Mchechu, kama umeshindwa kazi utoke

Mchechu, kama umeshindwa kazi utoke

Aisee sijaelewa malengo ya kufanya hivyo kama ni kwenda kuangalia micholo wale ni wakandarasii wameenda wamepiga pesa tuu
 
Mkuu eddy
watanzania tunachekesha satellite city at kawe!!? mi nimeona ile taarifa hao waheshimiwa sana wamepelekwa kuonyeshwa huo mji mpya ulipo, ni nje mbali na Abu dhabi,

Mmkuu Me Hata Sijaelewa Hiyo Fisibility Study Ya Kawe Imefanywaje, Ivi Kwanini Wang'ang'anie Maeneo Yenye Msongamane Kama Kawe? Maeneo Kama Ya Pande Kule, Kinakojengwa Kile Chuo Cha Afya Kule, Pia Kuna Chanika Kule Nk Kuna Maeneo Ya Maana Kwanini Wasingejenga Miji Mipya Ya Kisasa Wakapeleka Huduma Za Maana Za Kijamii.Wanakimbilia Kugombana Na Watu Kule Kawa Hata Fidia Hawalipi.
 
Mashirika yanayoonesha kufa hamyapigii kelele. Yenye matumaini mwataka ianze migogoro. Aibu sana.
 
support aliyopewa mchechu na IKULU mtu yeyote humu JF angepewa NHC ingekuwa zaidi ya hii ya MCHECHU. Nilishasema na narudia kusema MCHECHU ni MZIGO kama walivyo mizigo mingine kama Eng Kipande, Maingu wa PSPF, Mafuru wa Hazina, na January makamba N waziri

Acha wivu kaka, chapa kazi kama Mchechu......watu kama hawa wanahitaji support yenu ili wafanye zaidi ya hapo. Watz kama wewe hawapendi kuona mchapa kazi bali wala rushwa na wavivu kazini ndiyo wajanja.!!!
 
Nadhani mleta mada unamaanisha Mchechu na si Msechu. Kama ni huyo, mwache afanye kazi. Usilete fitna kama za Tibaijuka. Mchechu ni presidential material.

Kitu ambacho hukijui ni kwamba NHC kuonekana walau inafanya kazi ni kwa sababu ya mama Tiba

Mama Tiba alikua na mtazamo mpana na kuona mambo nje ya box...exposure yake ilimsaidia

Bila Tibaijuka sasa subiri uone yatakayotokea NHC.

Yule mama pamoja na madhaifu yake lakini ni mchapa kazi
 
Nadhani mleta mada unamaanisha Mchechu na si Msechu. Kama ni huyo, mwache afanye kazi. Usilete fitna kama za Tibaijuka. Mchechu ni presidential material.

Mkuu, watz ni sheeeda hawataki kuona mchapa kazi....wamezoea kuona na kupongeza wapiga dili na wazembe
 
Misingi ya NHC iliwekwa na magufuli alivyokuwa waziri wa ardhi na mzee ole madeye akiwa MD wa NHC, yeye kabebwa na mbeleko bado hakuna anacho deliver, matangazo chungu mzina nyumbanyumba hamnakitu, ona nyumba zinazojengwa monduli hovyo tu tangu lini gorofa likawa la matofari ya kuchoma hata timbiktu wasingejenga hivi, kama kweli alikuwa anania ya kujifunza angeenda Israel akaona wayahudi wanavyojenga makazi ukingo wa gaza, ipo haja ya kuajiri MD kutoka Israel.
Qater kila mtu ananyumba wanachojenga ni vitega uchumi vya kibiashara tena vya kimataifa sisi hata pakuishi ni shida, eti anaenda kujifunza huko kama sio ndoto za abunuwasi ni nini? kwahiyo hayo mabembea ndo walienda kujifunza kwani fancity hayapo?

Hawahawa walipelekwa na tibaijuka Hongkong hadi wengine wakapigana bar bado hawakuelewa, basi sikuingine tumpeleke profesa Muhongo kama hao akina lembeli ni nanga.
Ndugu unahitaji kuombewa mapepo yakutoke. tangu lini ole medeye amekuwa MD wa NHC? hujawahi kuona ghorofa ya tofari za hydraform hapa nchini? kama mshamba si vizuri ukajionesha ushamba wako....
 
Mmkuu Me Hata Sijaelewa Hiyo Fisibility Study Ya Kawe Imefanywaje, Ivi Kwanini Wang'ang'anie Maeneo Yenye Msongamane Kama Kawe? Maeneo Kama Ya Pande Kule, Kinakojengwa Kile Chuo Cha Afya Kule, Pia Kuna Chanika Kule Nk Kuna Maeneo Ya Maana Kwanini Wasingejenga Miji Mipya Ya Kisasa Wakapeleka Huduma Za Maana Za Kijamii.Wanakimbilia Kugombana Na Watu Kule Kawa Hata Fidia Hawalipi.

Mkuu mi nashindwa kuwaelewa hawa viongozi wetu wanafikra zipi,wanakwenda kuangalia mfano wa mji, huko walipotoka wameona mji mpya umeanzishwa mbali na mji wa zamani,ule mji wa zamani unaachwa intact hauguswi zaidi wanaulinda,wakirudi hapa wana bomoa mji wa zamani kujenga mji mpya amazing! lakini hivi katika dunia ya leo kuona mfano wa ujenzi wa miji mizuri ni lazima kamati ya Bunge isafiri kwenda kuona are we serious?
 
