Kuna mchungaji alikuwa akihubiri kanisani akisema Mtu atakayetenda mema siku ya kwenda mbinguni atakwenda kwa ndege. Sasa ikafika siku ya kwenda mbinguni, jamaa mmoja akafanikiwa kwenda kwa ndege. Wakiwa wanaendelea na safari jamaa akatazama chini kupitia dirishani, lahaula akamuona mchungaji akiwa anaenda mbinguni kwa GARI. Jamaa akamuuliza mchungaji imekuwaje anakwenda kwa GARI inamaana hakuwa akitenda yale anayohubiri, mchungaji akamjibu afadhali yangu mimi nimepanda gari hebu mtazame Askofu nyuma yangu, alipotizama alimuona Askofu akiwa anakwenda kwa BAISKELI.