chabby chubby
Member
- Aug 7, 2015
- 11
- 4
Habari wana jf. Naombeni ushauri wenu kwani nipo njia panda na maumivu makali mno moyoni. Mm ni binti nilikua na mpenzi wangu tumedumu miaka 4 na mwaka Jana mwishoni alikuja hom kwa wazazi kujitambulisha but suddenly mwaka huu January alibadilika sana na akanipiga stop kwenda kwake akinidanganya kuna wageni so yeye ndio atakua akinifuata mm,basi tukaendelea ivyoivyo huku mapenzi yake kwangu yakiwa yamepungua kwa kiasi kikubwa ila nikimuuliza anadai ananipenda Sema anabanwa tu na mishe. Binafsi nikaamua kumfatilia kimyakimya nikaja gundua ana mwanamke anayemchanganya,pale kwake anapoishi kuna Mpangaji mwenzake wa kike sasa mdogo wa yule Dada ndio anatoka na mpenzi Wangu na wanaishi kama mke na mume. Nilimwambia mpenz Wangu tuachane lakini aligoma katakata tena kwa machozi juu lakini hapohapo akawa ananipangia muda wa kumpigia cm yani mm nisimpigie mpaka yeye apige wala nisiweke kitu chochote dp whatsp kitakochoonyesha kua mm na yeye bado ni wapenzi kiukweli nilishtuka nikamuuliza kwanini akanijibu nimpe muda ataachana na yule mwanamke. Kichwa changu kilifanya kazi nikagundua hapa napotezwa maboya huyu anaonekana anampenda sana uyo mwanamke so nikaamua liwalo na liwe lakini kabla ya kufanya lolote nikamuweka kikao huyu mchumba Wangu nikambembeleza sana tuachane tu kwa amani kwani nafahamu hajiwezi kwa uyo mwanamke mpya lakini alikataa katakata tena akilia kua ananipenda nimpe tu muda me nikaona huu ujinga sasa,alipoondoka tu nikaweka picha dp nilizopiga naye na status nzuri mpango wako ukatiki yule mwanamke akaona(ieleweke nilifanya hv ili achague moja kwani wkt huo nilikua nimechanganyikiwa sn nilimpenda sn mchumba Wang) jamani siku hiyo nilijutaaa sikuamini macho Yangu walinipigia cm wakanitukana mnoo,mchumba Wangu alinigeuka mbele ya yule mwanamke kama hanijui alinitukana me Malaya sina bwana niche kumng'ang'ania yani mengine Naona aibu kuandika..wanapokezana tu kunitusi mm nikamjibu tu mchumba wangu asante nashukuru..sasa basi nikaja kugundua kwa uchunguzi Wangu binafsi yule mwanamke kumbe ni mke wa mtu na amezaa watoto watatu na mumewe ila kwasasa mumewe yupo nje ya nchi kimasomo huyu x Wangu hajui kitu yeye amedanganywa kua wameshaachana na mumewe..jamani huyu mwanamke pamoja na kwamba nimeshaachana na uyo x Wangu lakini ananitukana mno mpaka kesho Mimi Hi mkimya siwezi kujibishana nae namwangalia tu..sasa jamani naombeni ushauri wenu nimsaidieje uyu x Wangu kwani namuonea huruma sana mke wa mtu ni sumu na pia Nina no ya mume wa yule Dada..kuna siku alinitukana nikashikwa na hasira kwanini still ananifuatilia wakati nimesha accept the fact sitakiwi tena basi nilitaka kumtext mumewe nimueleze madudu ya mkewe lakini nikajizuia nikajisemea kisasi ni cha Mungu. Naumia sn uyu mwanamke anavyonifatilia nifanyeje Mimi? Naumia mchumba Wangu kunigeuka tena kwa matusi na kashfa kisa mke wa mtu.