Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
Na Elizabeth Suleyman
MCHUNGAJI wa Kanisa la Tanzania Assembles of God (Tag) Macmilan Lyimo
MCHUNGAJI wa Kanisa la Tanzania Assembles of God (Tag), lililoko eneo la Mabibo jijini Dar es Salaam Macmilan Lyimo, jana alitangaza nia yake ya kumvaa Rais Jakaya Kikwete, katika uchaguzi mkuu ujao unaotarajia kufanyika Oktoba mwaka huu.
Alisema lengo lake ni kutaka kupata uongozi na kuasisi taifa jipya la Tanzania na kwamba kizazi cha walioleta uhuru yaani Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimeshamaliza muda wake, na ni vyema kikaondolewa kutokana na kushindwa kuleta maendeleo hapa nchini.
Lyimo ambaye alisema atagombea nafasi ya urais kupitia tiketi ya Chama cha Tanzania Labour Party (TLP) kinachoongozwa na Mwenyekiti Augustine Mrema, aliliambia gazeti la Mwananchi jana katika mahojiano maalumu yaliyofanyika ofisini kwake kwamba, nia ya kugombea ni kuasisi taifa jipya la Tanzania litakalokuwa na misingi inayokubalika na lenye mueleleko wa kisasa.
Ukiangalia siasa ya sasa hivi imeshaingia doa, kutokana na wanaoshikilia nafasi hizo kuivuruga na matokeo yake, Tanzania inakuwa na siasa chafu ya watu kulala makaburini, kwenda kwa waganga, na kufanya mambo ya kishirikina, lengo ni kutaka tu! kupata nafasi ambazo zina maslahi yao binafsi, alisema Lyimo.
Alisema cha kushangaza viongozi waliotokana na mfumo wa kuleta uhuru zaidi ya miaka 50 iliyopita, bado wanaendelea kutembeza mabakuli na hakuna jitihada zozote ambazo wamezifanya, badala yake nchi inaishia kuingia katika dimbwi la ufisadi.
Chanzo: Gazeti la Mwananchi
MCHUNGAJI wa Kanisa la Tanzania Assembles of God (Tag) Macmilan Lyimo
MCHUNGAJI wa Kanisa la Tanzania Assembles of God (Tag), lililoko eneo la Mabibo jijini Dar es Salaam Macmilan Lyimo, jana alitangaza nia yake ya kumvaa Rais Jakaya Kikwete, katika uchaguzi mkuu ujao unaotarajia kufanyika Oktoba mwaka huu.
Alisema lengo lake ni kutaka kupata uongozi na kuasisi taifa jipya la Tanzania na kwamba kizazi cha walioleta uhuru yaani Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimeshamaliza muda wake, na ni vyema kikaondolewa kutokana na kushindwa kuleta maendeleo hapa nchini.
Lyimo ambaye alisema atagombea nafasi ya urais kupitia tiketi ya Chama cha Tanzania Labour Party (TLP) kinachoongozwa na Mwenyekiti Augustine Mrema, aliliambia gazeti la Mwananchi jana katika mahojiano maalumu yaliyofanyika ofisini kwake kwamba, nia ya kugombea ni kuasisi taifa jipya la Tanzania litakalokuwa na misingi inayokubalika na lenye mueleleko wa kisasa.
Ukiangalia siasa ya sasa hivi imeshaingia doa, kutokana na wanaoshikilia nafasi hizo kuivuruga na matokeo yake, Tanzania inakuwa na siasa chafu ya watu kulala makaburini, kwenda kwa waganga, na kufanya mambo ya kishirikina, lengo ni kutaka tu! kupata nafasi ambazo zina maslahi yao binafsi, alisema Lyimo.
Alisema cha kushangaza viongozi waliotokana na mfumo wa kuleta uhuru zaidi ya miaka 50 iliyopita, bado wanaendelea kutembeza mabakuli na hakuna jitihada zozote ambazo wamezifanya, badala yake nchi inaishia kuingia katika dimbwi la ufisadi.
Chanzo: Gazeti la Mwananchi