Mchumba wangu na mke wa mtu wamenitenda

Mchumba wangu na mke wa mtu wamenitenda

chabby chubby

Member
Joined
Aug 7, 2015
Posts
11
Reaction score
4
Habari wana jf. Naombeni ushauri wenu kwani nipo njia panda na maumivu makali mno moyoni. Mm ni binti nilikua na mpenzi wangu tumedumu miaka 4 na mwaka Jana mwishoni alikuja hom kwa wazazi kujitambulisha but suddenly mwaka huu January alibadilika sana na akanipiga stop kwenda kwake akinidanganya kuna wageni so yeye ndio atakua akinifuata mm,basi tukaendelea ivyoivyo huku mapenzi yake kwangu yakiwa yamepungua kwa kiasi kikubwa ila nikimuuliza anadai ananipenda Sema anabanwa tu na mishe. Binafsi nikaamua kumfatilia kimyakimya nikaja gundua ana mwanamke anayemchanganya,pale kwake anapoishi kuna Mpangaji mwenzake wa kike sasa mdogo wa yule Dada ndio anatoka na mpenzi Wangu na wanaishi kama mke na mume. Nilimwambia mpenz Wangu tuachane lakini aligoma katakata tena kwa machozi juu lakini hapohapo akawa ananipangia muda wa kumpigia cm yani mm nisimpigie mpaka yeye apige wala nisiweke kitu chochote dp whatsp kitakochoonyesha kua mm na yeye bado ni wapenzi kiukweli nilishtuka nikamuuliza kwanini akanijibu nimpe muda ataachana na yule mwanamke. Kichwa changu kilifanya kazi nikagundua hapa napotezwa maboya huyu anaonekana anampenda sana uyo mwanamke so nikaamua liwalo na liwe lakini kabla ya kufanya lolote nikamuweka kikao huyu mchumba Wangu nikambembeleza sana tuachane tu kwa amani kwani nafahamu hajiwezi kwa uyo mwanamke mpya lakini alikataa katakata tena akilia kua ananipenda nimpe tu muda me nikaona huu ujinga sasa,alipoondoka tu nikaweka picha dp nilizopiga naye na status nzuri mpango wako ukatiki yule mwanamke akaona(ieleweke nilifanya hv ili achague moja kwani wkt huo nilikua nimechanganyikiwa sn nilimpenda sn mchumba Wang) jamani siku hiyo nilijutaaa sikuamini macho Yangu walinipigia cm wakanitukana mnoo,mchumba Wangu alinigeuka mbele ya yule mwanamke kama hanijui alinitukana me Malaya sina bwana niche kumng'ang'ania yani mengine Naona aibu kuandika..wanapokezana tu kunitusi mm nikamjibu tu mchumba wangu asante nashukuru..sasa basi nikaja kugundua kwa uchunguzi Wangu binafsi yule mwanamke kumbe ni mke wa mtu na amezaa watoto watatu na mumewe ila kwasasa mumewe yupo nje ya nchi kimasomo huyu x Wangu hajui kitu yeye amedanganywa kua wameshaachana na mumewe..jamani huyu mwanamke pamoja na kwamba nimeshaachana na uyo x Wangu lakini ananitukana mno mpaka kesho Mimi Hi mkimya siwezi kujibishana nae namwangalia tu..sasa jamani naombeni ushauri wenu nimsaidieje uyu x Wangu kwani namuonea huruma sana mke wa mtu ni sumu na pia Nina no ya mume wa yule Dada..kuna siku alinitukana nikashikwa na hasira kwanini still ananifuatilia wakati nimesha accept the fact sitakiwi tena basi nilitaka kumtext mumewe nimueleze madudu ya mkewe lakini nikajizuia nikajisemea kisasi ni cha Mungu. Naumia sn uyu mwanamke anavyonifatilia nifanyeje Mimi? Naumia mchumba Wangu kunigeuka tena kwa matusi na kashfa kisa mke wa mtu.
 
