Mchango watangazaji RTD ni wa kutukuka

Mchango watangazaji RTD ni wa kutukuka

Juma nkamia enzi hizo anatangaza mpira
Tumetoka mbali
 

Hujamtaja Christine Chakunegela (usomaji wake taarifa ya habari saa nne usiku ilikuwa kama vile ni software, hakuna kigugumizi wala kurudiarudia maneno)

Hebu tujuze kila mmoja alipo sasa, maana hawa watangazaji walikuwa na kiswahili kilichotukuka kisicho na doa

Pascal Mayalla, alitokea RTD!
Ingependea awe anatumegea siri ya nini walikuwa wanafanya mpaka kuwa kivutio sana kwenye ubora wa lugha ya Kiswahili
Pascal Mayalla

Juma Nkamia (rubbish)
Huyu ametukuka kwako mleta mada
Umeniamsha usingizini mkuu huyo mtu uliyemtaja mwanzo achaaaa usiguse hicho kitufe ni hatati yaani danger namaanisha. Huo usomaji wake wa taarifa ya habari na ile sauti havijawah kutokea kwenye sayari hii labda huko mars.


Nyakati zinakimbia sana.
 
MBAZIGWA HASSAN,
H.MCHUKA,
J..NKAMIA,
EZEKIEL MILONGO,
TIDO MHANDO,
SHABAN KISSU.
Na wengine wengi. Enzi hizo mpira wa Simba na Yanga tunatangaziwa na Juma Nkamia alafu anakwambia wao bila sisi moja.......!!!! SAA moja na nusu usiku kipindi cha michezo hunibandui......... Kusikiliza habari za Said Maulid(SMG), Emanuel Gabriel,Joseph Kaniki,Atuman Machupa, Juma Kaseja, Said Sued, na wachezaji wengine wengi.......
 
Umeniamsha usingizini mkuu huyo mtu uliyemtaja mwanzo achaaaa usiguse hicho kitufe ni hatati yaani danger namaanisha. Huo usomaji wake wa taarifa ya habari na ile sauti havijawah kutokea kwenye sayari hii labda huko mars.


Nyakati zinakimbia sana.
Hv jina lake kwa usahh ni lipi haswa naona kila mtu anaandika kivyake humu. I mean spelling zake. Dah RTD acheni tu
 
Umeniamsha usingizini mkuu huyo mtu uliyemtaja mwanzo achaaaa usiguse hicho kitufe ni hatati yaani danger namaanisha. Huo usomaji wake wa taarifa ya habari na ile sauti havijawah kutokea kwenye sayari hii labda huko mars.


Nyakati zinakimbia sana.


Hivi alipotelea wapi?
Alitakiwa kuwa anarithisha hiyo karama, ni nadra sana kukutana na watu wa aina yake.
 
Wachafuzi wa lugha

Siku hizi tbc wengi wababaishaji. Nimesema wengi. Sio wote! Huyo Enock ana pompous mnoooooo hadi anakirihisha. Ajifunze kwa akina Sued Mwingi na Kisu ambao siku zote wako composed
 
Christine Chokunogela bado yupo tbc katika ubora wake. Katika niliowasahau yupo pia Eshe Muhidini. Huyu nae ni bonge la mtangazaji mahiri. Anaijua kazi yake vizuri mno. Utampenda.
Katika ambao bado wapo sasa vichwa ni Kissu, Mwinyi, Alecia Maneno, Eshe, Chokunogela, yule wa kipindi cha hotuba za Mwalimu nk. Nasema hizi ni lulu au tuseme 'unsung heroes and heroines'
Akina Neema Mwasyoghe na Agness Mbapu nao wanajitahidi kutangaza kwa umakini.
 
Utakuwa humtendei haki Dominick Chilambo wa RTD Mwanza na mmoja wa manguli wa kutangaza mpira kutokea uwanja wa CCM Kirumba..

Vinginevyo orodha imetimia.
Apumzike kwa amani. nakumbuka alifariki siku moja na mke wa Mzee Kawawa mama Sophia Kawawa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom