Mchumba wangu ni mbinafsi na bahili sana

Mchumba wangu ni mbinafsi na bahili sana

Joined
Jun 13, 2015
Posts
7
Reaction score
1
Habari wana jamii,

Mimi ni msichana wa miaka 29 naishi Morogoro nafanya kazi katika Taasisi fulani ya fedha nina mchumba ambae tuna mahusiano huu mwaka wa tatu sasa.Tumebarikiwa kupata mtoto mmoja wa kiume bado mdogo, mwenzangu anafanya kazi Dar es salaam. Kikubwa kilichonifanya niombe ushauri ni kuwa mwenzangu anajipenda sana namaanisha vitu vyake ni vyake pekeake ila vyangu tutumie wote.

Sio kwamba hana pesa, hapana ana hela nyingi na tumefanikiwa kufanya investments nyingi ila pesa yote anashika mwenzangu. Kifupi ni mchungu na mbahili sana hata kwangu na mwanangu. Ukizingatia ameshanitolea mahari kwetu tupo kwenye taratibu za ndoa. Kiukweli uwa inaniumiza sana hadi nawaza niahirishe hiyo ndoa.

Naombeni ushauri wadau
 
Mmmmh pole mkuu...mi hapa ntakuwa msomaji tu
 
Wachaga ndivyo walivyo!

Mmmh mkuu why are u generalise :what::what:

Hiyo no hulka na moyo wa mtu ulivyojijenga na si kabila , kabila linahusiana nini na Roho ya kibinafsi na na uchoyo :what::what::what: think twice
 
Kaa chini uongee nae, asipokuelewa ita wazee wake na wako na akiwa bado mbishi Nakushauri uwe na subira kuingia katika ndoa na huyo jamaa.
Kuna vitu unaweza kudhani ni vidogo ukavipuuzia sasa lakini baadae vikawa chanzo cha kuiona ndoa chungu
 
Whats bad na kibaya kabisa investments nimefanya mm mwenyewe ata kabla cjapata ajira aisee kabadilika yan tuongee stori nyingine sio pesa
 
Hivi ninyi bhuwa mnasoma mada kweli?

Halafu kuna mtu amekugongea "LIKE" .....

Mungu atusaidie sana na hii nchi ....

Hebu tazama hapa chini kwenye red ..
Habari wana jamii mm ni kijana wa miaka 29 naishi Morogoro nafanya kazi katika Taasisi fulan ya fedha nina mchumba ambae tuna mahusiano huu mwaka wa tatu sasa.

Tumebarikiwa kupata mtoto mmoja wa kiume bado mdogo,mwenzangu anafanya kaz Dar es salaam.

Kikubwa kilichonifanya niombe ushauri ni kuwa mwenzangu anajipenda sana namaanisha vitu vyake ni vyake pekeake ila vyangu tutumie wote.

Sio kwamba hana pesa, Hapana ana ela nyingi na tumefanikiwa kufanya investments nyingi ila pesa yote anashika mwenzangu.

Kifupi ni mchungu na mbaili sana hata kwangu na mwanangu. Ukizingatia ameshanitolea mahari kwetu tupo kwenye taratibu za ndoa.

Kiukweli uwa inaniumiza sana hadi nawaza niairishe hiyo ndoa.

Naombeni ushauri wadau.
 
Kaa chini uongee nae, asipokuelewa ita wazee wake na wako na akiwa bado mbishi Nakushauri uwe na subira kuingia katika ndoa na huyo jamaa.
Kuna vitu unaweza kudhani ni vidogo ukavipuuzia sasa lakini baadae vikawa chanzo cha kuiona ndoa chungu

Nimeshawaambia wazee pande zote anaelewa kwa muda afu anarud pale pale amenichosha kabisa
 
Kaa chini uongee nae, asipokuelewa ita wazee wake na wako na akiwa bado mbishi Nakushauri uwe na subira kuingia katika ndoa na huyo jamaa.
Kuna vitu unaweza kudhani ni vidogo ukavipuuzia sasa lakini baadae vikawa chanzo cha kuiona ndoa chungu
Unajua nilitaka kumshauri huyu dada lakini naona hata maana ya ndoa hajui ....

Kuna mambo mtu unapaswa kuyajua kwanza kabla ya kufikiria ndoa sasa huyu naona kama bado kabisa .....

Yaani mtu hataki muwe kitu kimoja kwenye suala la muhimu kama pesa halafu unataka kuingia nae kwenye ndoa?

Inashangaza sana......!!
 
Back
Top Bottom