Achana nao, Mungu atadeal nao kwa wakati wake. Wewe cha kufanya ni kutoa sadaka ya shukrani, tubu na umuombee na ujiombee Mungu akuponye majeraha waliokusababishia. Ukiona unasindwa uombe nini, muombe Mungu aingilie kati na mapenzi yake yatimizwe na usisahau kutoa sadaka.
 
1: usishindane na mjinga, 2: seems unampenda jamaa ako bt yet u can let him go

MUHIMU: holding onto smthng is like holding onto your own breath, u will suffocate. the only way of getting smthng u deserve into this physical world is by letting go of the past...
TAKE IT FRM ME: I LOST the one person i've truly loved n simply by letting GO of her i gained smthng much better, SELF RESPECT.. let him gO trust me u'll gain smthng much better.
NB: LEARN HOW TO BE OKY WITHOUT HIM
 
Badili phone number x wako na huyo mpenz wee wasikuone mengn achana nayo uzuri una busara
 
Achana nao na uendelee na maisha yako. Ila nikushauri kitu kimoja. Kuna wakati inabidi kuamua kufanya maamuzi mapema ili kujipunguzia maumivu. Kama ulishapata ukweli kuwa mchumba wako anaishi na mtu mwingine, ni bora ungeendelea na maisha yako tu, maana mtu kama yuko teyari kukuacha wewe mchumba wake uteseke na kuumia rohoni, kisa hataki kumuumiza mwingine inamaanisha thamani yako kwake imeshuka kulinganisha na huyo anaemlinda. Maana mwanaume anaekupenda kwawaida anahakikisha anakulinda na kila jambo linaloweza kukuumiza.
 
Habari wana jf. Naombeni ushauri wenu kwani nipo njia panda na maumivu makali mno moyoni. Mm ni binti nilikua na mpenzi wangu tumedumu miaka 4 na mwaka Jana mwishoni alikuja hom kwa wazazi kujitambulisha but suddenly mwaka huu January alibadilika sana na akanipiga stop kwenda kwake akinidanganya kuna wageni so yeye ndio atakua akinifuata mm,basi tukaendelea ivyoivyo huku mapenzi yake kwangu yakiwa yamepungua kwa kiasi kikubwa ila nikimuuliza anadai ananipenda Sema anabanwa tu na mishe. Binafsi nikaamua kumfatilia kimyakimya nikaja gundua ana mwanamke anayemchanganya,pale kwake anapoishi kuna Mpangaji mwenzake wa kike sasa mdogo wa yule Dada ndio anatoka na mpenzi Wangu na wanaishi kama mke na mume. Nilimwambia mpenz Wangu tuachane lakini aligoma katakata tena kwa machozi juu lakini hapohapo akawa ananipangia muda wa kumpigia cm yani mm nisimpigie mpaka yeye apige wala nisiweke kitu chochote dp whatsp kitakochoonyesha kua mm na yeye bado ni wapenzi kiukweli nilishtuka nikamuuliza kwanini akanijibu nimpe muda ataachana na yule mwanamke. Kichwa changu kilifanya kazi nikagundua hapa napotezwa maboya huyu anaonekana anampenda sana uyo mwanamke so nikaamua liwalo na liwe lakini kabla ya kufanya lolote nikamuweka kikao huyu mchumba Wangu nikambembeleza sana tuachane tu kwa amani kwani nafahamu hajiwezi kwa uyo mwanamke mpya lakini alikataa katakata tena akilia kua ananipenda nimpe tu muda me nikaona huu ujinga sasa,alipoondoka tu nikaweka picha dp nilizopiga naye na status nzuri mpango wako ukatiki yule mwanamke akaona(ieleweke nilifanya hv ili achague moja kwani wkt huo nilikua nimechanganyikiwa sn nilimpenda sn mchumba Wang) jamani siku hiyo nilijutaaa sikuamini macho Yangu walinipigia cm wakanitukana mnoo,mchumba Wangu alinigeuka mbele ya yule mwanamke kama hanijui alinitukana me Malaya sina bwana niche kumng'ang'ania yani mengine Naona aibu kuandika..wanapokezana tu kunitusi mm nikamjibu tu mchumba wangu asante nashukuru..sasa basi nikaja kugundua kwa uchunguzi Wangu binafsi yule mwanamke kumbe ni mke wa mtu na amezaa watoto watatu na mumewe ila kwasasa mumewe yupo nje ya nchi kimasomo huyu x Wangu hajui kitu yeye amedanganywa kua wameshaachana na mumewe..jamani huyu mwanamke pamoja na kwamba nimeshaachana na uyo x Wangu lakini ananitukana mno mpaka kesho Mimi Hi mkimya siwezi kujibishana nae namwangalia tu..sasa jamani naombeni ushauri wenu nimsaidieje uyu x Wangu kwani namuonea huruma sana mke wa mtu ni sumu na pia Nina no ya mume wa yule Dada..kuna siku alinitukana nikashikwa na hasira kwanini still ananifuatilia wakati nimesha accept the fact sitakiwi tena basi nilitaka kumtext mumewe nimueleze madudu ya mkewe lakini nikajizuia nikajisemea kisasi ni cha Mungu. Naumia sn uyu mwanamke anavyonifatilia nifanyeje Mimi? Naumia mchumba Wangu kunigeuka tena kwa matusi na kashfa kisa mke wa mtu.

