Mdogo wangu kanisaliti

Broo....pole sana....so kwa sasa na mimba unalea....duh una roho ya chuma mangi!!! Aende kwao kaka,,,mengine yatafuata, watoto usiwadhulumu, wawe huru kuwa na mama yao au wewe......hakikisha watoto hawaathiriki na hili.
Ni gumu mno, aidha hama wewe, kama ni nyuma mmejenga wote, ili watoto wawe salama na uhakikishe wanapata mahitaji yote....pole kaka......wanawake hawa.....Mungu tusaidie.....
 
Huyo mwanamke muache tu akaishi na aliyempa mimba, hakuna sababu ya kuendelea nae, hautokuwa na amani ya moyo tena hata iweje kila unapomuona huyo mtoto, hakuna namna kama umliweza kufukuza mdogo wenu basi ni ahisi pia kumfukuza huyo malaya mkubwa, hivi vitu vinauma sn
 
Mlaumu aliyeleta Tasnia ya NDOA...ndio kaleta majanga yote..hit n' run mpango mzima(kumegewa ni Siri ya ndani)aliimba rich mavoko mababu wakakasirika wakambania tuzo za Kilimanjaro
 
nashangaa kuwa hujanielewa aisee. You are better than that, i am sure!
Hakuna dini yeyote duniani au kitabu cha dini yeyote duniani kinachotangaza, oeni "mmoja tu" isipokuwa Qur'an. Jee unalijuwa hilo?

Usilolijuwa ni usiku wa kiza.
 
mie nimeshamalizana nae. siwezi kubakia kwenye ukristo kwa kwa sababu ya kuogopa uke wenza. for the same reason sioni kama kigezo kimoja tu kinatosha kunisaidia maamuzi ya kupata mwenza say kwa sababu mwanaume ni mkristo tu ndo niamue kuolewa nae. hapo ni akili ama matope?
King'asti na Faiza sidhani kama mnakoelekea mtamaliza. BTW Hivi kubadili dini ndo suluhisho eenh! Hizi dini zisitufanye tushindwe kutumia common sense Kha!
Kila kitu dini dini waliotuletea wenyewe wanaendelea ila sisi zinatuwehusha.
 
Samehe saba mara sabini maana yametokea tayari pia wakati unafanya fumanizi ni wazi ulijua kamwe ndgyo hawezi kukusaliti

Sio kwa dhambi kama hii ya usaliti.. mimi namshauri apige chini maana hawa wanawake hua wanakua wajinga sana ilishawahi kunitokea hii na X GF wangu,allitembea na mshikaji wangu wa karibu sana sasa baada ya kuweka mitego yangu nikamnasa tena alikua ni mjinga sana huyo binti nilimweka mtego kidogo tu akanasa, ilikua hivi kuna siku niligombana na huyo mshikaji tena ilikua Bar, na nilikua na hasira sana hata GF wangu aliponipigia simu alihisi nina mabadiliko sana kwa sababu always hua nakua cool, akaniuliza mbona unaongea hivyo na unaonekana una hasira? nikamwambia nimezinguana na mshikaji JAMAL(sio jina lake).. akauliza ilikuawaje nikamwambia akajifanya anamtetea sana mimi nikamwambia achana nae mjinga tu.. kwanza mtu mwenyewe ana UKIMWI" kusikia hivyo Demu akachanganyikiwa.. akaanza kubabaika sana akauliza mara tatu eti unasema JAMMALI ana UKIMWI? nikamwambia ndio? mamamaa nimekufa nikamuuliza una maana gani?? akasema nilitembea nae.. (Nakatisha) baada ya muda tukayaongea yakaisha nikarudiana nae yule binti lakini akaja tena akkarudia kwa jamaa mwingine na nilifuatilia nikabaini ilikua kweli.. akalia sana nikamwambia nipe muda wa kufanya maamuzi.... wakati nipo kwenye kutafakari maamuzi akaja akafanya tena blunder nyingine... nilichafanya sijaongea nae tena akipiga simu sipokei, wala FB sijibu SMS zake na nimeamua ku Block kabisa.. anapiga simu na anabadilisha namba, anaandika sms hata 30 kwa siku lakini sijibu neno.. yeyey mwenyewe ameamua kusepa...
nakushauri mkuu Lee2 achana nae huyo, lea wanao kuendelea nae ni aibu na dharau kubwa sana
 
Last edited by a moderator:
huu ni utani sasa....yani mkeo kalala na ndugu yako na amempa mimba bado unauliza kuendelea kuishi naye??
hamna mtu hapo mpe TALAKA TU HUYO,,huwa ninaamini kama kaamua kulala hata na mdogo wako manake sio mara yake ya kwanza hiyo hata huko nyuma kwa mmoja wa maex alishalala na mmoja wa ndugu zake hao x,,sema arobaini yake ilifikia kwako ukitoa huku nyuma...POLE SANA uzinzi una mipaka sio kutembea na ndugu yangu angekuwa mtu baki unafunika kombe mwanaharamu apite
 
Msiachane isipokuwa kwa zinaa tu,apo unasubiri nini nae kakiri??
 
Pole sana, usitoe ujauzito kubali matokeo.

Ila dogo nae amekosea sana wanawake wote waliopo hakuwaona hadi ifikie hatua ya kuwa na mkeo?!

Kwa kweli dogo amekosea sana
 
Hilo jamaa ni yabo kabisa,fukuza jini hilo.
 
Me ntamuwinda mpaka nimbake nione kama hutamfukuza coz tunakubembeleza sana umfukuze hulifukuzi shyn.
 
mke wako ni mwanamme au mwanamke?
 

Sasa mie nakuelewesha!Kitu pekee ulichowasaidia wazazi wako ni kumuacha kijana wao hai baaaasi!Huyo hawezi kuwa mkeo!Hakuna mila ya namna hiyo siku hizi hata umasaini!
 
Huyo malaya muachie mdogo wako tu mkuu uzuri hukuzaa naye
 
Naam
 
Ukisikia pambana na Hali Yako ndio kama hivyo, aliyekusaliti sio mdogo wako ni mkeo, huyo mwanamke piga chini haraka sana hata huko Kwa ndugu mlienda kujichoresha tu, maamuzi ungeyafanya mapema wewe mwenyewe , hivi mwanamke akusaliti na mimba juu halafu uweke kikao Cha familia??
 
Pole sana mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…