Nilitegemea niwaone wanapewa maelekezo na waziri wa makazi au meyor wa jiji au maofisha wa huo mji lakini naona wadogo tu wa NHC wakiwasomesha sasa kulikuwa na sababu gani ya kwenda huko? Wakati anasign mkopo wa dola billioni hakuwa amefanya survey ya kutosha? kwa hiyo wanataka kujenga kama joberg doha hongkong? kama hawajui wanataka kufanya nini basi wangezurura kwanza kabla ya kuomba mkopo,

Mkapa kabla ya kuanzisha mradi wa DART alileta consultant kutoka brazil, akafanya upembuzi yakinifu na proposal, kwa msechu lembeli ndo consultant au? Haya Mnyika na uhandisi majengo wapi na wapi?
Nehemiah Mchechu Kyando usijali ndugu yangu, nabii hakubaliki kwao, piga mzigo kijana, huyu Eddy anaweza kuwa mhanga wa reformed NHC, mazuri hatupendi kuyaona! Sijui tumerogwa na Nani?
 
anatumia pesa nyingi kuwalipa wabunge ili wamtetee bungeni lakini hamna chochote kama kujifunza angeondoka na wataalamu wa ardhi au wanafunzi wa uhandisi hivi ndivyo namna wabunge wanavyotafuna pesa na kushindwa kusimamia mashirika ya umma angalia makampuni binafsi yanavyojenga majengo halafu linganisha na nyumba za nhc
 
support aliyopewa mchechu na IKULU mtu yeyote humu JF angepewa NHC ingekuwa zaidi ya hii ya MCHECHU. Nilishasema na narudia kusema MCHECHU ni MZIGO kama walivyo mizigo mingine kama Eng Kipande, Maingu wa PSPF, Mafuru wa Hazina, na January makamba N waziri

Huu ni wivu wa kike! Vijana pendaneni na pigeni mzigo, kulalamika hakutatusaidia kitu, tutoe challenges au constructive criticism, siyo kashfa kila kukicha!
 
Nyuma ya Mchechu halisi ni nani? Na huku sio kuongeza deni la Taifa ? Kama anafanya bila hila tumpongeze ila binafsi nina doubts.
 
Kitu ambacho hukijui ni kwamba NHC kuonekana walau inafanya kazi ni kwa sababu ya mama Tiba

Mama Tiba alikua na mtazamo mpana na kuona mambo nje ya box...exposure yake ilimsaidia

Bila Tibaijuka sasa subiri uone yatakayotokea NHC.

Yule mama pamoja na madhaifu yake lakini ni mchapa kazi
Mambo ya Nje ya box yamepitwa na wakati, siku hizi unatakiwa kufikiri bila ya uwepo wa box,
 
JK kakubeba kwa mbeleko hadi china kakutafutia mkopo wa dola billioni, ili uje utujengee nyumba sasa badala ya kujenga umeanza semina elekezi na akina lembeli, ulikuwa hongkong juzi africa ya kusini mala doha sasa mko brunei sijui Qater, hao akina lembeli ubunge ulishakwisha huko kote unafanyanao nini? nilitegemea kukuona una sign mikataba na wakandarasi kuanza ujenzi maramoja.

Kiwanja kawe ulishapewa, fedha unazo, michoro unayo sasa tatizo liko wapi? kama huwezi kudeliver utoke waje wenye huo uwezo. Sasa nakubaliana na Zitto kuwa uwezo wako wa kazi ni mdogo, leo nimeona ITV mko sijui nchi gani huko uarabuni haya munashangaa magorofa tu hamkuwa na mwenyeji hata mmoja, kujifunza gani bila kupata maelezo kutoka kwa mwenyeji.
Acha wivu wa ki@@#$ juhudi zote a nazo fanya bado tu huna shukrani
 
Aende kwa ALHAJI DAU PALE NSSF AKALISHWE KITAKO AELEKEZWE KAZI

KAZI NI VITENDO SIYO MANENO MATUPU HAINA MAANA

PESA ZA WALALAHOI ZINAPASWA KUWEKEZWA KATIKA MAMBO YENYE TIJA NA YANAYOONEKANA

dawa ni kupiga chini tu huyu jamaa tulete Myahudi mmoja atuchapie kazi, sasa nakubaliana na zitto kuwa NHC hawana ubavu wa kutujengea makazi bora.
 
Speaking of unfinished business,after conspiring against Maige,Kagasheki,Tibaijuka and Muhongo now you're after Mchechu head.Sadly you're satisfied with incompetency of such officials as Saada Mkuya,Pinda,Kawambwa, Malima,Kombani and the list goes on...oh yeah it's Tanzania's mentality whereby the hardwory,visionary and ethical people are being hated to death!
 
hili.shirika ndio walau shirika la umma linajiendeshe lenyewe tena kwa faida ninamshangaa sana mtu akimpiga madongo msechu....


_shukrani za pekee sana sana zimwendee yule waziri mstaafu ambeye ni mbuge wa huko singida jina limenitoka.

aliyewatimua wanyonyaji waliokuwa wamechukua nyumba za nhc na kuzipangisha kwa bei ya juu na sasa nikiwemo mimi nalipa moja kwa moja kodi ya kibanda changu kwa shirika

mh chiligati
 
Back
Top Bottom