Kama wamemwaga mboga wewe mwaga ugali.... Yanini uteseke peke yako ... Hebu kinukishe fasta kwa huyo mume kama unaogopa niambie nikusaidie
 
Unaumia wewe lakini unamuonea huruma anayekuumiza. . . . . .!!!!

Ni ngumu sana kupotezea kama mtu mlizoeana na unamfahamu a to z na unaona anapotea, hata kama unaumia vipi unapata huruma na kutaka kumsaidia especially km una hofu ya Mungu
 
The way I see it, huyo mwanamke has much more to loose than ex wako so you're better off dealing with her directly. Mimi ningemwambia moving forward it is her responsibility to ensure that you are left alone in peace . Any word from her or huyo jamaa yake (your ex) then mumewe will know everything.
 
Achana nao, Mungu atadeal nao kwa wakati wake. Wewe cha kufanya ni kutoa sadaka ya shukrani, tubu na umuombee na ujiombee Mungu akuponye majeraha waliokusababishia. Ukiona unasindwa uombe nini, muombe Mungu aingilie kati na mapenzi yake yatimizwe na usisahau kutoa sadaka.

Atoe sadaka baada ya kufanya uasherati kwa miaka minne? Hiyo sadaka ya shukrani anamtolea nani??
 
We dada unamwonea huruma mtu aliyempenda na akakuumiza wakati yeye hana mpango na wewe?jamani si wanawake hatujipendi au ni nini.wewe inabidi uwablock wote uangalie maisha yako.jionee huruma mwenyewe kwa kupoteza miaka minne kwa huyo mtu.move on dada muda haurudi juma.kilasiku nasema wanawake tuwe na misimamo umeshasema mmeachana sasa ya nini kuendelea kuwasiliana nae?jiamini na kuwa na msimamo acha umama huruma.
 
Ni ngumu sana kupotezea kama mtu mlizoeana na unamfahamu a to z na unaona anapotea, hata kama unaumia vipi unapata huruma na kutaka kumsaidia especially km una hofu ya Mungu

ni ngumu kupotezea lakini sio kumwonea huruma mtu aliyekuchelewesha miaka minne na kukuumiza juu.
 
Dada yani halo jibu rahisi kabisa usiruhusu nafsi kuteseka maana kuteseka kwa nafsi ni sawa sawa jeraha la kidonda... chakufanya achana nae kamwe hata kama akirudi kuomba msamaha jasiri aachi asiri nmemaliza kwa maelezo mengine nitafute kwenye PM
 
Back
Top Bottom