ilikuwa ni nadra sana, ma meneja wa TANESCO wa mikoa na wilaya walikuwa matumbo joto.
Kitengo cha emergency kilifanya kazi mchana kutwa, usiku kucha, huko vijijini speed ya kuwasha umeme kwenye miradi ya REA haikuwa ya kawaida.
Kila aliye ingia kwenye 18 za waziri Kalemani alikwenda na maji.
Mheshimiwa Rais warudishe hawa watu na uwape uhuru wapige show kabambe tule maisha.
Hivi vitu ndo vinatugusa moja kwamoja. Tunamkumbuka sana JPM huu ni ukweli mheshimiwa. Umeanza kutuchosha.
Mwaka jana mikataba ya mabilioni ya shillingi,mama nae bila hiyana kawapa ila hamna walichofanya.