Kwenye tawi moja la KCB kuna dada mmoja alikuwa ananirudishia excess kila nikipeleka hela inakuwa inazidi 20 sometimes mpka 40 hivi. Nikawa natulia sana wakati wa ku count ili niwe na uhakika, sikuwa nafikiria vibaya maana ni hela ya company. Sasa ikafika mda nikiiingia tu pale bank tellers wananiambia nenda pale kwa huyo dada nikawa na wasi wasi sana. Siku nikaangia sikumkuta ma teller wengine wakanihudumia kimya kimya. Nikamuuliza security wa pale akaniambia yule dada ameacha kazi ila akawa anacheka cheka, nikayaacha kama yalivyo. Baada ya miezi kadhaa nipo office nasikia kuna mgeni wako kuchungulia ni yule dada wa KCB nikamchangamkia sana, saa saba hio mchana tukaenda kula lunch ndio akanipa story yake kuwa anafanya biashara zake na anamshukuru Mungu zinaenda vizuri yupo pale anataka kununua mzigo amepungukiwa na laki 2, roho ikafanya paaaa!! nimpe nisimpe? nikaendaa ATM nikampa laki na nusu akashukuru na ahadi kunirudishia within 3 days, akarejesha kweli!! mwisho nikaja kugundua kumbe alinizimikia sana. Mkuu na wao ni binaadamu wanapenda pia. Tongoza mkuu lakini uwe na nia ya kuoa tu