MTAZAMO
JF-Expert Member
- Feb 8, 2011
- 19,643
- 33,439
Wakuu,
Jana ulifanyika mjadala mzuri ulioandaliwa na mediabrains lakini uliokosa balance nzuri ya watu waliostahili kuwa sehemu ya panel ile lakini hasa kukosa muda wa kutosha kudadavua mkataba wenyewe.
Sasa tunashauri Mediabrains waandae mdahalo mwingine ambao utajikita kwenye kuuchambua mkataba wenyewe bila kupoteza muda na mada za udini, uzanzibar n.k
Tunaomba huo mjadala washiriki watu waliojipambanua vizuri kuusoma na kuuchambua huo mkataba ili hoja zao zijibiwe na serikali wakisaidiwa na akina Kitila na Rostam! ikiwezekana spika Tulia pia.
Wafuatao waitwe kuwasilisha mada za kupinga huu mkataba 1) Tundu Lissu 2) Dr Slaa 3) Prof Tibaijuka 4) Dr Lwaitama 5) Advocate Mwabukusi 6) Prof Lipumba
Tuwe na mjadala wa siku nzima kwa faida ya Taifa ili wote tuelewe. Tulitegemea mjadala utakaokata kiu zetu kupitia bunge lakini uliishia kuwa mjadala wa upande mmoja na mipasho na imechangia kuchochea hofu kwa wananchi.
Mediabrains representative brother Kibanda na Prof Kitila kwavile umejipambanua kupenda midahalo tunaomba mdahalo huu haraka tufunge mjadala na kutoa mapendekezo.
Mdahalo uwe live kwenye media kubwa zote.
Jana ulifanyika mjadala mzuri ulioandaliwa na mediabrains lakini uliokosa balance nzuri ya watu waliostahili kuwa sehemu ya panel ile lakini hasa kukosa muda wa kutosha kudadavua mkataba wenyewe.
Sasa tunashauri Mediabrains waandae mdahalo mwingine ambao utajikita kwenye kuuchambua mkataba wenyewe bila kupoteza muda na mada za udini, uzanzibar n.k
Tunaomba huo mjadala washiriki watu waliojipambanua vizuri kuusoma na kuuchambua huo mkataba ili hoja zao zijibiwe na serikali wakisaidiwa na akina Kitila na Rostam! ikiwezekana spika Tulia pia.
Wafuatao waitwe kuwasilisha mada za kupinga huu mkataba 1) Tundu Lissu 2) Dr Slaa 3) Prof Tibaijuka 4) Dr Lwaitama 5) Advocate Mwabukusi 6) Prof Lipumba
Tuwe na mjadala wa siku nzima kwa faida ya Taifa ili wote tuelewe. Tulitegemea mjadala utakaokata kiu zetu kupitia bunge lakini uliishia kuwa mjadala wa upande mmoja na mipasho na imechangia kuchochea hofu kwa wananchi.
Mediabrains representative brother Kibanda na Prof Kitila kwavile umejipambanua kupenda midahalo tunaomba mdahalo huu haraka tufunge mjadala na kutoa mapendekezo.
Mdahalo uwe live kwenye media kubwa zote.