Mchezo wa draft

Mimi ni nomaa kwa mchezo wa draft kama kuna mtaalamu mwingine aombe mechi na mm nina michezo 5 ya hatari
 
Juma mchafu amefariki aisee...
R.I.P.
 
Hao wote mliowasema hawajui kitu, kuna kichwa kinaitwa Msundafilo ni hatari tupu, kete tatu ashakumaliza
 
drafti ni kujua copy tu. kuna namna saba za kuanza game na zote zina majina. ni namna mbili tu unaweza kushinda kama unacheza na mafundi. kuanza na kete ya kati wanaita oldfaithful na kuanza na kete ya kwenye kona wanaita double corner. namna zingine zote ukikutana na anayejua copy atakukimbiza sana. nilijifunza hizi copy na counter zake hata miezi sita siku hizi napiga drafti kila mtu anashangaa. zamani nilikuwa naendaenda bila copy nilikuwa napigwa sana japo ilinisaidia uzoefu ikitokea mtu ametoka nje ya copy. mchezo poa sana huu.
 
Unapocheza draft zingatia hesabu ya steps (hatua), yaani kabla haujasukuma kete jiulize kuwa nikisukuma hapa yeye atacheza vipi kuhusu hiyo kete? UNAWEZA KUWA UMEPUNJWA KETE (Mfano wewe una kete 4 yeye 5 au 6) HALAFU BADO UKAMFUNGA AU DROO
 
Niliowahi kucheza nao, wanakijua kiwango changu.
Ni mchezo mzuri ambao inabidi ubadilishe mbinu kwa kadri ya mpinzani wako anavyocheza.
Kwa sehemu kubwa,unahitaji kulinda na kushambulia kwa akili kubwa sana.
 
Njia rahisi ya kushinda huu mchezo unaenda mbele na kete tatu tatu. Lakini hivi juzi nilikutana na jamaa alikua na mchezo wake unaitwa ebola. Alinipiga nne firster mpaka nimejiuliza. Ni mchezo mzuri
Ni mchezo mzuri sana
 
Nchi nyingi wanacheza draft la kwenda mbele na nyuma, lakini kwa Tanzania yapo ya aina mbili, kuna hilo la mbele na nyuma na kuna la mbele tu

We ni mtaalamu wa lipi?
Binafsi yote nacheza...lile la two way linaitwa French kwa kuwa limeibuliwa Ufaransa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…