kabila01
JF-Expert Member
- Apr 21, 2009
- 4,235
- 4,949
Kwa miaka takribani 10 iliyopita nilikua sijawahi kusikia sauti ya mbunge wa jimbo langu ikisikika bungeni. Sijutii uamuzi wangu na gharama nilizozitumia kusafiri kutoka Kigoma hadi Iringa kwenda kumpigia kura Mchungaji Peter Msigwa. Wiki iliyopita nimeenda Iringa Municipal nimeshangaa kukuta barabara inayokuja mtaani kwetu ikiwekwa Lami na nilipofika mtaani hadi wale akina mama wa hali ya chini wakizinguliwa kidogo tu na maafisa watendaji wanaandamana kwenda kusemelea kwa mchungaji Msigwa ambaye ndiye mtetezi wao. Kuna wazee wengine maeneo ya Mkimbizi na Kihesa kilolo walidhulumiwa viwanja vyao wakaenda kumwambia mchungaji Msigwa nae amewapigania hadi ardhi yao na haki yao wameipata. Tupo pamoja Mchungaji Msigwa ukitoka bungeni usisahau kuja kuongea na wananchi utupe feedback ya huko mjengoni na usikilize kero zetu. Iringa kwa sasa ni wajanja wamekubali mabadiliko na hili liwe Funzo kwa majimbo mengine yaliyobaki katika mkoa wa Iringa