Mh Naibu Speaker kajitangazia ushindi mnono wa hiyoo kesho! alijitangazia ushindi huo leo asbh wakati wa kutoa matangazo ndani ya mjengo.
Ilivyoonekana alikuwa na hofu khs mdahalo huo.
aliwaomba walipukaji wenzie wawepo kesho ndani ya mdahalo kumpa support kiaina wakati akitangaza mjengoni!, alionyesha hofu kubwaaa..!!!
huyo Bibie Mwendesha mdahalo inavyoonyesha ana usongo na walipukaji....., habari za chini ya jamvi nackia alikuwa ameajiriwa na Habari Corporations ya Rostam Aziz.
Baadae Mh Rostam akampiga chini kiaina! so still ana usongo na walipukaji mjengoni!
Muhimu 2waombe TANESCO chini ya Mh Ngeleja wasijeficha aibu kwao kwa kuuchukua Umeme wao!
Kama ndungai ni mwanasheria mahiri na makini, na ametulia nina shaka na waliobaki..Mimi kwa upatu wangu naona utakuwa mdahalo mzuri sana kama Lissu atapunguza jazba na kuzungumza vizuri kwani Ndugani ni mwanasheria mahiri sana na mtulivu sana katika kupambana na hoja.
Nazidi kusisitiza kuwa LISSU apunguze jazba ili mjadala uwe mzuri kwa faida ya wachangiaji na watanzania wote kijumla .
nawatakia mafaniio mema.
Huo mdahalo sidhani kama utatokea, lazima Ndugai ataingia mitini. Ila kama ikitokea unafanyika muulizeni Ndugai kuhusu kutelekeza mkewe wa ndoa na kumuacha anauza machungwaWaiting for this moment to come and see degrees of arguments and issues presentation , ila am sensing power blackout hiyo kesho ikifika!
OPTION,mdahalo urushwe kwnye redio pia,kwani endapo umeme utakatwa itakuwa easy kusikiliza mdahalo kupitia simu.
Lissu amtolee uvivu huyu Naibu Spika na amuulize kama macho yake yana uwezo wa kuuona upande mmoja tu yaani upande wa CHADEMA & NCCR- Mageuzi.
Je, Ndugai ana ubavu wa kushindana hoja na Tundu Lissu? Hapa naona mlima na kichuguu.
<br />..namshauri Tundu Lissu ajiandae vyema kwa ajili ya mdahalo huo.<br />
<br />
..Ndugai si mtu wa kumdharau ukizingatia kwamba alimdhibiti Freeman Mbowe ktk mahojiano waliyofanya pamoja.<br />
<br />
..katika mdahalo wake na Mbowe, Job Ndugai alifanikiwa kujenga taswira kwamba wabunge wa CDM ni watu wasiojua sheria na taratibu za bunge, pamoja wajibu wao kama wawakilishi wa wananchi. The sad thing ni kwamba Mbowe alishindwa kujibu mashumbulizi hayo.<br />
<br />
..tusimdharau Ndugai, he can do some damage to CDM's image and reputation. tusisahau kwamba he comes across as an innocenct, calm, and collected individual.
Hivi Ndugai ndio mkurugenzi wa SFO?Ndugae yuko fiti nyie, hamkumbuki alivyojitahidi sana kuwashawishi waingereza waturudishie chenji!!!!!!!!!!!!!1
TAASISI ya Vox Media Centre Tanzania na East Africa Business and Media Training Institute (EABMTI) kwa ushirikiano na kituo cha Star TV kesho wataendesha mdahalo wa kibunge, mada ni Bunge la 10 na Tanzania tunayoitaka. Taarifa kwa vyombo vya habari iliyopatikana Dar es Salaam jana kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Vox Media, Ansbert Ngurumo, inaeleza kuwa mdahalo huo utafanyika kwenye ukumbi wa Mtakatifu Gaspar mjini Dodoma.
Kwa mujibu wa Ngurumo katika taarifa hiyo, wazungumzaji wakuu kwenye mdahalo huo ni Naibu Spika Job Ndugai na Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani, Tundu Lissu, huku wananchi 200 wakipata nafasi ya kuwauliza maswali; mdahalo huo utarushwa hewani kuanzia saa 12:00 jioni hadi saa 1:50 usiku. Inaelezwa kwenye taarifa hiyo kuwa ni fursa nyingine kwa wananchi kujadili masuala nyeti yanayohusu uhai wa taifa kwa kumulika, kuhoji na kutafakari namna Bunge linavyowawakilisha.
Ni fursa yetu kupima utendaji wa wabunge na kuhoji kama wanakoelekea ndiko tunakopaswa ni fursa pia kwa wazungumzaji wetu kusisitiza yanayopaswa na kukosoa yanayopotoshwa au kukosewa kuhusu Bunge, ni fursa kwa wabunge kujipima kwa maoni ya wananchi, ilieleza sehemu ya taarifa hiyo. Katika mdahalo huo Mkurugenzi Mtendaji wa EABMTI, Rosemary Mwakitwange, ataongoza mdahalo huo kwa kushirikiana na wajumbe wengine wa taasisi hizo. Mwaka jana taasisi hizo ziliaandaa midahalo kadhaa wakati wa kampeni kuelekea Uchaguzi Mkuu iliyohusu wagombea urais wa Tanzania.
Tanzania Daima
<br /><font color="#a52a2a"><b>Lissu hana ubavu kwa Ndugai, ni mgeni mno kwenye siasa. Na isitoshe Ndugai ni BOSS wa lissu</b></font>
Leo nimemsikia huyu Ndugai akitoa matangazo kikao cha asubuhi leo...amedai na hapa namnukuu...."KATIKA MECHI HII NAIBU SPIKA AMEKWISHA SHINDA" mwisho wa kunukuu....Yani huyu kilaza atapambana na Tundu mwanasheria aliyebobea,great thinker...Ndugai saizi yake ni akina Simbachawene,Kingwangala,Lusinde na vilaza wengine..........mtaona ukilaza wa huyu naibu spika wenu.....